Jengo la kihistoria la Mahakama ya Rufaa litabomolewa kupisha upanuzi wa hoteli ya zamani ya Kilimanjaro Kempinski ambayo imebadilishwa jina hivi karibuni na kuitwa Hyatt Regency – Kilimanjaro. Jengo hilo lilikuwa linatambulika kama jengo la kihitoria kupitia Gazeti la Serikali Namba 498 la mwaka 1995. Hata hivyo serikali imeamua kutolitambua jengo hilo tena kama la kihistoria
Hata hivyo, baadhi ya watu wanalalamika kuwa kuvunjwa kwa jengo hilo la kihistoria kutaadhiri mwonekano ya Kivukoni Front ambapo pia kuna majengo mengine ya kihistoria yakiwemo yale ya Mahakama Kuu, Tanzania Bureau of Statistics na Mahakama Kuu ya Biashara. Msemaji kutoka Wizara Utalii na Maliasili ambaye hakutaka jina lake litajwe ameliambia gazeti la Daily News kuwa serikali imekubali mmiliki wa eneo la hoteli ya Hyatt Regency – Kilimanjaro kubomoa jengo hilo la kihistoria na kujenga jengo jipya ili kupanua hoteli hiyo. Jengo jipya litakuwa na presidential suites nyingi.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Bw. Rutabanzibwa, amesema amesikia mpango wa kuboa hilo jengo hilo lakini bado hajataarifiwa kiofisi. Hata hivyo, amesema ingekuwa vizuri kama jengo hilo lingebakia kama lilivyo ili kuendana na plan ya jiji la Dar Es Salaam. Msemaji mwigine ndani ya wizara hiyo amesema kama jengo hilo la kihistoria litabomolewa, basi itabidi majengo mengine ya kihistoria nayo yabomolewe.
Alipoulizwa Waziri wa Wizara ya Utalii na Maliasili, Mh. Ezekiel Maige, alisema taarifa zote zinapatikana kwa katibu wake, Bi. Maimuna Tarishi. Alipofuatwa Bi. Tarishi alisema atatoa habari kimaandishi. Afisa Mawasiliano wa hoteli ya Hyatt Regency anayejulikana kwa jina moja Nasra alipoulizwa alisema hana mamlaka ya kuongelea hili suala.