Hyatt Yatangaza kufungua Hoteli Mpya huko Cape Town, kuna watu kama nawaona

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,432
7,055
Inaonekana South Afrika panalipa! Jamaa wamefungua hoteli yao ya pili kwenye Jiji la Jo'berg. Sisi tunaotarajia kuanza kusafiri safiri lazima tukatesti mitambo kuona yaliyomo kama yamo kweli!

Kiukweli inapendeza kuona uwezekezaji mkubwa hivi unafanyika katika sekta hii ya utalii na ukarimu. Natamani jamaa huko mbeleni waongeze nyingine hapa hapa Bongo manake vyuma vinaweza kulegea huko tuendako. Well, ngoja tuendelee tu kuzichanga changa aisee!

Kuna watu fulani tutarajie kuwaona wakisafiri sana baada ya uchaguzi na corona kupita. Wanajulikana wazee wa 'misele' ya kutafuta wadhamini. Si ajabu tukaanza kuona video za Bongo Fleva zinaanza kushutiwa tena kwa wingi Sauzi.

Simo!
-----------

Kampuni ya Hyatt inayomiliki Hoteli za hadhi ya Kimataifa saba Barani Afrika kufungua Hoteli nyingine jijini Cape Town, Afrika Kusini Mwezi Desemba mwaka huu. Hoteli hiyo mpya itakayokuwa na jumla ya vyumba 137 itakuwa ni ya nane Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambapo mbili zitakuwa nchini Afrika Kusini.

1603481455822.jpeg

Muonekano wa vyumba wa Hyatt Hotel Cape Town

Hyatt imeingia makubaliano ya uendeshaji wa Hoteli hiyo mpya na Kampuni ya Majengo, Millat Properties ya Afrika Kusini. Bara la Afrika hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara inatajwa kama moja ya maeneo ambayo yanaonyesha matumaini ya mazingira mazuri ya kibiashara hivyo hali hiyo imeifanya Kampuni ya Hyatt kuliweka eneo hilo kama eneo lake la kimkakati.
Pia eneo la Kusini mwa Janga la Sahara ni kati ya maeneo yenye vivutio vingi vya Utalii na huvutia idadi kubwa ya wageni kutoka Bara la Ulaya na Marekani kuja kutembelea vivutio hivyo. Takwimu zinaonyesha kuwa kipindi cha janga la Corona, idadi ya Watalii wa Kimataifa imekuwa kwa asilimia 6 Kusini mwa Janga la Sahara kinyume na matarajio, ambapo idadi hiyo haikutarajiwa.

Jiji la Cape Town

Cape Town ambapo Hoteli hiyo ya Hyatt itafunguliwa ndio jiji la pili linaloongoza kwa idadi kubwa ya watu baada ya Johannesburg nchini Afrika Kusini. Vilevile, ni mji wa kwanza ulioanzishwa katika eneo la Afrika Kusini hivyo huitwa mara nyingi "Mji Mama" wa nchi. Kihistoria mji ulianzishwa kama kituo cha mapumziko kwenye njia ya safari za meli kati ya Uholanzi na makoloni yake huko Asia, hasa Indonesia ya leo.

Cape Town pia ndimo kuna jengo la Bunge la Taifa hilo tajiri Barani Afrika. Mwaka 2014, jiji la Cape Town lilitajwa kama sehemu bora zaidi duniani ya kutembelea na magazeti mawili ya The New York Times na The Daily Telegraph.

Cape Town pia huvutia matukio ya kimichezo makubwa duniani, mfano imewahi kuwa mwenyeji wa kombe la dunia la mwaka 1995 la mchezo wa Rugby na pia Kombe la Dunia la Soka mwaka 2010.

Pia jiji la Cape Town linasifika kwa fukwe nzuri zenye kuvutia na upepo mwanana ambapo idadi kubwa ya watalii hufika kuzitembelea hasa kipindi cha kiangazi.
Takwimu zinaonyesha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town hupokea wageni milioni tano kwa mwaka, pia husifika kwa maeneo ya kupumzika na starehe kwa watu wanaokuwa kwenye mapumziko.

Makamu wa Rais anayehusika na Maendeleo wa Hyatt Barani Afrika na Mashariki ya Kati amesema, “Tunafuraha kufanya kazi na Millat Properties kuileta Hyatt Cape Town, kama eneo lenye kuvutia wasafiri wengi ni lengo letu kubwa kuwa na Hoteli ya Hyatt Cape Town na tunaamini kuna uwezekano wa kukua zaidi nchini Afrika Kusini. Hyatt Regency Cape Town ni mkakati wetu wa kukua kwenye soko ambalo tunajua wageni wetu hutembelea.”

Hoteli hiyo ya Hyatt Regency Cape Town itakuwa katika eneo maarufu la Mlima Meza (Table Mountain) ambalo ni maarufu kwa kuvutia watalii.

1603481456133.jpeg

Muonekano wa nje kutoka ndani ya Hyatt Hotel Cape Town

Kampuni ya Millat Properties itahusika kwenye kuitengeneza kisasa hoteli hiyo mpya kwa ndani kabla haijafunguliwa rasmi. Pia itatumia wabunifu wa viwango vya kimataifa ili kuifanya hoteli hiyo kuwa na muonekano mzuri wenye hadhi.

Hoteli hiyo itakuwa na jumla ya vyumba 137, ikiwemo 15 vyenye hadhi ya rais (Presidential Suites), pia vyumba maalumu vya kufanyia mazoezi vyenye vifaa vya kisasa na eneo kwa ajili ya kuogelea kwa nje. Kwa wageni ambao watafika kwa ajili ya mikutano imeandaliwa eneo lenye mita za mraba 400 mahususi kwa shughuli hizo.

Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini Mmamoloko Kubayi-Ngubane amesema kuwa habari ya kufunguliwa kwa hoteli mpya ya Hyatt Afrika Kusini ni njema kwa utalii wa taifa hilo ambalo ni miongoni mwa nchi za uchumi mkubwa zaidi barani Afrika na kitovu cha utalii.

’Habari kuwa hoteli ya Hyatt itafunguliwa ndani ya jiji la Cape Town ni njema kwa sekta ya utalii, n ani kiashiria chema kinachoonesha kufufuka kwa sekta ya usafiri na utalii’’,
Waziri Mmamoloko amesema.

‘’Kama ilivyo kwa sehemu nyingine nyingi nchini kwetu, Cape Town ni ya kipekee kweli, ikiwapatia wageni uzoefu ambao hautasahaulika na uzuri wa asili na vivutio vya kutembelea. Hyatt Regency Cape Town itakuwa nyongeza kamili kwa sekta ya ukarimu katika jiji hili la kihistoria'', Mmamoloko ameongeza.

Taarifa hizi za kufunguliwa kwa Hoteli hii Afrika Kusini zinakuja wakati tayari Hyatt ina Hoteli za kisasa ambazo ni Hyatt Regency Johannesburg, Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kilimanjaro na Hyatt Regency Addis Ababa. Nyingine mbili zinatarajiwa kufunguliwa ndani ya miaka mitatu ijayo, ambazo ni Hyatt Regency Nairobi, Kenya na Hyatt Regency Lagos Ikeja, Nigeria.

CHANZO: Hyatt Yatangaza kufungua Hoteli Mpya Jijini Cape Town
 
Back
Top Bottom