Jenerali Ulimwengu, njoo kivingine!

Jenerali Ulimwengu, njoo kivingine!

Nashukuru kwa link na ukweli wenyewe nilishaisoma kwenye the East African.
Suala lenyewe sasa. Kwa uelewa wangu au upeo wangu wa lugha ya malkia, Ulimwengu hakumpigia chapuo EL katika makala hiyo. Kinyume chake anakejeli iweje mposaji atoe mgodi wa dhahabu wakati baba mkwe mtarajiwa anataka ng'ombe wawili tu wa kulimia?

Sure, the article was ironical! Nitashangaa sana kama Lowassa aliipenda hii article. Ilikuwa ni kejeri iliyoandikwa kwa lugha ya upole.
 
meningitis

Kweli shule za kata zineteremsha kiwango cha elimu. Meningitis hakuwa mlengwa wa ile makala, hata ukirudi english course haitakusaidia labda usome literature 2
 
Last edited by a moderator:
Nadhani ni ushauri wa busara sana kama mleta mada akienda pale british council itamsaidia sana ...
 
Ni mwaka wa uchaguzi ambapo tunategemea na kutarajia watu muhimu au viongozi au waandishi kuchukua na kuupamba upande wanaouamini au kutegemea maslahi.

Kuna mada iliwahi kuonekana humu jamvini lakini ilipotea kwa bahati mbaya.

Mada hiyo ilionya waandishi wa habari kutohadaa wananchi juu ya nani anayekubalika na kuwa mgombea wa urais.Mada hii ilikumbushia madhara ya wanahabari kuwaaminisha watanzania kuwa huyu ndiye kumbe ni bomu.sijui mada hiyo imepotelea wapi ndio maana nimeleta mada hii hapa jamvini.

Jenerali Ulimwengu mwandishi mkongwe na mwenye heshima katika tasnia ya uandishi na serikali na nchi hii au East Africa kwa ujumla.

Mwandishi huyu aliitumia kalamu yake na ujuvi wake wa Serikalini kutushawishi watanzania, wazalendo, CCM na Team Lowassa kuwa EL ndiye mgombea anayekubalika na ni mgombea sahihi.

Kazi hii aliifanya kwa ustadi mkubwa kwa kutumia lugha ya na platform za kilami kujaribu kuuza jina la EL.Inawezekana aliifanya kazi hii kwa utashi au kwa kuhongwa lakini tunamshukuru Mungu kuwa amemuumbua!

Ulimwengu alitoa articles mbili ninazozikumbuka na kuziona hapa JF zote zikituaminisha madudu au hadaa kwamba EL ndio. Nashukuru responce ya wanaJF zilikuwa chache pengine ni ku-ignore au ignorance ya members wa wakati huu.

Jishughulisheni kuzitafuta articles hizo humu JF mtanielewa naongelea nini.Sasa ombi langu kwa comrade Ulimwengu ni kuja kivingine kama ataweza au kununuliwa!

Nataka azithibitishe articles zake kwa kuhakikisha CCM inadondoka kwa kuwa maoni yake yake yalikuwa sahihi pole natoa kwa wazee wote wa vibahasha!

Kama ilivyo vitani, waandishi wa habari ndio huwa wahanga wa kwanza kwa kuficha ukweli na ndivyo ilivyo pia kwenye siasa. Waandishi wetu, kwa kuwinda vihela vya wagombea ndio wamekuwa wahanga wa makundi yanayovutana kisiasa. Si hela tu lakini siku hizi wanasiasa wamegundua mbinu mpya, kuwapa vyeo waandishi. Utaona kila mgombea ana kakundi kake ka waandishi na ndio hutumika kugawa rushwa, hapana, wenyewe huita posho. Sasa wamehamia kwa Magufuli, kila mmoja ana matumaini ya kupata U-DC au kacheo kokote ili mradi agange njaa kwa muda na kusahahu machungu yake ya maisha. Lowassa alikuwa na kundi kubwa la waandishi,tena wenye heshima zao. Sasa wamehama wanatafuta boss mpya! Ila sidhani, kama Jenerali yumo katika kundi la waandishi wa kundi kama hilo.
 
Kwahiyo mimi nikikwambia kwamba mimi ndiyo BABA yako, na wewe utakwenda kuandika hivyo? "By JK Nyerere"
Tumia quote ya Mtu mahali stahiki na katika issue zinazoendana , mleta mada pamoja na wewe mna haki ya kukubali ya Jenerali au kuyakata kwa facts na kwa kuelewa Maana ya makala yake , zaidi ya hapo issue ya Nyerere was base on conclusion ya mwandishi kwa jinsi alivyo muuliza mwl lile swali, makala ya Jenerali haikuwa conclusive kwamba El atapita , ilikuwa juu ya vyombo husika kuchukua taadhari ikiwemo wewe Mpiga kura
 
Acha Uongo, Raia Mwema muda wote halikuwa kwa Mamvi, hata kubenea kuna kipindi aliyumba akawa anaandika mbinu za kumkata Lowassa kwa njia ya kulaumu au kufichua mbinu. GENERALI Ulimwengu muda wote hajawahi kuwa kwa Lowassa, Kibanda ndo alihama kabisa Tanzania Daima akaenda kwa Bashe Habari corporation ili atumike vizuri. MUNGU kaipenda zaidi nchi

Uko sahihi
 
hahaaa! eti mwl can't stop him this time. now Kanali Kikwete stop him.

Ninao wasiwasi kuwa hujaipata vizuri maana halisi ya hiyo sentensi; pengine unajaribu kuilewa kutokana na maneno moja moja yaliyomo ndani yake. Maana yake hasa ni kukejeli watu wanaoamini kuwa maadam Nyerere hayupo tena, basi njia iko wazi!
 
Ukitaka kuwapumbaza watanzania basi waeleze katika lugha ya malkia.

intention ya Ulimwengu ilikuwa ni nini hasa?

Ni kweli Ulimwengu na Unguli wake katika siasa na uandishi aliamini kuwa Lowassa ndiye?

Ni kweli Lowassa alikuwa anakubalika?

Kwa nini Ulimwengu ali-miss hii fact ya kwamba EL Hakubaliki bali ni show tu za kwenye TV lakini kwenye field sio hivyo.

Siamini mimi na wengine humu JF tulikuwa ni wajuvi kuliko Ulimwengu.

Hebu tazama Mzee Mwanakijiji alovyotoa maoni yake tulipokuwa tunaelekea uteuzi wa ccm ndio ujiridhishe kuwa Ulimwengu alikuwa na lake jambo.

mkuu meningitis,bado hutaki kuelewa unayofafanuliwa na watu wanaokielewa kile mzee Ulimwengu anachoandika kwa lugha ya malkia?Basi inawezekana hata akiandika kwa lugha yetu adhimu ya kiswahili huwezi kumuelewa kamwe.
usione aibu kukubali kuwa una shida ya kuelewa maandiko yake,iwe maudhui ama lugha anayoitumia.
 
Last edited by a moderator:
Ni mwaka wa uchaguzi ambapo tunategemea na kutarajia watu muhimu au viongozi au waandishi kuchukua na kuupamba upande wanaouamini au kutegemea maslahi.

Kuna mada iliwahi kuonekana humu jamvini lakini ilipotea kwa bahati mbaya.

Mada hiyo ilionya waandishi wa habari kutohadaa wananchi juu ya nani anayekubalika na kuwa mgombea wa urais.Mada hii ilikumbushia madhara ya wanahabari kuwaaminisha watanzania kuwa huyu ndiye kumbe ni bomu.sijui mada hiyo imepotelea wapi ndio maana nimeleta mada hii hapa jamvini.

Jenerali Ulimwengu mwandishi mkongwe na mwenye heshima katika tasnia ya uandishi na serikali na nchi hii au East Africa kwa ujumla.

Mwandishi huyu aliitumia kalamu yake na ujuvi wake wa Serikalini kutushawishi watanzania, wazalendo, CCM na Team Lowassa kuwa EL ndiye mgombea anayekubalika na ni mgombea sahihi.

Kazi hii aliifanya kwa ustadi mkubwa kwa kutumia lugha ya na platform za kilami kujaribu kuuza jina la EL.Inawezekana aliifanya kazi hii kwa utashi au kwa kuhongwa lakini tunamshukuru Mungu kuwa amemuumbua!

Ulimwengu alitoa articles mbili ninazozikumbuka na kuziona hapa JF zote zikituaminisha madudu au hadaa kwamba EL ndio. Nashukuru responce ya wanaJF zilikuwa chache pengine ni ku-ignore au ignorance ya members wa wakati huu.

Jishughulisheni kuzitafuta articles hizo humu JF mtanielewa naongelea nini.Sasa ombi langu kwa comrade Ulimwengu ni kuja kivingine kama ataweza au kununuliwa!

Nataka azithibitishe articles zake kwa kuhakikisha CCM inadondoka kwa kuwa maoni yake yake yalikuwa sahihi pole natoa kwa wazee wote wa vibahasha!

Sijajua kwa nn mtu kama Generali ulimwengu mtu mwenye maono aliamua kuwaandikia watanzania ujinga na upumbavu kama huo,sijui lini watanzania wataacha kununuliwa kama bidhaa Sokoni,nina hakika Mwl.Nyerere angekuwepo angewashangaa watu sana ambao alijua wana akili kumbe ni mazuzu na mazezeta kama JU,unawezaje kumtaja mwizi na kumpamba na kuwaaninisha watanzania kuwa ndiye anayefaa kuwa Rais hali mtu huyo akiwa tayari amelisababishia Taifa hasara.
USHAURI: Waandishi tubadilike na Tusinunuliwe na daima tuandike ukweli utakao lisaidia Taifa na wala unafiki usipate nafasi kamwe.
 
Sasa kama kiswahili tu Jenerali watu wengi hawamuelewi
itakua Kiingereza?

Kusema Jenerali anamsapoti Lowassa ni kumtukana

English kwa kweli ni janga la taifa....
 
Sijajua kwa nn mtu kama Generali ulimwengu mtu mwenye maono aliamua kuwaandikia watanzania ujinga na upumbavu kama huo,sijui lini watanzania wataacha kununuliwa kama bidhaa Sokoni,nina hakika Mwl.Nyerere angekuwepo angewashangaa watu sana ambao alijua wana akili kumbe ni mazuzu na mazezeta kama JU,unawezaje kumtaja mwizi na kumpamba na kuwaaninisha watanzania kuwa ndiye anayefaa kuwa Rais hali mtu huyo akiwa tayari amelisababishia Taifa hasara.
USHAURI: Waandishi tubadilike na Tusinunuliwe na daima tuandike ukweli utakao lisaidia Taifa na wala unafiki usipate nafasi kamwe.

Kuna watu humu wanaponda sana kwamba hatukijui kimombo....hahaha mimi nakubali lakini hawajajibu hoja ya msingi kwamba kusudio la mwandishi lilikuwa ni nini?

Ndio maana alikuja kimalkia zaidi ili awashike wengi wanaodhani wanakifahamu king'eng'e.

EL ndio kakatwa sasa tumsubiri Ulimwengu atatuambia nini.
 
Ninao wasiwasi kuwa hujaipata vizuri maana halisi ya hiyo sentensi; pengine unajaribu kuilewa kutokana na maneno moja moja yaliyomo ndani yake. Maana yake hasa ni kukejeli watu wanaoamini kuwa maadam Nyerere hayupo tena, basi njia iko wazi!
mkuu unaweza kuwa sahihi lakini hiyo ni tafsiri yako. mimi nimeeleza kilichoandikwa. usilete yale mambo ya sekondari kuwa fasihi ni koti 'jadili' humu
 
Sasa kama kiswahili tu Jenerali watu wengi hawamuelewi
itakua Kiingereza?

Kusema Jenerali anamsapoti Lowassa ni kumtukana

English kwa kweli ni janga la taifa....

Kuna njia nyingi za kumtukana mtu. Mmojawapo ndiyo hii inatumika kumtukana Ulimwengu. Not in a million years Ulimwengu atamsapoti Laigwanani.
 
Acha Uongo, Raia Mwema muda wote halikuwa kwa Mamvi, hata kubenea kuna kipindi aliyumba akawa anaandika mbinu za kumkata Lowassa kwa njia ya kulaumu au kufichua mbinu. GENERALI Ulimwengu muda wote hajawahi kuwa kwa Lowassa, Kibanda ndo alihama kabisa Tanzania Daima akaenda kwa Bashe Habari corporation ili atumike vizuri. MUNGU kaipenda zaidi nchi
Hakika wewe ndiye nakuamini, yani Gen . Ulimwengu asifie fisadi, hakika angefanana na Zitto.
 
Siasa za makundi au kutengamana zilishamgharimu sana Gen Ulimwengu mpaka akafurumishwa. Hawezi kurudia tena. Mfano Banyamlenge/ Kagame vs Joseph Kabila vs JK nk.
 
Kuna njia nyingi za kumtukana mtu. Mmojawapo ndiyo hii inatumika kumtukana Ulimwengu. Not in a million years Ulimwengu atamsapoti Laigwanani.

Kukosolewa sio kutukanwa mkuu!
 
Back
Top Bottom