Jenerali Muhoozi: Uganda ipo tayari kuisaidia Israel

Jenerali Muhoozi: Uganda ipo tayari kuisaidia Israel

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Muhoozi Kainerugaba, amesema nchi hiyo ipo tayari kujiingiza katika mgogoro wa Mashariki ya Kati ikiwa kutakuwa na jaribio lolote la kuiangamiza Israel.

Kupitia mtandao wa Machi 25, 2026, Muhoozi alieleza wazi msimamo huo:

"Mazungumzo yoyote ya kuangamiza au kuipiga Israel yatatuingiza vitani (upande wa Israel)."

Hata hivyo, ameongeza kuwa wanatamani vita vinavyoendelea katika eneo hilo vikome haraka:

"Tunataka vita vya Mashariki ya Kati vikome sasa. Dunia imechoshwa navyo."


IMG_1341.jpeg
Mgogoro huo unahusisha United States na Israel dhidi ya Iran pamoja na kundi la Hezbollah, hali inayozidi kuongeza taharuki kimataifa.

Muhoozi, ambaye ni mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amewahi mara kadhaa kutoa kauli zenye utata mtandaoni kuhusu masuala ya kijeshi na siasa za kimataifa, baadhi zikizua mjadala mkubwa kabla ya kufutwa au kufafanuliwa baadaye.

Kauli yake ya hivi karibuni imeongeza mjadala kuhusu nafasi ya Uganda katika siasa za kimataifa na ushiriki wake katika migogoro ya nje ya bara la Afrika.
 
Muhoozi, ambaye ni mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amewahi mara kadhaa kutoa kauli zenye utata mtandaoni kuhusu masuala ya kijeshi na siasa za kimataifa, baadhi zikizua mjadala mkubwa kabla ya kufutwa au kufafanuliwa baadaye.
Akishalewa awe anapokonywa simu, madhara ndio haya sasa ila hapo shida sio bia shida ni yeye maana ukishalewa kila unachosema ni ukweli ukilewa huwezi kusema uongo.
Cc:
Nikilewa mniache
 
Huyu jamaa na baba yake waliwahi kusema kuwa Kenya ni sehemu ya Uganga.
Hhivyo walikuwa na mpango kukomboa maeneo yao ya kijografia ili waipate bandari za Mombasa na Lamu..
Nadhani project hiyo ni muhimu kwao kuliko kujaribu kucheza na Persian.
 
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Muhoozi Kainerugaba, amesema nchi hiyo ipo tayari kujiingiza katika mgogoro wa Mashariki ya Kati ikiwa kutakuwa na jaribio lolote la kuiangamiza Israel.

Kupitia mtandao wa Machi 25, 2026, Muhoozi alieleza wazi msimamo huo:

"Mazungumzo yoyote ya kuangamiza au kuipiga Israel yatatuingiza vitani (upande wa Israel)."

Hata hivyo, ameongeza kuwa wanatamani vita vinavyoendelea katika eneo hilo vikome haraka:

"Tunataka vita vya Mashariki ya Kati vikome sasa. Dunia imechoshwa navyo."
View attachment 3562786
Mgogoro huo unahusisha United States na Israel dhidi ya Iran pamoja na kundi la Hezbollah, hali inayozidi kuongeza taharuki kimataifa.

Muhoozi, ambaye ni mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amewahi mara kadhaa kutoa kauli zenye utata mtandaoni kuhusu masuala ya kijeshi na siasa za kimataifa, baadhi zikizua mjadala mkubwa kabla ya kufutwa au kufafanuliwa baadaye.

Kauli yake ya hivi karibuni imeongeza mjadala kuhusu nafasi ya Uganda katika siasa za kimataifa na ushiriki wake katika migogoro ya nje ya bara la Afrika.
Na hili ni kichaa na kesho linarithi urais wa baba yake.
 
Kama ni mwanaume,basi ni wakati sasa wa kutuma drones na makombora iran ili kuiokoa israel, yaani miafrika shida tupu.
 
Muhoozi atawakasirisha kobazi, bora uganda imejiweka wazi ipo upande gani kwenye mnyukano wa mashariki ya kati
 
Muhoozi Kainerugaba, mwana wa rais wa muda mrefu wa Uganda, Yoweri Museveni na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda (UPDF):

"Tunataka vita vya Mashariki ya Kati viishe sasa. Dunia imechoka navyo. Lakini mazungumzo yoyote ya kuiangamiza au kuinyonghonyeza Israeli yatatuingiza vitani sisi tukiwa Upande wa Israeli!"
 

Attachments

  • IMG_20260326_065332_021.jpg
    IMG_20260326_065332_021.jpg
    59.8 KB · Views: 1
"Tunataka vita vya Mashariki ya Kati viishe sasa. Dunia imechoka navyo. Lakini mazungumzo yoyote ya kuiangamiza au kuinyonghonyeza Israeli yatatuingiza vitani sisi tukiwa Upande wa Israeli!"
Iran asije akatupa Kombora kuelekea UG
 
Back
Top Bottom