Je wewe ni mwandishi wa ICT ??

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Hi Wadau .

Kwa mara ya kwanza napenda kuulizia waandishi wa tekinologia na ICT waliopo Tanzania au afrika ya mashariki , kuna mambo napenda kuongea nao mmoja mmoja au kama ni kundi au kikundi kipo sehemu Fulani .

Najua pengine wako lakini hawapendi kujitokeza au waandikia sehemu ambazo binafsi sijawahi kusoma au kuchangia lakini wasiogope au wasiwe na choyo ya kuonana angalau mara moja katika maisha yao .

Kama wewe ni mwandishi unahusika na masuala ya tekinologia na ICT naomba tuwasiliane naamini pamoja tutaweza kwenda mbele na kuendeleza fani hii pamoja na wengine ambao wanapenda kuona maendeleo Fulani Fulani yanafikiwa katika afrika ya mashariki .

Hata kama wewe ni mwanafunzi hii ni fursa yako pia unaweza kuwasiliana nasi , piga simu au beep tutakupigia au andika ujumbe mfupi sms zote zitajibiwa na kupanga jinsi ya kuonana na wewe popote ulipo ndani ya afrika mashariki .

Tafadhali unaweza kuwasiliana ni kwa namba +255784 360204 au email mwanahabari@gmail.com unapopiga au kuandika email uwe huru tu jisikie ko nyumbani usiogope chochote wala kuwa na wasi wasi wowote najua wengi ni waoga na hawajiamini kuanzia leo jiamini basi .

Nakukumbusha italeta faida sana kwako wewe mwandishi na nchi yako au katika jamii unayotoka kama tukifanikiwa kukutana na kuongea mambo mbali mbali sikumoja tuwe katika mkutano wa pamoja kutunga sera za pamoja zilizo na masilahi ya afrika mashariki yetu .

Karibu sana

Piga + 255784 360204 ( Celtel ) au Email : mwanahabari@gmail.com waambie na wenzako waambie wote ambao unawajua .
 
Kwa mara ya kwanza napenda kuulizia waandishi wa tekinologia na ICT waliopo Tanzania au afrika ya mashariki , kuna mambo napenda kuongea nao mmoja mmoja au kama ni kundi au kikundi kipo sehemu Fulani .

Maelezo ya ziada yanahitajika, kwa mfano una maanisha nini unaposema waandishi wa Tekinoloji na ICT? Je, una maana ya waandishi wa habari wanaoandika habari za Tekinolojia na habari za mawsiliano ya tekinolojia (ICT)kwenye magazeti? au una maana ya wataalamu wa Tekinolojia na Mawasiliano ya kompyuta kama vile Systems Administrator, Systems Analysts, Programmers,Database Administrators, Web designers n.k? au wanaondika habari kwa kutumia nyenzo za komputa na makandokando yake kwa mfano, bloggers, wiki n.k.?

Tafadhali fafanua>
 
Back
Top Bottom