Je Waziri Mwakyembe anastahili kuwa kielelezo bora cha PhD za hovyo hovyo?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
60,422
120,747
Huko nyuma nilikuwa nikipenda sana ujengaji wake wa hoja hasa katika masuala mazima ya Sheria na Katiba nchini Tanzania ila kwa bahati mbaya mno matukio mawili ya hivi karibuni tu yamenifanya nianze kuwa na wasiwasi na Shahada ya Uzamivu ( PhD ) aliyonayo Waziri wa Sheria na Katiba nchini Mheshimiwa Harrison Mwakyembe.

Ni huyu huyu mwezi mmoja uliopita alijitokeza tena huku akijigamba kabisa kuwa Chama cha Wanasheria nchini TLS ( Tanzania Law Society ) hakipaswi kugombewa na Mtu ambaye tayari ni Mwanasisa hoja ambayo mbele ya Mahakama na Mahakimu waliokwenda shule ilitupiliwa mbali na Mwakyembe akaangukia pua.

Kuonyesha kuwa hana mshipa wa aibu ni juzi tu huyu huyu Waziri Mwakyembe kakurupuka tena kwa kusema kuwa kuanzia tarehe 1 mwezi May wale wote ambao wanatarajia kufunga Ndoa basi sharti wawe na Vyeti vya Kuzaliwa uamuzi ambao tunashukuru Bosi wake Rais Dkt. Magufuli aliutengua kwa hoja zenye mashiko mbele ya Great Thinkers tuliotukuka kabisa.

Kutokana na matukio haya kutoka kwa Daktari wa Falsafa Mwakyembe je kwa utaalam na uchambuzi wenu wana JF mnadhani huyu Mtu ni Kielelezo tosha cha PhD makini au anawakilisha wenye PhD za hovyo hovyo nchini Tanzania?

Karibuni na naomba kuwasilisha.
 
Kwanza aliikana dhana ya muungano wa serikali tatu kama alivyowasilisha katika thesis yake ya phd kisha akakengeuka kuhusu watuhumiwa wa sakata la Richmond ambako alitangulia kusema "sehemu ya ripoti" hakuisoma ili kuilinda serikali, wakati wa kampeni akabadilika!
Phd (parmanent head damage) ndio jambo lililotokea kwa mwanafyale harrison!
 
Mimi masikitiko yangu ni kipindi ameugua kiasi kile baada ya ile issue ya richmond,
Tukahimizwa makanisani tumuombee huyu mtu kumbe daaaaa!

Naomba Mungu anisamehe kwani sikuwa makini na huyu mtu nilijua anatetea maslahi mapana ya taifa letu kumbe njaa tu ilikua inamsukuma!
 
nampenda Lissu kuwaumiza walimu wake kuhusu sheria mbalimbali. Dr migiro alichemka, mwakyembe huyu alichanwa mbaya na Mr TLA sasa jamani naona magumu yatampata prof kabudi. aliyemuimili lissu ni change kwa kumkubali au kutaka wabadirishe lugha inayotumika na kidoogo jaji werema.
 
Back
Top Bottom