Je, Wajua Bunge linaweza kutoa azimio batili? CAG yuko kikatiba. Je, Bunge lina uwezo kutopokea ripoti ya CAG?

Kwenye bandiko hili tulizungumzia Bunge letu kutoa azimio batili.
Kwanza azimio batili hilo lilisema Bunge halifanyi kazi na Ofisi ya CAG.

Tukasema humu Ofisi ya CAG ni Ofisi ambayo ipo kikatiba, Bunge halina mamlaka kuamua kuwa halifanyi kazi na Ofisi ya CAG, Bunge halina uwezo huo, hivyo azimio lile ni batili.

Ndipo Spika ili kulikingia kifua azimio batili hilo, Mhe. Spika, akatoa ufafanuzi wa kuondoa ubatili huo, kuwa Bunge sasa sio halitafanya kazi na Ofisi ya CAG, bali Bunge ni halitafanya kazi na CAG Prof Assad, hivyo halitapokea ripoti ya CAG yenye saini ya Prof Assad, ila ripoti hiyo ikisainiwa na mtu mwingine yoyote, itapokelewa.

Pia tukasema humu, hilo haliwezekani kwa sababu huwezi kumtenganisha CAG Prof Assad na Ofisi ya CAG.

Mwisho wa siku, Ripoti ya CAG yenye saini ya CAG Prof Assad ndio iliyowasilishwa Bungeni na kupokelewa rasmi hivyo kuthibisha rasmi ubatili wa azimio lile.

Leo nimemsikia Mhe. Spika akizungumzia kupokea ripoti ya ukaguzi wa Ofisi ya CAG.



P

Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuna jambo analitafuta na majibu anataka yawe kama jinsi anavyotaka yawe.
 
Baada ya uteuzi wa CAG mpya, sijui sasa kama hili azimio batili sasa litafutwa rasmi au litaachwa lijifie kifo cha mende, kimya kimya.

Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu kwasababu ameacha Legacy.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali na alama za kuuliza nimeziweka, maana watu tusije itwa mahali kuhojiwa kuwa tumelidhalilisha Bunge.

Swali lenyewe ni hili,
Jee Wajua Bunge Linaweza Kutoa Azimio Batili?. CAG yuko Kikatiba, Jee Bunge Lina Uwezo Kutofanyakazi na CAG?. au kutopokea Ripoti ya CAG?.

P.
Naendelezea hapahapa~~chochote chenye public interest kina mawazo na maamuzi yanayotoka kwa watu kwa ajili ya watu,mwenyekiti wa ccm ndiye anejigeuza kuwa mwenyekiti wa Tanzania,yeye ndiye anayeamua nini kiwe for public interest na kipi kisiwe,alipomtimua mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali baada ya mkaguzi huyo kusimamia public interest wewe Pascal Mayalla hukumgombeza magufuli au kumkumbusha kuwa pesa iliyopotea ni ya umma,na mkaguzi ndiye jicho la umma,unamshangilia mwizi halafu unaongea habari za public interest,fool
Mkuu Capt Tamar ,
Asante,
Ubarikiwe
Japo sina uhakika, kwavile siwezi kusoma mabandiko ya watu wote humu, lakini humu JF, mimi ni miongoni mwa tuliomuongelea sana CAG, Ofisi ya CAG na Ripoti za CAG!.
Nakutakia Jumapili Njema
P
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali na alama za kuuliza nimeziweka, maana watu tusije itwa mahali kuhojiwa kuwa tumelidhalilisha Bunge.

Swali lenyewe ni hili,
Jee wajua Bunge linaweza kupitisha Azimio Batili?. CAG yuko kikatiba, jee Bunge lina uwezo kupitisha azimio la kutokufanyakazi na CAG?. au kutopokea Ripoti ya CAG?. Bunge linalopitisha azimio batili tuliiteje?. Tukiliita ni Bunge linaongozwa na vilaza, ni kulionea?.

Ukisikia ulevi wa madaraka sasa ndio huu. Hawa viongozi wa Bunge letu tukufu, wamelewa madaraka kuruhusu azimio batili lijadiliwe bungeni, lakini na wabunge waliopitisha azimio hilo, batili, pia ni wabunge vilaza!, jee wanakijua kitu kinachoitwa "The Constitutional mandates of the Controller and Auditor-General"?. Yaani mandate ya CAG iwekwe kwenye katiba yetu halafu waheshimiwa wabunge wetu walioapa kulinda katiba, wazuie jambo lililoelekezwa kikatiba?. Ukisema hili ni Bunge la ajabu sana, utakuwa unawaonea?

Kwa kumbukumbu yangu kupitia mafunzo ya sheria ya katiba tulivyofundishwa, Katiba ndio sheria mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni sheria batili, hivyo azimio lolote lililo kinyume cha katiba ni azimio batili, Bunge la JMT, limepitisha azimio batili, huku kule bungeni kuna AG, wanasheria wabobezi!. Nashauri Job Ndugai, ndie awe spika wetu wa mwisho asiye mwanasheria!.

Hivyo nahitimisha na lile swali kuu la msingi la bandiko hili
Jee wajua Bunge linaweza kupitisha Azimio Batili?. CAG yuko kikatiba, jee Bunge lina uwezo wa kutofanya kazi na CAG?. Au lina uwezo, kutopokea Ripoti ya CAG?. Bunge linalopitisha azimio batili, liitweje?.

Paskali
Ni katika kujikumbusha tuu.
P
 
Back
Top Bottom