Je, ushawahi kuumizwa Kama Mimi?

Mbondijr

Senior Member
Joined
Sep 9, 2024
Posts
183
Reaction score
355
Aisee yamenikuta nikahisi nipo kwenye njozi ni wiki mbili tu lakini nilikonda kiasi ambacho hata upepo kidogo ukija napepesuka

Kiufupi siku moja nimelala usiku naskia simu vuuu, vuuu, vuuu nilikuwa nimeweka vibration kuangalia mama ndio alikuwa anapiga ile kupokea tu hakuna salamu Wala Nini niliskia sauti ya huzuni ikisema mwanangu hamna kulala tena fanya ufanyavyo asubuhi uwe umefika nyumbani, muda huo naangalia saa ni saa 5 usiku halafu simu akakata napiga simu haipokelewi napiga tena zaidi ya mara tano lakini haikupokelewa.

Kwanza nguvu zikaniisha gafla kwa kuwaza nNini kimetokea huko nyumbani, ghafla nikapata wazo nipigie jirani yetu labda atanipa taarifa iliyokamilika lakini pia skumpata nikipiga simu haipatikani, aisee niliwaza mengi pasipo majibu

Nikaona isiwe tabu acha nifuate maneno ya mama kuwa asubuhi ikifika niwe nishafika nyumbani nikavuta shati chap nikavuta kiatu chapu nikatinga nikatoka nje nikauwasha mkoko nikauacha ungurume kidogo kwa ajili ya safari dakika 5 mbele nikaanza safari ya kwenda nyumbani
 
Pole mwamba, nilikuja kuona message asubuhi saa nne, baba yako ametutoka, basi nikaingia bafuni nikaoga. Nikawasha chuma huyo kuitafuta Mwanza from Dar .. nakumbuka nilitoka dar kama saa sita hivi mchana, nimeingia mwanza usiku kama wa nane au tisa
 
Mkuu unakimbizwa..?
 
Huu ni uandishi wa mwanafunzi aliyetoka shule hivi karibuni. Story haina uhalisia! Bora likizo yenu iishe ili mkaendelee na masomo.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…