Heparin
Senior Member
- Sep 24, 2021
- 127
- 420
Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha baada ya gari la abiria la kampuni ya Batco linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Mahaha wilayani Magu linadaiwa kusombwa na maji mapema asubuhi wakati dereva akijaribu kuvuka daraja la Mto Simiyu.
Afisa Habari wa wilaya ya Magu amekiri kutokea kwa ajali hiyo na kwamba uongozi upo njiani kuelekea eneo la tukio.
Taarifa zaidi zinafuata.
---- UPDATE----
Mtu Mmoja amefariki Dunia na wengine ishirini na tano kunusurika kufuatia ajali iliyotokea katika mto Simiyu Wilayani Magu Mkoani Mwanza baada ya basi dogo aina ya Tata kampuni ya Batco iliyokuwa inatokea Wilayani Bariadi kuelekeka Jijini Mwanza kuacha njia na kutumbukia ndani ya mto huo.