mr. Thomas a.k.a uncle Tom..... Huyu ticha alikua wa hisabati, sasa sera yake ilikuwa maswali 50 ya hesabu usikose zaidi ya maswali 3. vinginevyo zikizidi kila swali utakalokosa anakuramba bakora 3,,, ilikuwa Kilakala primary school.
Mr. Shija - TBR Girls, hata sijui alikuwa anafundisha somo gani maana nilikua A-Level alikua anafundisha O-Level nadhani ni masomo ya ufundi maana ofisi zake zilikuwa karakana. Huyu O-Level walikuuwa wanamwita "chimpanzee" kutokana na umbo lake na mwendo. Ikiwa zamu yake wiki nzima mnakuwa kama mko kwenye wasiwasi wa vita! Alikuwa hajali kuingia mabweni ya wasichana kutimua watu waende prep usiku na kuwahi mchaka mchaka asubuhi. Muwe mnavaa au mmelala ye hajali anachojali ni muda tu!
Alikuwa na uwezo wa kuchapa form I mpaka VI mtu wa 1 na wa mwisho wakatapa maumivu sawa.
Kuna siku alinichapa kwa kutosafisha eneo tulilopangiwa Form V, fimbo iliuma mpaka nikahisi kupata kichaa! Nilijikuta nampigia makelele "UMENICHAPA HIVI? NA SIFAGIII! NASEMA SIFAGIIIII! Wenzangu hawakuamini maana sikufagia kweli na aliamua kuniacha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.