Je, unajua kwamba huyo mke/mme uliye naye sasa sio wako?

Je, unajua kwamba huyo mke/mme uliye naye sasa sio wako?

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Naongea na wewe uliyeachana na mwenzi wako wa kwanza na kuoa au kuolewa tena. Nakujulisha kuwa huyo mke/mume uliye naye sasa sio wako mbele za Mungu — unazini.

Katika dunia ya sasa ambapo talaka na ndoa ya pili au ya tatu zinaonekana kama jambo la kawaida, ni muhimu sana kwa watu wanaotamani kwenda mbinguni kufahamu msimamo wa Mungu juu ya ndoa, talaka, na kuoa au kuolewa tena baada ya talaka.

1. Ndoa ni agano la milele, sio mkataba wa muda
Biblia inafundisha kuwa ndoa ni muungano wa kiroho na kimwili uliowekwa na Mungu mwenyewe.
Katika Mwanzo 2:24 tunaambiwa:
“Kwa hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

Muungano huu wa “mwili mmoja” si wa muda, ni wa kudumu mpaka kifo kitakapowatenganisha. Hili linasisitizwa tena na Yesu Kristo katika Mathayo 19:6
"Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe..”

Kwa hiyo, talaka haibatilishi kile Mungu alichokiunganisha. Ingawa mwanadamu anaweza kutoa talaka, mbele za Mungu bado mme na mke wa kwanza wanahesabika kuwa wameunganishwa.

2. Talaka haitoi ruhusa ya kuoa au kuolewa tena
Yesu mwenyewe alizungumzia jambo hili kwa uwazi sana. Katika Luka 16:18 anasema:
"Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine anazini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe anazini.”

Hapa tunaona wazi kuwa kuoa au kuolewa tena baada ya talaka ni uzinzi. Kwa lugha nyingine, kama ulimwacha mume au mke wako wa kwanza, ukaoa au kuolewa tena, basi huyo uliye naye sasa sio wako. Mbele za Mungu unahesabika unaishi katika uzinzi.

3. Talaka iliruhusiwa kwa sababu ya ugumu wa mioyo — sio mpango wa Mungu
Yesu alipoulizwa kuhusu talaka, alisema katika Mathayo 19:8:
“... Musa aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.”

4. Hatari ya kuishi katika uzinzi
Wale wanaoishi na wake au waume wa ndoa ya pili, wanaishi katika hali ya dhambi — yaani uzinzi wa kudumu. Na Biblia inasema wazi katika 1 Wakorintho 6:9-10:
"Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti.”

Hili ni onyo kali. Kama unaendelea kuishi na mke au mume asiye wako bila kutubu na kurekebisha, una hatari ya kupoteza uzima wa milele.

5. Suluhisho: Tubu na umrudie mme au mke wako wa kwanza
Suluhisho sio kuhalalisha mahusiano uliyo nayo sasa. Suluhisho ni kutubu kwa dhati, kujitenga na hali ya uzinzi, na kumrudia mwenzi wako wa kwanza. Kama huwezi kumrudia huyo wa kwanza, ukae hivyo hivyo peke yako.
Katika 1 Wakorintho 7:10-11, Paulo anaandika:
“Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.”

Biblia haiungi mkono ndoa ya pili baada ya talaka, bali inashauri ama kubaki bila kuolewa/kuoa au kumrudia mwenzi wa kwanza.
 
Kuna watu wanaodai kwamba kama mume au mke amefumaniwa akifanya uzinzi basi ni halali kumwacha au kumpa talaka na kuoa au kuolewa na mwingine. Wanatumia andiko la Mathayo 5:32 kuhalalisha madai yao. Andiko hilo linasema hivi:
Mathayo 5:32
"Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini."

Ni muhimu kujua kuwa kuna tofauti kati ya uasherati na uzinzi.
Uasherati ni kabla watu hawajaoana. Uzinzi ni baada ya watu kuoana. Kumbuka jinsi Yusufu alivyotaka kumwacha Mariamu. Alifikiri amefanya uasherati. Malaika akamwambia asimwache kwakuwa mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

Kwa sababu hiyohiyo watu walio katika uchumba, hata kama wamepeana posa tayari, ikithibitika kuwa mmoja amefanya uasherati, huyo mwenzake ni ruksa kumwacha kwa sababu anaonyesha wazi sio mwaminifu. Lakini watu wakiishaoana, uzinzi siyo kisingizio cha kuachana. Mwenzako akifanya uzinzi msamehe. La sivyo, ukimwacha, ukae hivyohivyo, usioe/usiolewe. Ukweli huu ni mchungu. Lakini hakuna shortcut, kama tunataka kwenda mbinguni ni lazima tutii maagizo ya Mungu.
 
Biblia haiungi mkono ndoa ya pili baada ya talaka, bali inashauri ama kubaki bila kuolewa/kuoa au kumrudia mwenzi wa kwanza.
Unasisitiza kuwa Biblia haiungui mkono ndoa ya pili, mbona kama kwa makusudi kabisa umeacha andiko la 1 Kor 7:15?

1 Corinthians 7:15 CEV
[15] If your husband or wife isn't a follower of the Lord and decides to divorce you, then you should agree to it. You are no longer bound to that person. After all, God chose you and wants you to live at peace.

Je, Kuna amani gani utaipata kwa kuishi na mtu asiyeamini unachokiamini kiimani, au aliyeliwa mbususu kimasihara?
 
Uasherati ni kabla watu hawajaoana. Uzinzi ni baada ya watu kuoana.
Uasherati ni matendo ya ngono yanayofanyika nje ya ndoa, hata mwanandoa anapofanya ngono na mtu mwingine ambaye sio mwenza wake, huo pia ni uasherati. Ni kweli pia kuwa uzinzi unahusianisha mmoja wa washiriki wa ngono kuwa na ndoa. Ijulikane kuwa uzinzi ni uasherati ingawa sio kila uasherati ni uzinzi.
Lakini watu wakiishaoana, uzinzi siyo kisingizio cha kuachana.
Hii mkuu, unaitolea wapi wakati Biblia imeeleza kwa uwazi kabisa kuwa mtu anapokuwa sio mwaminifu kwenye ndoa, anakua amejikatia tiketi ya kupewa uhuru wa kufanya uzinzi wake atakavyo ila awe nje ya ndoa. Imeruhusu mtu huyo kupewa talaka.

Na pia ni vyema kusoma Biblia kwa lugha ya kiingereza, inarahisisha kupata maana iliyokusudiwa.

Matthew 5:32 EASY
[32] But what I tell you is this: A man must not send his wife away except for one reason. He may only send her away if she has had sex with another man. If he sends her away for any other reason, he has done a wrong thing. It is like he has caused her to have sex with another man. Also, if a woman has left her husband, another man must not marry her. That is the same as if he had sex with another man's wife.

Na hii
Matthew 5:32 CEV
[32] But I tell you not to divorce your wife unless she has committed some terrible sexual sin. If you divorce her, you will cause her to be unfaithful, just as any man who marries her is guilty of taking another man's wife.
 
1) Adultery is a biblical ground for divorce . And yes you can remarry.

"And I tell you this, whoever divorces his wife and marries someone else commits adultery—unless his wife has been unfaithful.”
mat.19.9.NLT


2) Another biblical ground is if the spouse is not a beleiver and THEY want a divorce. You can now remarry in the Lord.

"But if the husband or wife who isn’t a believer insists on leaving, let them go. In such cases the believing husband or wife is no longer bound to the other, for God has called you to live in peace."
1cor.7.15.NLT

3) Not all marriages are works of God.

One sign of such a marriage is the presence of betrayal.

Another is if the marriage doesn't glorify / brings insult to the Lord's name.

Hence the above provisions for divorce.


a) Kind Ahab married Jezebel. That was not God's work. God killed his wife.


b) During Ezras time the Israelite men married pagan women, had children with them, a great sin similar to adultery in God's eyes. They had to divorce their wives and send their families away as part of the repentance process. (Ezra 9, 10)

c) King Solom married pagan women and bought a curse upon himself. His marriages weren't God's work.

" So now the Lord said to him, “Since you have not kept my covenant and have disobeyed my decrees, I will surely tear the kingdom away from you and give it to one of your servants."
1ki.11.11.NLT

Ndoa zote ambazo MUNGU mwenyewe ameziunganisha amezibariki. Alichokibariki Bwana hakimletei suto. Bwana hana show mbovu.

Bwana Yesu asifiwe sana.

Repent and be faithful to your spouses our Lord is coming!
 
Uasherati ni matendo ya ngono yanayofanyika nje ya ndoa, hata mwanandoa anapofanya ngono na mtu mwingine ambaye sio mwenza wake, huo pia ni uasherati. Ni kweli pia kuwa uzinzi unahusianisha mmoja wa washiriki wa ngono kuwa na ndoa. Ijulikane kuwa uzinzi ni uasherati ingawa sio kila uasherati ni uzinzi.

Hii mkuu, unaitolea wapi wakati Biblia imeeleza kwa uwazi kabisa kuwa mtu anapokuwa sio mwaminifu kwenye ndoa, anakua amejikatia tiketi ya kupewa uhuru wa kufanya uzinzi wake atakavyo ila awe nje ya ndoa. Imeruhusu mtu huyo kupewa talaka.

Na pia ni vyema kusoma Biblia kwa lugha ya kiingereza, inarahisisha kupata maana iliyokusudiwa.

Matthew 5:32 EASY
[32] But what I tell you is this: A man must not send his wife away except for one reason. He may only send her away if she has had sex with another man. If he sends her away for any other reason, he has done a wrong thing. It is like he has caused her to have sex with another man. Also, if a woman has left her husband, another man must not marry her. That is the same as if he had sex with another man's wife.

Na hii
Matthew 5:32 CEV
[32] But I tell you not to divorce your wife unless she has committed some terrible sexual sin. If you divorce her, you will cause her to be unfaithful, just as any man who marries her is guilty of taking another man's wife.
Ili uweze kuelewa vizuri maana halisi za Maandiko inabidi usome Biblia ya Kigiriki, sio tafsiri za Kiingereza. Biblia za Kiingereza zimetafsiriwa kutoka Kigiriki.

Sasa neno la kigiriki lililotumika katika Mathayo 5:32 ni: porneia (πορνεία)
Katika Mathayo 5:32, Yesu anasema:
“...parektos logou porneias...”

Kwa hiyo tafsiri inayosema “isipokuwa kwa sababu ya porneia (uasherati)” ndiyo sahihi kulingana na Kigiriki.

Maana ya porneia katika Kigiriki cha Agano Jipya ni uasherati. Uasherati ni mahusiano ya kimwili kabla watu hawajafunga ndoa.

Moicheia (μοιχεία) ndilo neno la Kigiriki linalomaanisha uzinzi kwa watu walio katika ndoa.

Yesu alitumia moicheuō (kuzini) katika Mathayo 5:28 na 19:9 kwa maana ya uzinzi wa mume au mke aliye ndani ya ndoa.

Hivyo ndugu, kama mwenzi wako wa ndoa amefanya uzinzi, msamehe tu hata saba mara sabini, sio kumwacha au kumpa talaka. Kwani Yesu alitusamehe dhambi zote isipokuwa uzinzi? Ukiamua kumwacha, hupaswi kuoa au kuolewa tena. Vinginevyo utahesabika mzinzi.
 
Kuna watu wanaodai kwamba kama mume au mke amefumaniwa akifanya uzinzi basi ni halali kumwacha au kumpa talaka na kuoa au kuolewa na mwingine. Wanatumia andiko la Mathayo 5:32 kuhalalisha madai yao. Andiko hilo linasema hivi:
Mathayo 5:32
"Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini."

Ni muhimu kujua kuwa kuna tofauti kati ya uasherati na uzinzi.
Uasherati ni kabla watu hawajaoana. Uzinzi ni baada ya watu kuoana. Kumbuka jinsi Yusufu alivyotaka kumwacha Mariamu. Alifikiri amefanya uasherati. Malaika akamwambia asimwache kwakuwa mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

Kwa sababu hiyohiyo watu walio katika uchumba, hata kama wamepeana posa tayari, ikithibitika kuwa mmoja amefanya uasherati, huyo mwenzake ni ruksa kumwacha kwa sababu anaonyesha wazi sio mwaminifu. Lakini watu wakiishaoana, uzinzi siyo kisingizio cha kuachana. Mwenzako akifanya uzinzi msamehe. La sivyo, ukimwacha, ukae hivyohivyo, usioe/usiolewe. Ukweli huu ni mchungu. Lakini hakuna shortcut, kama tunataka kwenda mbinguni ni lazima tutii maagizo ya Mungu.
Nakupenda 😋
 
Naona umedhamiria kutingisha meza hadi vinywaji vyote vimwagike mkuu.
 
Ndiyo lakini pia napenda uwe mke wangu.
Umechelewa. Nilitoa mwaliko wa arusi yangu zamani. Hukuupata?

Kama unataka mke mwema, mwambie Bwana atakupa wa kufanana na wewe.

Maandiko yanasema mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana(Mithali 19:14).

Usitafute mke hapa JF.
 
Umechelewa. Nilitoa mwaliko wa arusi yangu zamani. Hukuupata?

Kama unataka mke mwema, mwambie Bwana atakupa wa kufanana na wewe.

Maandiko yanasema mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana(Mithali 19:14).

Usitafute mke hapa JF.
Nimekata tamaa mazima.
 
Back
Top Bottom