Je, unaifahamu meli ya MV Dar es Salaam?

Je, unaifahamu meli ya MV Dar es Salaam?

MV DAR ES SALAAM

View attachment 1643635

Rais John Pombe Magufuli akiizindua meli ya MV DAR ES SALAAM.

Meli ya MV DAR ES SALAAM ilitengenezwa kwa nia ya kurahisisha usafiri kwa wakazi waishio kwenye fukwe za Bagamoyo na Dar es Salaam.
View attachment 1643636
Kampuni ya kutengeneza meli iitwayo Western Marine Shipyard (Hull WMShL-124) ilipokea oda kutoka kwa JGH Marine A/S, Denmark, kwamba iunde meli ya abiria ambayo iko kwa muundo wa aluminum body catamaran Mali ya Tanzania Electrical, Mechanical, and Electronics Services Agency (TEMSA).

Uundwaji huu wa meli ulikamilika na kukabidhiwa mwaka 2014 kwa wizara ya ujenzi

Vessel Type: Aluminum Body Catamaran Type Passenger Ship

Length OA: 37.54m
Breadth Molded: 11.5m
Depth Molded: 3.8m
Net Tonnage: 363.19 tons
Engine and Propulsion: 2x Yanmar 12AY-WET IMO Tier 2 1140kW at 1840RPM with 2x fixed-pitch propellers
Waterline Length: 31.84m
Draft: 1.7m
Gross tonnage: 471.98 tons
Complement: 300 person

View attachment 1643638
View attachment 1643639
View attachment 1643640
View attachment 1643641
View attachment 1643642
iko wapi sasa mbona haionekani na nani aliieleta tum'bane atueleze alikoipeleka.. au ndo tumiingizwa CHAKABOVU
 
Bila shaka ulikusudia kusema Mnadhimu, na si huyo uliyemtaja
washasahau lile swala la kifaru bagamoyo...sasa ngoja mhadhini mkuu wa jeshi aione hii post...wabongo tunaishi sana kwa mazoea
 
Mkuu ilikatazwa kuizungumzia hii. Ni sawa na kuzungumzia vifaru.
 
Bujibuji mbona kutuumiza mioyo na kutukumbusha masononeko?

Kwa maslahi mapana ya JF na familia za baadhi ya watu, naomba Moderator mfunge huu uzi.

Agizo lilitoka juu kukataza kuongelea hiki chombo kwa vile sasa hivi ni mali ya jeshi.

Maxence Melo bado hajatulia na kuandamwa kwa kesi zisizo na msingi, tusiwaongezee matatizo mengine tafadhali.
 
iko wapi sasa mbona haionekani na nani aliieleta tum'bane atueleze alikoipeleka.. au ndo tumiingizwa CHAKABOVU
Ililetwa na mkuu Wa Nchi mzee magu, alivyoona ni kshfa kwake ili isiendelee kujadiliwa akaamuwa kuwapa wanajeshi

Sasa hivi hutakiwi kuijadili hii meli
 
Ililetwa na mkuu Wa Nchi mzee magu, alivyoona ni kshfa kwake ili isiendelee kujadiliwa akaamuwa kuwapa wanajeshi

Sasa hivi hutakiwi kuijadili hii meli
tuanzie hapa kuiadili tena maana hii nayo uhujumu uchumi pia wahusika washughulikiwe
 
Back
Top Bottom