Je Uko Huru?? Jitathmini.....

Je Uko Huru?? Jitathmini.....

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,802
Reaction score
43,205
Habari za siku ya jumapili wapendwa,

Nahisi maelezo yatakuwa marefu ila najitahidi kuyafupisha. Nimekuwa nikijitathmini na kulinganisha na uhalisia wa maisha.... nikagundua vingi tuu kuhusu uhuru wa mwanadamu hata mimi Kasie.

Tangu ulipozaliwa hadi una miaka 18 (kwa waliolelewa chini ya wazazi au walezi ) hapo hawakuwa huru kwa maana ya kuwa unafanya kile anachopenda na kusema mzazi au mlezi hata kama anakosea au si sawa au hukipendi. Hii inaanzia kwenye kuchaguliwa nguo za kuvaa chakula gani ule asubuhi mchana na jioni, uende wapi na wapi kutembea au kupumzika, likizo ufanye nini, hata marafiki saa ingine mzazi au mlezi aliingialia kati. Kiufupi unakuwa huna uhuru wa kufanya unachopenda au unachotamani.

Kwa sie waafrika baada ya miaka 18 ni wachache sana wanapata uhuru wa kufanya yao kuishi wanavotaka wao kwasababu bado wanakuwa wanaomtegemea mzazi kwa kiasi kikubwa. Inapofikia unaanza kazi kuna baadhi huapata uhuru wa maisha yao kwa kuishi watakavyo na wapendanao japo kuna baadhi huendelea kuwa watumwa wa familia au kutokuwa huru kwa kufanya na kutenda wasemacho wazazi na familia aliyokuwa nayo sisemi kuwa hivi ni vibaya hapana. Hapa naongelea je uko huru?

Au kuwa huru ni nini? Naomba mtu anisaidie kuelezea maana ya kuwa huru...

Hapohapo kuna baadhi akishapata kazi anaoa au anaolewa hapa anaanza kuishi kwa matakwa ya mpenzi wake na akishapata watoto anaishi kwa matakwa ya watoto wakwe wifi shemeji n.k. jiulize tena uko huru? Sisemi uache familia yako?

Ni hivi, kama katika maisha yako umefanikiwa kufanya matakwa ya wazazi huku ukapata wasaa wa kufanya matakwa yako basi ulikuwa huru. Hapa yaweza kuwa unapenda bustani au kufuga na uliweza kufanya haya chini ya himaya ya wazazi basi ulikuwa huru kwa kiasi. Kama umefanikiwa kuwa na maisha yako unajitegemea mwenyewe na bado unatimiza matakwa yako binafsi na unatimiza matakwa ya wazazi au walezi wako na mpenzi wako mke au mume na watoto basi uko huru.

Ukiona hadi leo unaishi maisha yako na familia au hata kama huna familia na hujafanikiwa kufanya au kutimiza matakwa yako binafsi kama kujiendeleza kieleimu kufuga au kupima kisasa kama unapenda hivyo basi ujue hauko huru. (uhuru bunafsi)

Na ukiona hata ukitaka kwenda short call ni hadi upate ruhusa au ushauri wa mtu ujue wewe ndo uko gerezani kabisa.

Poleni kwa kuwachosha na maelezo mengii. Kwa waliolelewa mtanisaidia kuwaelewesha wengine tafadhali.

Muwe huru kuchangia na mchango wako utaonesha kama uko huru au laah. Watch out hehehehee.

Jumapili njema.

Kasie Mahaba bin Nyonda-ake Mtufudenge.

UPDATE:



Mkiwa mnaendelea kutafakari na kuchangia burudikeni na jiwimbo hilo la Lucky Dube...

Again Kasie Mahaba, Mahabat wake mtu....
 
mie pia siko huru! maana sina njaa lakini nipo jikon napika ili familia ile... sijui nasaidiwaje hapo! [HASHTAG]#naanzishaMaandamano[/HASHTAG]
 
utakuwaje huru sasa? we are controlled by power from outside kwa hiyo kama mimi nimeletwa kwa kusudi la Mungu hapa duniani nitaishi kwa mapenzi yake na nisipotimiza aliniambia sitoingia katika ufalme wake naweza kusema kuwa huru kabisa kabisa hiyo kitu hakuna na haipo na haitokuwepo
 
Hakuna msamiati wa uhuru katika maisha,tusidanganyane.
Kuna sheria za nchi,dini,moral ethics,utumishi sijui nk mavazi daima zinachukua uhuru wetu. Mfano mimi napenda sana kutovaa nguo kabisa lakini nathubutuje? Uchumi pia unalimit uhuru wetu,sipendi kabisa kuendesha vitz lakini uwezo umekomea hapo,sipendi kuishi uswazi ila hali sasa! Kwa hiyo dunia haitoi huo uhuru tunaousema,kwangu mimi ni imaginary tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmmh hakuna uhuru usio na mipaka
Unaweza kuwa na uhuru wa jambo moja au mawili ila sio yooote maishani maana hapo utagusa maisha ya wengine wasiwe nao huru
Kwahiyo upo Ila kiasi sio asilimia maishani
 
Maisha ni mipaka .Huwezi kwenda hovyo hovyo tu kwa kisingizio cha uhuru.
Mipaka inaanza kwa sheria za kiroho.
Sheria za nchi .
Taratibu za ndoa zinakufanya uwe kwenye mipaka.
Sheria za ofisini zinakufanya uwe ndani ya mipaka.
Labda uhamue tu kwa utashi wako uchupe mipaka ndio utakuwa huru.
 
Haiwezekani kuwa huru kabisa.
Hata uhuru tunaohisi tunao ni kujiliwaza tu.

Kwa mfano mtu hudhani akijitegemea bila mpenzi, mbali na wazazi na bila watoto basi yuko huru anasahau kwamba bado unatawaliwa na sheria za kazini kwenu kwa hiyo kuna mambo huweZi fanya.

Hata kama huna kazi umejiajiri bado miongozo ya kijasiriamali na kanuni za fedha zitakunyima uhuru fulani.

Hata ukiwa huna hayo yote bado unabamwa na kanuni za kiimani(labda dini) au kanuni za kimazingira na kisayansi mf huwezi kuwa huru kukimbia kwa kasi ya mwanga, huwezi kupaa hata kama ungetamani.
 
Nilitamani sana kuwa huru na nilipomaliza tu chuo sikurudi nyumbani,, Aaaaah!!! Story ndefu umenigusa niliteseka ili mradi tu niwe huru.....
Sikutaka ku apply kazi yoyote ile hata mabest zangu walikua wakinitumia matangazo niliona ujinga tu!!!!
Ndoto yangu ilikua ni kumiliki mali na kuwa na uhuru na si kupangiwa kazi za kufanya nimepitia mengi Sana yani we mama umenigusa mnooooooo!!!!
Niliamua tu kuvaa uso mgumu nimefanya mengi lkn ntasimulia mawili tu yaliyonifanya Kuwa na uhuru..
2014 Nikapata baba mmoja mfanyabiashara wa dhahabu basi mapenzi moto moto huyo baba akahamia mpanda kikazi baada ya muda akanitumia nauli nikaenda tukawa tunaishi pamoja hapo kambini
Alikua akichimba dhahabu na kununua na alikua akichoma mwenyewe Kwa aliniamini sna so akawa ananipa natunza sehemu maalum chumbani tulipokua tunalala nilijifunza jinsi ya kuiba kupitia wafanyakazi wake nikawa naikwangua kutumia wembe Gillette kabla haijachomwa Mara ya pilina kuwekewa ubora ili iweze kusafirishwa.. na ule unga wa dhahabu niliutunza bdae nilifanikiwa kuuchoma na kuunganisha kupitia mafunzo aliyonipa....
Kila siku niliweza kumuibia tshs efu 50000 maana yeye kila bda ya siku 3 alikuwa anatumiwa million 100 na partners wake ambao ni wahindi na hawataki kujulikana Kama wanafanya hio kazi nilijiwekea utaratibu wa kuzipeleka benki kila ninapokamilisha laki 5
Nilikaa huko miezi 8 na siku naondoka toa nauli na mahitaji yangu alinipa m5 nifanye ninachotaka plus alinipa dhahabu gram 25 ukihesabu niliyoiba na PESA bank almost nilikua na hela ya kutosha...
Dhahabu zote niliuza na pesa zote niliweka bank sikutaka kukurupuka mana angejua nimemuibia na naujua mtandao wake wangeningoa kucha!!!!!.
Hapo nilikua na kibwana changu kidereva huyo nilikua namtumia kusafirisha mizigo yangu yangu ya biashara... Nilimshawishi na kumfanya awe tabia mbaya tuweze kuendana maana alikua muislamu Sana kila kitu aliona dhambi.....
Mapori ya runzewe nyakanazi na biharamulo huko nikamuunganisha na wakulima wa bangi tukawa tunapata tenda ya kupeleka dar tulisafiri usiku Kwa usiku na kila geti tuliacha 1m kasoro singida hapo askari ni wanoko tulikua tunaacha 2m mpk wkt mwingine 3m Kwa muda mrefu tulifanya ivyo...
Dogo utamu wa hela akaujua na akaniona mm Kama malaika mpk akaanza kutangaza ndoa,,,, mie hata lile wazo sikua nalo maana mie malengo yangu ilikua kukusanya PESA nitimize malengo yangu......
Nikampa sharti la kunioa tuuze gari alikua anaiendesha scania Daf then tutoroke nje ya nchi...... Kuuza gari ikabuma hii story sielezea maana naweza fahamika.
Basi tukapanga tuiuze Kama screpa so akajifanya gari imeharibika misugu sugu hapo kumbuka tajiri wa hayo magari Hana muda wa kufatilia gari moja kwa haraka coz anamiliki zaidi ya magari Mia 3 na yote yako barabarani tulikaa pale wiki1 tukijifanya gari imeharibika huku tukiuza vifaa Kila mmoja alikimbilia anakopajua kutuliza soo.......
Yule tajiri alienda kubeba ile gari baada ya wiki mbili na aliamini vibaka wa misugusugu wamefanya hio kazi!!!!!!!
Nilienda kwetu walipokea Kwa furaha.......
Nilianza research kwenye maduka ya hardware kkoo bda ya kujua bidhaa ambazo zinahitajika nilirudi kwenye ule mji nikafungua duka la ujenzi LA kuuza jumla jumla leo hii na mie ni boss
Lkn niliyopitia na niliyofanya hayasimuliki...
Kwangu mie nilitaka uhuru na sikutaka kuajiriwa na sijawahi kuajiriwa na sitaajiriwa rafiki zangu wananiona mpambanaji na hasa wale niliosoma nao laiti wangejua..........
We mama umenifanya nitoe ya rohoni yani umenikumbusha mbali sanaaaaa........
Hiii anzishia thread yake
 
Huwezi kuwa huru hadi ukawa huru, kila ukiona upo huru lazima kuna pingamizi la huo uhuru wako. I'd like to bang as many pretty chicks out there but uhuru huo sina due to morals za kidini, I'd like to drive the most expensive car out there but financial constraints won't let me.

Ndio maana hata mkulu akasema you've got freedom but not to that extent.
 
Back
Top Bottom