Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 22,802
- 43,205
Habari za siku ya jumapili wapendwa,
Nahisi maelezo yatakuwa marefu ila najitahidi kuyafupisha. Nimekuwa nikijitathmini na kulinganisha na uhalisia wa maisha.... nikagundua vingi tuu kuhusu uhuru wa mwanadamu hata mimi Kasie.
Tangu ulipozaliwa hadi una miaka 18 (kwa waliolelewa chini ya wazazi au walezi ) hapo hawakuwa huru kwa maana ya kuwa unafanya kile anachopenda na kusema mzazi au mlezi hata kama anakosea au si sawa au hukipendi. Hii inaanzia kwenye kuchaguliwa nguo za kuvaa chakula gani ule asubuhi mchana na jioni, uende wapi na wapi kutembea au kupumzika, likizo ufanye nini, hata marafiki saa ingine mzazi au mlezi aliingialia kati. Kiufupi unakuwa huna uhuru wa kufanya unachopenda au unachotamani.
Kwa sie waafrika baada ya miaka 18 ni wachache sana wanapata uhuru wa kufanya yao kuishi wanavotaka wao kwasababu bado wanakuwa wanaomtegemea mzazi kwa kiasi kikubwa. Inapofikia unaanza kazi kuna baadhi huapata uhuru wa maisha yao kwa kuishi watakavyo na wapendanao japo kuna baadhi huendelea kuwa watumwa wa familia au kutokuwa huru kwa kufanya na kutenda wasemacho wazazi na familia aliyokuwa nayo sisemi kuwa hivi ni vibaya hapana. Hapa naongelea je uko huru?
Au kuwa huru ni nini? Naomba mtu anisaidie kuelezea maana ya kuwa huru...
Hapohapo kuna baadhi akishapata kazi anaoa au anaolewa hapa anaanza kuishi kwa matakwa ya mpenzi wake na akishapata watoto anaishi kwa matakwa ya watoto wakwe wifi shemeji n.k. jiulize tena uko huru? Sisemi uache familia yako?
Ni hivi, kama katika maisha yako umefanikiwa kufanya matakwa ya wazazi huku ukapata wasaa wa kufanya matakwa yako basi ulikuwa huru. Hapa yaweza kuwa unapenda bustani au kufuga na uliweza kufanya haya chini ya himaya ya wazazi basi ulikuwa huru kwa kiasi. Kama umefanikiwa kuwa na maisha yako unajitegemea mwenyewe na bado unatimiza matakwa yako binafsi na unatimiza matakwa ya wazazi au walezi wako na mpenzi wako mke au mume na watoto basi uko huru.
Ukiona hadi leo unaishi maisha yako na familia au hata kama huna familia na hujafanikiwa kufanya au kutimiza matakwa yako binafsi kama kujiendeleza kieleimu kufuga au kupima kisasa kama unapenda hivyo basi ujue hauko huru. (uhuru bunafsi)
Na ukiona hata ukitaka kwenda short call ni hadi upate ruhusa au ushauri wa mtu ujue wewe ndo uko gerezani kabisa.
Poleni kwa kuwachosha na maelezo mengii. Kwa waliolelewa mtanisaidia kuwaelewesha wengine tafadhali.
Muwe huru kuchangia na mchango wako utaonesha kama uko huru au laah. Watch out hehehehee.
Jumapili njema.
Kasie Mahaba bin Nyonda-ake Mtufudenge.
UPDATE:
Mkiwa mnaendelea kutafakari na kuchangia burudikeni na jiwimbo hilo la Lucky Dube...
Again Kasie Mahaba, Mahabat wake mtu....
Nahisi maelezo yatakuwa marefu ila najitahidi kuyafupisha. Nimekuwa nikijitathmini na kulinganisha na uhalisia wa maisha.... nikagundua vingi tuu kuhusu uhuru wa mwanadamu hata mimi Kasie.
Tangu ulipozaliwa hadi una miaka 18 (kwa waliolelewa chini ya wazazi au walezi ) hapo hawakuwa huru kwa maana ya kuwa unafanya kile anachopenda na kusema mzazi au mlezi hata kama anakosea au si sawa au hukipendi. Hii inaanzia kwenye kuchaguliwa nguo za kuvaa chakula gani ule asubuhi mchana na jioni, uende wapi na wapi kutembea au kupumzika, likizo ufanye nini, hata marafiki saa ingine mzazi au mlezi aliingialia kati. Kiufupi unakuwa huna uhuru wa kufanya unachopenda au unachotamani.
Kwa sie waafrika baada ya miaka 18 ni wachache sana wanapata uhuru wa kufanya yao kuishi wanavotaka wao kwasababu bado wanakuwa wanaomtegemea mzazi kwa kiasi kikubwa. Inapofikia unaanza kazi kuna baadhi huapata uhuru wa maisha yao kwa kuishi watakavyo na wapendanao japo kuna baadhi huendelea kuwa watumwa wa familia au kutokuwa huru kwa kufanya na kutenda wasemacho wazazi na familia aliyokuwa nayo sisemi kuwa hivi ni vibaya hapana. Hapa naongelea je uko huru?
Au kuwa huru ni nini? Naomba mtu anisaidie kuelezea maana ya kuwa huru...
Hapohapo kuna baadhi akishapata kazi anaoa au anaolewa hapa anaanza kuishi kwa matakwa ya mpenzi wake na akishapata watoto anaishi kwa matakwa ya watoto wakwe wifi shemeji n.k. jiulize tena uko huru? Sisemi uache familia yako?
Ni hivi, kama katika maisha yako umefanikiwa kufanya matakwa ya wazazi huku ukapata wasaa wa kufanya matakwa yako basi ulikuwa huru. Hapa yaweza kuwa unapenda bustani au kufuga na uliweza kufanya haya chini ya himaya ya wazazi basi ulikuwa huru kwa kiasi. Kama umefanikiwa kuwa na maisha yako unajitegemea mwenyewe na bado unatimiza matakwa yako binafsi na unatimiza matakwa ya wazazi au walezi wako na mpenzi wako mke au mume na watoto basi uko huru.
Ukiona hadi leo unaishi maisha yako na familia au hata kama huna familia na hujafanikiwa kufanya au kutimiza matakwa yako binafsi kama kujiendeleza kieleimu kufuga au kupima kisasa kama unapenda hivyo basi ujue hauko huru. (uhuru bunafsi)
Na ukiona hata ukitaka kwenda short call ni hadi upate ruhusa au ushauri wa mtu ujue wewe ndo uko gerezani kabisa.
Poleni kwa kuwachosha na maelezo mengii. Kwa waliolelewa mtanisaidia kuwaelewesha wengine tafadhali.
Muwe huru kuchangia na mchango wako utaonesha kama uko huru au laah. Watch out hehehehee.
Jumapili njema.
Kasie Mahaba bin Nyonda-ake Mtufudenge.
UPDATE:
Mkiwa mnaendelea kutafakari na kuchangia burudikeni na jiwimbo hilo la Lucky Dube...
Again Kasie Mahaba, Mahabat wake mtu....
maishani