Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,833
- 978
Wakuu, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28.10.2020, hebu tutafakari pamoja hii kauli mbiu ya CHADEMA: Uhuru, Haki na Maendeleo.
Uzi huu hautalenga kuichambua kaulimbiu hiyo bali utalenga kwenye kuangalia kama kweli kauli mbiu hiyo imekuwa ikitekelezwa kwa vitendo kwenye chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Uhuru na Haki
Wakati bunge la Ndugai linakaribia kuvunjwa, viongozi wakuu wa CHADEMA waliwataka wabunge wao kuacha vikao vya bajeti na kwenda kijikarantini. Huenda hili lilikuwa jambo jema lakini halikupaswa kulazimishwa hasa katika kipindi ambacho wananchi waliwahitaji sana wabunge wao wawatetee kwenye bajeti. Wakati wabunge hao ambao walishavuta posho wakijikarantini, wananchi wao walikuwa barabarani wakitafuta riziki zao za kila siku.
Baadhi ya wabunge waligomea amri hiyo. Sote ni mashahidi kilichowakuta akina Lijualikali, Silinde na wenzao.
Wabunge wa CHADEMA hukatwa shilingi milioni moja kila mwezi kutoka kwenye mishahara yao. Je, makato hayo ni makato ya hiyari ambayo yanatawaliwa na misingi ya haki na Uhuru?
Maendeleo
CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kilipaswa kuonesha kwa vitendo kuwa ndio mbadala wa CCM. Pamoja na ruzuku, michango na miradi, ofisi ya makao makuu ya chama hicho haiakisi dhana ya maendeleo. Wengi wa wabunge wake hawaoneshi ubunifu kwenye majimvo yao ili tuone kwa vitendo kuwa hawa ni watu wa maendeleo.
Je, kaulimbiu yao sio ghiliba kwa wananchi?
Povu, utopolo na ugoro: RUKSAAA
Amani Msumari
Tanga
Uzi huu hautalenga kuichambua kaulimbiu hiyo bali utalenga kwenye kuangalia kama kweli kauli mbiu hiyo imekuwa ikitekelezwa kwa vitendo kwenye chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Uhuru na Haki
Wakati bunge la Ndugai linakaribia kuvunjwa, viongozi wakuu wa CHADEMA waliwataka wabunge wao kuacha vikao vya bajeti na kwenda kijikarantini. Huenda hili lilikuwa jambo jema lakini halikupaswa kulazimishwa hasa katika kipindi ambacho wananchi waliwahitaji sana wabunge wao wawatetee kwenye bajeti. Wakati wabunge hao ambao walishavuta posho wakijikarantini, wananchi wao walikuwa barabarani wakitafuta riziki zao za kila siku.
Baadhi ya wabunge waligomea amri hiyo. Sote ni mashahidi kilichowakuta akina Lijualikali, Silinde na wenzao.
Wabunge wa CHADEMA hukatwa shilingi milioni moja kila mwezi kutoka kwenye mishahara yao. Je, makato hayo ni makato ya hiyari ambayo yanatawaliwa na misingi ya haki na Uhuru?
Maendeleo
CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kilipaswa kuonesha kwa vitendo kuwa ndio mbadala wa CCM. Pamoja na ruzuku, michango na miradi, ofisi ya makao makuu ya chama hicho haiakisi dhana ya maendeleo. Wengi wa wabunge wake hawaoneshi ubunifu kwenye majimvo yao ili tuone kwa vitendo kuwa hawa ni watu wa maendeleo.
Je, kaulimbiu yao sio ghiliba kwa wananchi?
Povu, utopolo na ugoro: RUKSAAA
Amani Msumari
Tanga