Miwatamu
JF-Expert Member
- Oct 2, 2012
- 1,450
- 487
Kuhusu aina ya vijana aliotaka kuona, Mwalimu Nyerere alisema: Tunataka kuona katika Taifa hili vijana jeuri na wenye kujiamini; si vijana waoga, akina ndiyo bwana mkubwa; vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya Kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa.Alisema Mwalimu: Ni kazi bure kwetu, na kwa kweli ni ubatili mtupu, kuwa na Taifa lenye silaha za kisasa lakini vijana wake ni waoga.Wanajamvi, kwa maneno haya ya baba wa taifa, bado ndani ya CCM tunatumaini la kupata vijana wa style hii?Nawasilisha.Chanzo: Raia Mwema 19 Octobar 2012