Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Mkuki kwa Nguruwe kwa binadamu mchngu, watu kibao wamechafuliwa kule. Ila siku itakapokuwa zamu yako ama ya ndugu wako wa karibu ndio utajua kuwa ile web haifai.

We kama ni mchafu, mchafu tu. Mtu hawezi kukuchafua kama hauko karibu au ni sehemu ya uchafu.
 
Hatuwezi kukosa utetezi.

Tunapigia hili kelele kwa sababu, IS THE PRESIDENT.

Simple hatukurupuki.

Walimu wetu wa Siasa na JKT, waliTUFUNDISHA na TULIWAELEWA.
 
Maadili unayaona leo?
mbona hapa yanabadikwa mapicha machafu machafu hamuoni kama ni kinyume na maadili yatu watz......

Lete hiyo website tafadhali. Ya ze utamu. haipatikani au kwa ku-google! Wame-change url?
 

Post of tha day!

MODS sidhani baada ya mkuu Shishye kuiweka bayana hoja, kuna hoja iliyosalia. Nadhani itakuwa ni jambo la busara mkiufunga mjadala huu hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo.


Naomba kusikilizwa.
 
Duh, Everybody is here..........!


911, araway, Baba_Enock, Bonnie1974, Brooklyn, Chakaza, Choka mbaya, cool girl, Domo Kaya, Giroy, Ibrah, jethro, Kalunguyeye, Kang, Kijakazi, Killuminati, KYACHAKICHE, Magehema, Malunde-malundi, mduduwashawasha, Mfamaji, mmasaihalisi, Mongoiwe, Mtindiowaubongo, Mtu B, Mutensa, Nyambala, Pipiro, Robin, shishye, SMU, Tuntu
 
iko wapi hiyo picha; iwekeni tuichambue vema hapa or else kaichambulieni huko huko the utamu
 

Including you!😱
 
MOD please fungeni hii thread maana ni kama ina promote cheaply the so called zeutamu....
 
watu mnang'ang'ania kuandika hii thread ni kuitangaza hiyo website ila hamuoni tatizo lenyewe,imekuwa tabia yetu kuanza kutibu dalili badala ya kutibu ugonjwa na hili ndilo tatizo letu.

Sipendi watu wakaangalie hizo picha,ila nachosema ni pale picha zitakapoanza kusmbazwa kwa njia ya mtandao,athari zake ni kubwa zaidi,nilipoamua kuanzisha hii thread ni kutoa mwanga kwa watu kulaani kitendo hicho

Na kama mnaona ninaitangaza hiyo wbite basi mnakosea sana,ni nani asiyeifahamu ?na kwa taarifa yenu siyo mara ya kwanza kwa sisi kuijadili website hiyo na kama watu kuifahamu waliifahamu enzi hizo,so msinishupalie

Kwa mara nyingine Tena Nakusihi sana mwenye Picha hizi usiendele kuzisambaza kwa watu na the owner wa blog hiyo naomba kama Picha bado ipo iondoe!

Nakuomba sana mkulu wa Ze utamu,Please I beg you!


Na nimeanza kupitia thread ile tuliyomzungumzia Shigongo kuhusiana na website yake na magazeti yake..Am now so worried coz i couldnt expect tunaweza fika hapa na hii yote imechangiwa na tabia yetu ya kuzoea kukaa na uchafu!

sijaandika Url yake,hivyo sijaitangaza ila nimesema nilcihokiona!
 
Oyaaah ...thats too much jamani....hivi serikali imeshindwa fanya kitu? UwT wapo kweli....ile ni kashfa kwa watanzania na raisi oohhh....nililalamika sana waliponiweka kule. Siku hizi ukienda party usikae na kufurahi na wadada utajikuta umepigwa picha na kuwekwa kule. hii kitu haisaidii kitu kabisa..Nsia Swai na hata wale wadada wa IFM maisha yanaendelea....lazima kitu kifanyike kule....na muhusika afikishwe kwa pilato.
 

Hapa wewe unafikiri kuna UWT? hakuna kitu bongo bana wizi wizi na ujanja tu....wataalamu wenyewe wa mambo ya IT wanasinzia tu tumewapeleka kusoma nje wamerudi wanashindwa kazi unategemea wanaweza wakaufungia mtandao huo?
 
LAKINI seriously mbona watanzania tumezidi kwa unafiki..Now I SALUTE FMES, viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe.

Ok..The Institution of the Presidency ought to be respected. Lakini, hamuoni kwamba huyu kiongozi wetu ndo anapaswa kuwa jemedari wa vita dhidi ya haya mambo? sasa yeye akikaa kimya wakati ndo inabidi ayazuie unategemea nini? Labda wakiamuandika yeye itakuwa wake up call to do the needful. Who knows?

Ohh..juzi picha za Mange Kimambi..ziliwekwa pale..watu wakamtukana..hata hapa JF kuna thread... (watanzania hawa hawa) eti ni malaya hastahili sympathy..as if her private life inakupa passport ya kumtuhumu na kumdhalilisha. mtoto wa watu ..au kwa vile JK yeye ni msafi ndo anatetewa hapa?.

Tulivyo na akili finyu..kesho Kutwa RAIS akitajwa kwenye ufisadi tutasema hapana ni "kuvuka mipaka". Ohh Yes, WARIOBA ALISHASEMA ETI KUMTUHUMU RAISI (HATA KAMA ALIIBA) NCHI INAWEZA KUYUMBA. Hawa ndo watanzania wetu hawa!

Katika TANZANIA kama viongozi wetu wangekuwa wanajua wajibu wao..tusingekuwa tunafika huku. (Ze Utamu anaweza kuwa kavuka mipaka) lakini ukweli unabaki pale pale..we are not serious wananchi kwa viongozi. yaani nchi imejaa wasanii tupu..sisi wananchi na viongozi wetu....ndo maana tunachezeana akili..hakuna aliye serious.

Hivi hujiulizi..tukipata ugeni wa raisi kutoka nje (kama Bush mwaka jana) ndo bara bara ya airport inafukiwa mashimo..mitaa inakuwa misafi....akiondoka tunarudi kwenye uchafu wetu tuliouzoea. Kiongozi hata kiwa mwanamziki kutoka nje..akienda kuitembelea mwananyamala hospital..ndo watafagia..wagonjwa watapewa chakula kizuri na mashuka mazuri..akiondoka..tunarudi kule kule....Duh..bongo tambarare...

Folks, the problem is bigger than mh. mkuu wa kaya na Ze utamu. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
 
Nashindwa kushangaa kabisa sisi watz, sijui tukoje!...ndo maana hata mkuu NN kaamua kusema ''Miafrika Ndivyo Tulivyo''

Mambo ya ze utamu hayaanza leo, kuchafuliwa watu bila sababu yoyote hakujaanza leo, mipicha ya ajabu ajabu huko haijaanza kuwekwa leo na ofcourse nadhani hata UWT walishaiona hiyo site na mauchafu yake.......lakini wakaona ni vyema na inawapendeza machoni mwao tu pengine kwasababu haikuwachora wao au watu wafamilia zao au ndugu zao wa karibu, so wao walienjoy tu mbali ya kwamba watanzania wengi walishalalamika sana na kuomba kuungwa mkono kupambana na hiyo website but no one heard their voices!....kama unataka kupata ushahidi wa hili soma hapa https://www.jamiiforums.com/habari-...e-utamu-blog-ni-aibu-kubwa-mno-kwa-taifa.html

Sasa leo mamba huyo huyo aliyewajeruhi watz (watoto) kibao kamjeruhi mkuu wa kaya, eti watu wanakimbilia JF kuomba support yakumwinda na kummalizia mbali mamba huyu.....!mlikuwa wapi wakati anajeruhi na kuwaumiza vibaya watoto wafamilia yake (mkuu wa kaya i.e watanzania waliolalamika)? Huu si unafiki wa hali juu kabisa wandugu? Tutaendelea kuact like this mpaka lini? na je tutafika kweli kwa mtindo huu? yaani ugonjwa au tatizo au issue nyeti mpaka imkumbe a very sensitive personal ndo mnaanza kukimbia kimbia kutafute marobaini?

Kwenye link hapo juu kuna Thread tatu zilizo unganishwa pamoja zote zinaihusu Ze utamu, waanzilishi ni WOS, Jokathesi na Bibie! Hawa wote walianzisha thread hizo wakiinyesha kukerwa kwao na hii kitu Ze utamu! Je, mkuu Gembe & Co hamkuona hii kitu kuwa ni mbaya au didin't you think kwamba kulikuwa na risk ya hata sensitive people kujakudhalilishwa huko na hivyo the need ya kukimbilia kwa kina Mwanakijiji na Robot wasaidie kabla mambo hayajawa mabaya hivi kuliko sasa kuzima moto kwa Petrol wakati maji yameshamwagika? hii nadhani inatokana na kukosa vision au kuwa wanafiki na tabia ya kujipendekezapendekeza....labda coz of 2010 issues sijui!

Ni vizuri watanzania tuwe na vision kubwa, tuache unafiki matatizo yanapotokea hata kama yanahusu a low class tuyashughulikie consistently kuliko kuwa na double standards in dealing with our problems!

Notwithstanding my comments above, pole sana mkuu wa kaya kwa yaliyokukuta lakini kumbuka wanao wamekuwa wakiumizwa kihivyo kwa muda mrefu sana just for your information kama UWT hawakukutonya before.....!

Cheers!
 


masa,

lazima tuyakubali mabadiliko ya teknohama. Hatuwezi kuyakimbia. Enzi za gazeti moja la uhuru na mzalendo kama only source of news halipo tena. Kikubwa tujifunze kuacha unafiki na kuwa realistic na maisha yetu.

Ukipigwa picha unakula bia yako..huwezi kuwazuia watu ku-comment. Na hiyo nd inakuonyesha watu wanafikiria nini juu yako katika jamii inayokuzunguka. Ukipiga picha kama nsia swai, sorry buddy..thats self assumption of risk..unakuwa unajua what might happen.

Tatizo tuna madhambi mengi tunaogopa yatawekwa hadharani. Waafrika hatujazoea transparency na tunapenda kuishi maisha ya vivuli na double standards sana. We have to learn. We might succeed. Ila ndo hivyo teknohama imebadilisha maisha yetu now and forever. Ni kuikabili tuu kwa uwazi..siyo kutishana kwa kupelekana kwa pilato..maana, i am afraid hata hiyo sheria itakuwa haipo...
 
Wajameni!!! hapo ni kwamba nimeshangaa kisukuma, kweli me nilidhani kuwa zeutamu ni mtambo wakuwareekebisha watu tabia tabia furani chafu chafu na wasio jiheshimu na kujistili utu wao.sasa imefikia mpaka kwa JK? ni kuwa zeutamu imekiuka misingi ya huru wa vyombo vya habari kabisa. Kwa utaaramu wangu ktk kuichunguza iyo picha nimegundua kuwa huyo bwana amepachika kichwa cha JK. kwani kuna sehemu inaonekana wazi kabisa kuwa sio JK. na huyo mtu alie weka iyo picha hapo kwataarifa yake nikuwa anajifunza iyo kazi hajui. na ni mmoja kati ya wale watu wenye mipango ya kumchafua jamaa kwani hiki ni kipindi cha watu kujiandaa kabla ya uchaguzi mwakani kwaivyo wametumia hii web kwani wanajua fika % ya watanzania wengi hu visit hiyo web every day kuchwapo kutaka kujua ni nani leo zamu yake na alidfanya upumbavu gani mpaka akanaswa na watu mpaka wa mupload kwenye zeutamu. Ila mtu alie upload iyo picha hajashinda chochote bari kashindwa tena mno na ustaarabu umemshinda tena sana tu. watu wawe na heshima na vyombo vya habari wajameni. wabheja sana. Lekanize
 
Hii inanikumbusha suala la shamba la wanyama; kwa kweli ni aibu na kitendo cha kulaaniwa na kupingwa.

Acha unafiki! si wewe uliedai kuweka picha za Kikwete akiwa kwenye "compromise situation" kwenye thread ileee.

Mtu kwanza kupingwa na kulaaniwa ni wewe... pathetic!
 
Nye! Mwee! Ti! Mwenzenu nimesikia kichefuchefu kabisa!!
Lekini viongozi wetu wameyalea haya mambo ya kissshenzi kabisa! ni mara ngapi picha chafu zimeanikwa wazi kwenye magazeti ya udaku wamekaa kimya tuu!! Wahenga walisema "mchelea mwana kulia hulia yeye" yamewkuta sasa, mkulu kaadhiriwa. Hata UWT wafanyeje watakuwa hawatibu chanzo cha ugonjwa watakuwa wanakamua upele tu wa mtu mwenye TB.
 
Kilichofanyika si Ubinadamu ni unyama wa mwisho kumfanyia mtu yoyote yule sio rais tu hizi ni chuki pia kuna uwezekano kuna watu wenye uwezo au madakara nyuma yake ,Hastahiki kudhalilishwa kiasi hichi ni chuki za kundi fulani zaidi ya kundi jengine .
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…