Kitendo cha wana synnovate kuja juu kwa hasira nyingi za kufikia kutaka kushitaki vyombo vya habari vilivyoripoti habari zilizotolewa na mbowe kwenye mkutano wa hadhara kinatia shaka sana kama synnovate ni taasisi huru kama inavyodai. sababu ya kuoji ili ni kuwa kulikuwa hakuna sababu yeyote kwa synnovate kupaniki kiasi hiki na kuja juu kutishia kushitaki vyombo vya habari vilivyoripoti kauli ya mbowe. wasiwasi wangu ni kuwa synnovate wameshakula pesa za CCM km ambavyo wamekuwa wakifanya miaka ya nyuma kwa ajili ya kuwafumba watu macho sasa walioliwa pesa zao CCM wanakuja juu na ndio maana tunashuudia synnovate kupaniki namna hii. Taasisi yeyote ambayo aipokei pesa kutoka CCM ilikuwa haina sababu za kupaniki hovyo namna hii. Taasisi inayojieshimu itakanusha habari na kuonyesha ukweli huko wapi ili watu waamue pumba ni zipi na mchele ni upi?? na siyo kupaniki namna hii na kuanza kuvitisha vyombo vya habari hii inaonyesha wazi kuwa taasisi hii huenda ikawa inatumiwa CCM na siyo huru km inavyodai na hasa ukizingatia matamko ya nyuma ya ajabu ajabu kuwa watanzania wanachukia utendaji wa serikali na mawaziri wake lakini wananchi wanampenda sana kikwete inaonyesha wazi kuwa wana bwana wanaemtumikia na si Taasisi huru km ambavyo wangependa tuamini.