Je, Spika kalidanganya bunge ?

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizima hoja ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema) kuhusu tuhuma dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mchakato wa zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya taifa.

Akielezea kwa nini alichukua hatua hiyo Spika amedai Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama imemshauri kuwa ni busara mradi huo usichelewe, uachwe uendelee hadi mwisho na kama hapo baadaye itaonekana kuna tatizo, kamati itarejea kuijadili.

Tatizo ni kwamba kulingana na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, ushauri kama huo haukutolewa na wao kama kamati. Inasadikiwa kuwa kamati iliyomshauri Spika kuchukua hatua hiyo ni kamati ya wabunge wa CCM chini ya Waziri Mkuu.

wabunge wa CCM walikuwa wakitafuta msimamo wa pamoja wa namna na kumdhibiti Dk. Slaa atapowasilisha hoja binafsi inayotaka maelezo ya serikali kuhusu hatua ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mkachato wa utengenezaji wa vitambulisho vya taifa.

Lengo kuu ya hii kamati ya Wabunge wa CCM inaonekana ni kujaribu kumlinda na kumwokoa mhusika na kashfa ambayo ingemwandama. Je hii haithibishi ule woga wa wengi wetu kuwa wabunge wetu wako pale kwa maslahi ya CCM na si wananchi wala taifa?

Je, ni adhabu gani inafaa apewe Spika ikithibitika kadanganya bunge.
 
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizima hoja ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema) kuhusu tuhuma dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mchakato wa zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya taifa.

Akielezea kwa nini alichukua hatua hiyo Spika amedai Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama imemshauri kuwa ni busara mradi huo usichelewe, uachwe uendelee hadi mwisho na kama hapo baadaye itaonekana kuna tatizo, kamati itarejea kuijadili.

Tatizo ni kwamba kulingana na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, ushauri kama huo haukutolewa na wao kama kamati. Inasadikiwa kuwa kamati iliyomshauri Spika kuchukua hatua hiyo ni kamati ya wabunge wa CCM chini ya Waziri Mkuu.

Lengo kuu ya hii kamati ya Wabunge wa CCM inaonekana ni kujaribu kumlinda na kumwokoa mhusika na kashfa ambayo ingemwandama. Je hii haithibishi ule woga wa wengi wetu kuwa wabunge wetu wako pale kwa maslahi ya CCM na si wananchi wala taifa?

Je, ni adhabu gani inafaa apewe Spika ikithibitika kadanganya bunge.

Huyu ameshakuwa dikteta kwa kuzuia mambo mengi ambayo yana maslahi makubwa kwa nchi yetu kujadiliwa kwa kina. Tungekuwa na bunge huru na lenye nguvu basi wangeshampigia kura ya kutokuwa na imani naye na kumuengua katika nafasi hiyo, lakini kwa kuwa Bunge letu ni rubber stamp ya CCM na serikali basi anaweza kufanya lolote lile ili kuminya uhuru wa Bunge huku akijua fika hakuna lolote litakalomfika.
 
Huyu ameshakuwa dikteta kwa kuzuia mambo mengi ambayo yana maslahi makubwa kwa nchi yetu kujadiliwa kwa kina. Tungekuwa na bunge huru na lenye nguvu basi wangeshampigia kura ya kutokuwa na imani naye na kumuengua katika nafasi hiyo, lakini kwa kuwa Bunge letu ni rubber stamp ya CCM na serikali basi anaweza kufanya lolote lile ili kuminya uhuru wa Bunge huku akijua fika hakuna lolote litakalomfika.

Kufuatana na kauli ya Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF), mmoja wa wajumbe wa kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ni kuwa hawakujadili kuhusu kumshauri spika kusimamisha hoja ya Dk. Slaa hadi mchakato wa zabuni ya vitambulisho vya taifa ukamilike. Akisisitiza alisema, "Naona maneno hayo yalitokana na vikao vyao walivyofanya na kukubaliana hivyo na kamwe si wazo la kamati,"

Hapa kuna maswali makubwa mawili. Kwanza, kwa nini Spika aruhusu maamuzi ya vikao visivyo rasmi vya Bunge kuongoza bunge - hivi ndivyo kanuni za Bunge zinavyosema ? Pili, hivi vikao vya wabunge wa CCM vinavyofanyika sambamba na vikao rasmi vya Bunge, vinafanyika kikatiba ? Nachelea kusema ni vikao kama hivi vinavyowezesha ufisadi kushamiri kwa kutumiwa kama baraza za kuhalalisha na kutetea vitendo hivyo pamoja na kuzima mawazo huru yasiyoafiki.
 
Last edited:
Chanzo cha yote ni wananchi kuchagua wabunge wa CCM wakiongozwa na mkoa wa DSM ambapo wabunge wote ni CCM.
DSM wanafiki sana tena mno(samahani kama nimetoka nje ya mada)
 
Chanzo cha yote ni wananchi kuchagua wabunge wa CCM wakiongozwa na mkoa wa DSM ambapo wabunge wote ni CCM.
DSM wanafiki sana tena mno(samahani kama nimetoka nje ya mada)

Aliingia kwa mbwembwe kumbe ni wale wale kasoro tarehe. Eti alijiita 'mzee wa standard na speed'. Nilishawahi kusema hapo nyuma, tuna wabunge chini ya moja ya tatu, wengine ni sehemu ya Utawala (Executive Branch) Kupitia chama dola. Kuna haja ya kuweka mabadiliko katika sheria kuruhusu wapiga kura 'kurecall' wabunge wao ambao wanatenda kinyume na matakwa ya wapiga kura. Uganda wanayo hiyo sheria, yania kama Mh. Sita ametenda kinyume, basi mnakusanya sahihi na kupitisha azimio la kumwondoa. Hii itasaidia sana kuondoa watu kuanza kuabudu vyama vyao wakati ni waajiliwa wa wananchi.

Upande wa pili wa shilingi, Hivi jamani haya yataendelea mpaka lini? Kila ikija chaguzi, wapiga kura wanachagua tena viongozi hawa wenye kwikwi za mawazo chanya. Mtu unadiriki kuuza haki yako kwa kubadilishana na pilau, tisheti ya manjano na kofia. Yani unauza uhuru wako kwa miaka 5 kwa bei powa kabisa. Haya yanawezekana Tanzania pekee. Au tumelishwa limbwata? Tujiulize na kuchukua hatua. I seconding KGM Position!

 
Last edited:
Wana Jamii, huyu spika inabidi aangaliwe kwa makini sana. Nafikiri njia pekee ya kurudisha nguvu kwa wananchi ni kwa wananchi wenyewe kujishirikisha kikamili na masuala ya serikali. Wajinga wachache wanapojishughulisha na siasa halafu wajanja wengi wakawa hawana muda na siasa matokeo yake ni serikali na bunge kama la Tanzania. Watanzania shurti tuwe na munkari na nchi yetu, tuwe watu wa kuhoji viongozi tuliowateua. Shadow yuko sahihi, inabidi Tanzania kuwe na namna ya kuondoa monopolization kama Uganda, power to the people, kama tunaona unapiga debe tu bila ya kutimiza wajibu wako tunakuondoa. Wana Jamii, mtanisamehe kwa kuingia mbio mbio bila ya kubisha hodi, hata hivyo hayo ndio maoni yangu. Kila la heri.
 
Huyu Mzee ni Dikteta

Km ni wafuatiliaji wa mikutano ya bunge, mtakumbuka karibu hoja zote ambazo zina maslahi kwa taifa na zimepelekwa kwake na wapinzani ni lazima zipigwe chini kwa visingizo visivyokuwa na mashiko.

Labda mzee sitta ameitikia wito wa mzee kingunge maana kwa taarifa zilizopo, walipoketi ktk kile kikao chao chama mzee kingunge alitoa karipio kali kwa wabunge wa ccm na kusema maslahi ya chama kwanza then ndio waangalie maslahi ya taifa.

Tukiangalia kwa umakini hoja zote walizowasilisha wabunge wale wa3 ni za msingi sn kwa maendeleo ya taifa letu but utashi wa kisiasa za ccm zimetukwamisha.

Tusikate tamaa, tutambue mapambano kuelekea ktk demokrasia ya kweli yanachukua muda mrefu sana na hasa kwa mazingira ya nchi yetu. Tunahitajika kujitolea mali, muda na nafsi zetu ili (wananchi)tuje kuishi km wafalme hapo baadae.

Aluta kuntinua!!!
 


Upande wa pili wa shilingi, Hivi jamani haya yataendelea mpaka lini? Kila ikija chaguzi, wapiga kura wanachagua tena viongozi hawa wenye kwikwi za mawazo chanya. Mtu unadiriki kuuza haki yako kwa kubadilishana na pilau, tisheti ya manjano na kofia. Yani unauza uhuru wako kwa miaka 5 kwa bei powa kabisa. Haya yanawezekana Tanzania pekee. Au tumelishwa limbwata? Tujiulize na kuchukua hatua. I second KGM Position!


Tatizo sio pilau, t-shirt wala jezi wala lolote kama hilo. Tatizo ni hakuna upinzani wenye kuleta matumaini (FULL STOP).

Nakuhakikishia, Mambo hayo uliyoyataja ni vikolombwezo tu katika sherehe nzima ya uchaguzi. Maana hata kama visingekuwepo, wananchi wangechagua CCM tu. Siamini hata siku moja na sikubali kuwa wananchi wa Tanzania hawana msimamo. Nakuomba na wewe usiamini hivyo. Maana ukiamini hawana msimamo, hawana dira na hawana chaguo, utakuwa umekosea sana. Utakuwa umetoka kwenye mstari wa kuchagulika pia. Kama kuna chama cha upinzani kinachodhani waTanzania hawajui kuchagua, kijiangalie chenyewe kwanza. Kiangalie kina nini cha kuchagulika na kama kinaweza kkikawa bora zaidi. Vyama vya upinzani havijafikia kuchagulika (Bahati mbaya sana). Mtalaumu pilau, T-shirt na kila kitu. Ila vitu hivyo havipigi kura. Na kama mnadhani ndivyo vinavyoisaidia CCM, kwanini visisaidie na upinzani pia? Si pilau hata wapinzani wanajua kulipika? Si T-shirt zinatengenezwa popote ambapo wapinzani nao wanaweza kuagiza? Wapinzani waanze siasa za ukweli. Waanze kufanya mambo yakuwaletea ushindi. La sivyo, watabaki kulalamika kila siku. Do justice to this country by being competitive, please.
 
Wabunge wa CCM na Spika wao wako pale kwa maslahi ya CCM naWatawala, Spika huwa analazimika kupokea hoja za upinzani pale maji yanapozidi unga na kwa kuamriwa na Serikali. Si mwankumbuka jinsi alivyobeua madai ya Dk Slaa kuhusu LIST OF SHAME na BoT TWIN TOWR? Alimkatalia Dk Slaa kuwasilisha hoja binafsi kwa madai kuwa hizo ni habari za mitandao ya internet (alilenga JF) na hakuna ushahidi. Zaidi ya hapo alimtisha Dk Slaaa kupeleka vielelezo Polisi (yaani Dk alighushi). Alipoona Wananchi wamejulishwa na wamelipokea kwa maelfu ndipo Bunge likajiingiza kichwa kichwa kwa madhumuni ya kuiokoa serikali.

Spika alinyoosha mikono pale Dk Slaa alipoamua kupeleka hoja yake kwa Wananchi pale Mwembe Yanga. Nadhani Dk Slaa na Kambi ya Upinzani Bingeni watuletee tena Wananchi kama walivyofanya Mwembe Yanga nasi tutajaua la kufanya maana Uchaguzi uko karibu mno ni 2010 yaani mwaka kesho.
 
Wabunge wa CCM na Spika wao wako pale kwa maslahi ya CCM naWatawala, Spika huwa analazimika kupokea hoja za upinzani pale maji yanapozidi unga na kwa kuamriwa na Serikali. Si mwankumbuka jinsi alivyobeua madai ya Dk Slaa kuhusu LIST OF SHAME na BoT TWIN TOWR? Alimkatalia Dk Slaa kuwasilisha hoja binafsi kwa madai kuwa hizo ni habari za mitandao ya internet (alilenga JF) na hakuna ushahidi. Zaidi ya hapo alimtisha Dk Slaaa kupeleka vielelezo Polisi (yaani Dk alighushi). Alipoona Wananchi wamejulishwa na wamelipokea kwa maelfu ndipo Bunge likajiingiza kichwa kichwa kwa madhumuni ya kuiokoa serikali.

Spika alinyoosha mikono pale Dk Slaa alipoamua kupeleka hoja yake kwa Wananchi pale Mwembe Yanga. Nadhani Dk Slaa na Kambi ya Upinzani Bingeni watuletee tena Wananchi kama walivyofanya Mwembe Yanga nasi tutajaua la kufanya maana Uchaguzi uko karibu mno ni 2010 yaani mwaka kesho.


Ibrah thx for the analysis.

Mimi namuomba Dr. Slaa na timu yake kama wamekosa avenue Bungueni, basi waipeleke hiyo hoja jimboni kwa mtuhumiwa na wananchi wake waamue 2010.
 
Kwa maana nyingine kama kuna ufisadi umefanyika basi wabunge wanyamaze kimya tu ili kuacha mchakato uliojaa ufisadi uendelee tu!!! Bunge letu linahitaji spika mpya ambaye atawapa uhuru Wabunge kujadili lolote lile bila ya kuleta udikteta kama afanyavyo dikteta Sitta.

[Date::2/11/2009
Spika azima hoja binafsi toka kwa Slaa, Mdee na Mohamed

Na Leon Bahati, Dodoma

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizima hoja tatu binafsi za wabunge wa upinzani bungeni, ikiwemo ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema) kuhusu tuhuma dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mchakato wa zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya taifa.

Hoja nyingine iliyopanguliwa ni ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), aliyekuwa na pendekezo la kubadili katiba ili viwemo vifungu vya kumbana rais, kwa kuwa na ukomo wa idadi ya mawaziri kwenye serikali yake.

Akielezea juu ya kuizuia hoja ya Dk. Slaa, Spika alisema kamati imemshauri kuwa ni busara mchakato wa zabuni hiyo, kuendelea hadi mwisho ndipo iangaliwe uwezekano wa wazo la mbunge huyo wa Karatu kuzungumzwa.

"Kamati imenishauri kuwa ni busara mradi huo usichelewe, uachwe uendelee hadi mwisho, kama itaonekana kuna tatizo, kamati itarejea kuijadili (hoja ya Dk. Slaa)," alisema Sitta.

Kuhusu hoja ya Mohamed, alisema aliizima kwa sababu mabadiliko ya katiba, hayafanywi kwa mbunge kuwasilisha hoja binafsi.

Hoja nyingine iliyopanguliwa na Spika ni ile ya Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mdee (Chadema) juu ya mgogoro wa ardhi katika aneo la Boko-Chasimba, jijini Dar es Salaam .

Sitta alisema suala hilo haliwezi kujadiliwa bungeni, kwa sababu liko mahakamani.

Hata hivyo, Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF), alipinga maelezo ya spika nje ya bunge kwa maelezo kuwa ametangaza jambo ambalo Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ambayo ilijadili hoja ya Dk. Slaa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Khalifa alisema yeye ni mmoja wa wajumbe katika kamati hiyo na kwamba hawakujadili kuhusu kumshauri spika, asimamishe hoja ya Dk. Slaa hadi mchakato wa zabuni ya vitambulisho vya taifa ukamilike.

"Naona maneno hayo yalitokana na vikao vyao walivyofanya na kukubaliana hivyo na kamwe si wazo la kamati," alisema Khalifa.

Khalifa alisema bado walikuwa wanaendelea kuijadili hoja hiyo na kwamba ilikuwa haijafikia.
 

.............SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizima hoja tatu binafsi za wabunge wa upinzani bungeni, ikiwemo ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema) kuhusu tuhuma dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mchakato wa zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya taifa..............


Tatizo la Slaa ni mhuni. Tena sana. Mimi sijawahi mwona kama mwanasiasa halisi. Anapenda sana "cheap politics", kama walivyo wapinzani wengine pia. Katika lile bunge, mpinzani aliye serious ni mmoja tu, naye ni Cheyo. Ni kwasababu hiyo ndiyo maana watu hamwezi kumuona. Mtokeo yake watu wanaishia kushabikia Muhuni Slaa. Na huyu ndiye anayewapotosha watu wengi sana na kuishia kuchanganyikiwa na baadaye kuipa CCM ushindi wa mteremko.

CCM is there to stay. Kidumu chama! Zidume fikra sahihi za CCM!
 
Matatizo ya Spika wetu si magumu sana kuyaelezea. I will try.

His past, which is not anything to be proud of, has finally caught up with him. He gambled but the fisadis called his bluff and their weapon is his closet - it happens to be full of worms. His futile attempts to to appear what he is definitely not, had managed to hoodwink a few but immediately he touched the wrong nerves, his world came crashing down on him. He found himself left with little choice and chose the way of the coward that he is - if you cant fight them, join them.

In his efforts to salvage a little that remains of his image, he has decided to thrash out at everything - he is cornered and has nowhere else to run to but back to fold to dance to their tune. He has been brought back to earth with the stark reality that he is where he is only because they want him there. They were starting to feel uncomfortable with his lone ranger tactics and so took him to task and reminded him of his obligation as Speaker of the House and who put him there.

CCM ina wenyewe - rub them the wrong way and you wont know what hit you. There is a long list of all those fiery ones who dared but who hears of them anymore. The only ones that are heard are those that had the gut to get out and very few can do that - it requires one allergic to UFISADI. CCM can make or break you if you have something under your blanket for the sacred vow in CCM is - you scratch my back and I will scratch yours - no wonder it is attracting the like.
 
Wapinzani waanze siasa za ukweli. Waanze kufanya mambo yakuwaletea ushindi. La sivyo, watabaki kulalamika kila siku. Do justice to this country by being competitive, please.
Wewe ungeshauri vyama vya siasa wafanye vitu/mambo gani ya kuwaleta ushindi??
 
kapoteza mwelekeo huyu baba...

Mkuu we, jipombelee tuu huyu jamaa yaani hapo ndio yupo kwenye laini ya Sisi.M haswa. Mwanza alitaka kupoteza mwelekeo wamefanikiwa kumweka sawa.
 
Back
Top Bottom