Je Somo la Commerce limekuwa janga la taifa?

manumoo

Member
Dec 4, 2017
18
10
Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2017 yalitangazwa tarehe 8/1/2017. Matokeo hayo yanaonesha ufaulu mzuri kwa shule za binafsi kuliko shule za umma kwani kati ya shule kumi zilizofanya vizuri Tanzania, zote ni za binafsi.

Hata hivyo kwa shule zilizofanya mitihani ya masomo ya biashara inaonesha somo la commerce limefanya vibaya kuliko ilivyotarajiwa. Kwenye shule nyingine commerce imefanya vibaya kuliko hata hesabu na fizikia. Matokeo ya commerce yameendelea kuwa mabovu kwa mfululizo wa miaka kadhaa kwa kidato cha pili na cha nne.

Kwa mtazamo wangu, Kwanini tusitangaze matokeo ya somo hili kama janga la taifa ili kama inawezekana tulete mjadala wa kitaifa? Maana kama tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda, inabidi pia tutengeneze watu makini kwenye biashara ili kuiwezesha Tanzania kuuza bidhaa zitakazozalishwa na viwanda vyetu ndani na nje ya nchi.

Ni wazo langu tu kwamba kama tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda inabidi tutengeneze uwiano mzuri kati ya masomo ya biashara na sayansi maana kuongeza uzalishaji kunahitaji sana kupanua masoko yetu ya nje na ndani ili viwanda vistawi.
 
Serikali imefulia haina kitu mkuu.... magu hataki kusema... anasingizia vyuma vimekaza wakati yeye ndo kakata mirija ya mapato na grants kutoka nje ...sasa ngoja tuisome namba... hakuna ajira.... Kikwete ni jembe tutamkumbuka
 
Serikali imefulia haina kitu mkuu.... magu hataki kusema... anasingizia vyuma vimekaza wakati yeye ndo kakata mirija ya mapato na grants kutoka nje ...sasa ngoja tuisome namba... hakuna ajira.... Kikwete ni jembe tutamkumbuka
Daah inabidi ukatafute Pain killer kichwa kipoe uchangie vitu vinvyohusiana na mada kuu.

Au ndio vyuma vimekukazia kiasi kwamba unachanganya habari za maendeleo ya somo la Commerce na ukosefu wa ajira, mapato na grants?
 
c
Daah inabidi ukatafute Pain killer kichwa kipoe uchangie vitu vinvyohusiana na mada kuu.

Au ndio vyuma vimekukazia kiasi kwamba unachanganya habari za maendeleo ya somo la Commerce na ukosefu wa ajira, mapato na grants?
Sasa commarce ilo soma utaliendeleza bila nguvu ya serikali... kuajiri walimu wa commarce na kuhamasishaa umuhimu wa ilo somo.... Dish limeyumba we jamaaa
 
c

Sasa commarce ilo soma utaliendeleza bila nguvu ya serikali... kuajiri walimu wa commarce na kuhamasishaa umuhimu wa ilo somo.... Dish limeyumba we jamaaa
Kwa hivyo hapa unahisi hayo masomo mengine kuna wahamasishaji kibao wameajiriwa, na hii commerce ndio hawaja ajiriwa ndio sababu wanafunzi wanafanya vibaya?

Naheshimu mchango wako lakini bado haujanishawishi mkuu.
 
Walimu wa commerce na bookeeping ni adimu sana. Baadhi ya shule za kata hazifundishi kabisa hayo masomo kwasababu hiyohiyo ya kukosa walimu.
 
Haya masomo mi hua nayasikia tu, lakini naomba kuuliza UMUHIMU wake ni nini hasa haya masomo mana usikute viongoz wetu wenye dhamana nao ndo kama mimi hapa hawajui umuhimu wa haya masomo na matokeo yake hawayapi kipaumbele!
 
Labda shule hazina walimu wa Commerce na B/Keeping.

Commerce ni moja ya somo rahisi sana.
 
Haya masomo mi hua nayasikia tu, lakini naomba kuuliza UMUHIMU wake ni nini hasa haya masomo mana usikute viongoz wetu wenye dhamana nao ndo kama mimi hapa hawajui umuhimu wa haya masomo na matokeo yake hawayapi kipaumbele!
ww unaishi dunia ipi mkuu km hujui umuhimu wa com na bk yaan hujui wachumi au mabenki yanaendeshwa na watu walio soma chemistry ...hahahaaaa pole sana mkuuu
 
Hili somo la commerce nilikuwa nalipenda sana shuleni bila kusahau pacha wake book keeping,hyo ilipelekea advance kusomea eca
 
Uhalisia ni kwamba uwekezaji kwene hili somo upoje??,
1.walimu wapo Wa kutosha!?
2. Vitabu na VP how the government promoting this subject as important!!
 
Nimesoma eca ilisomo ni gumu Kama ujasoma wanafunzi wengi tunalichukulia rahisi Sana. Wanafunzi tunatakiwa teacher iyo mentality na tuisome A Y'all commerce mziki
 
Serikali imefulia haina kitu mkuu.... magu hataki kusema... anasingizia vyuma vimekaza wakati yeye ndo kakata mirija ya mapato na grants kutoka nje ...sasa ngoja tuisome namba... hakuna ajira.... Kikwete ni jembe tutamkumbuka
Hatuhitaji kumkumbuka Mkwere. Yeye ndiye chanzo chá janta hili
 
Haya masomo mi hua nayasikia tu, lakini naomba kuuliza UMUHIMU wake ni nini hasa haya masomo mana usikute viongoz wetu wenye dhamana nao ndo kama mimi hapa hawajui umuhimu wa haya masomo na matokeo yake hawayapi kipaumbele!
Nadhani haya masomo yana umuhimu mkubwa kwa nchi hii kuliko tunavyoyachukulia. Moja ya nchi zilizoendelea kwa kasi sana ni China. Kwa sasa ina uchumi mkubwa na inashika nafasi ya pili baada ya marekani. Kati ya Benki tano kubwa duniani, nne zina toka China. Na Benki ya kwanza kwa ukubwa inaitwa industrial and commercial bank of china ya pili ni China construction banks cooperation, ya nne ni agricultural bank of China. Ukiangalia hizo bank utagundua hata kwa majina tu ni "strategic banks" Bank hizi haiwezekani kuendelea na kusaidia maendeleo ya nchi kama hazitopata wasomi wa masomo ya biashara. Hata hivyo ukiangalia nchi zinazoongoza kwa biashara duniani ni nchi kubwa tu ya kwanza ikiwa China, ya pili marekani ya tatu ujerumani ya nne Japan na ya tano ni Korea ya kusini. Hizi zote zipo kwenye nchi tajiri duniani. Tanzania ni nchi ya 107 kwa biashara za kimataifa. Bado tu hatuoni umuhimu wa masomo ya biashara?
Kwa hivyo hapa unahisi hayo masomo mengine kuna wahamasishaji kibao wameajiriwa, na hii commerce ndio hawaja ajiriwa ndio sababu wanafunzi wanafanya vibaya?

Naheshimu mchango wako lakini bado haujanishawishi mkuu.
 
Haya masomo mi hua nayasikia tu, lakini naomba kuuliza UMUHIMU wake ni nini hasa haya masomo mana usikute viongoz wetu wenye dhamana nao ndo kama mimi hapa hawajui umuhimu wa haya masomo na matokeo yake hawayapi kipaumbele!
Nchi zenye ustawi mkubwa wa biashara duniani ni marekani China na japan . hata hivyo nchi zenye uchumi mkubwa sana kwa pato la ndani(GDP) ni marekani China na Japan. Unadhani ni Kwanini? Nchi zenye uzalishaji mkubwa zinaongoza pia kwa biashara. Huwezi kuwa na uchumi wa viwanda bila kustawisha biashara za ndani na nje maana uzalishaji unatakiwa uendane na biashara. Na ni wafanya biashara ndio wanaohamua nini kizalishwe, kwa namna gani, kiasi gani na wakati gani Maana wao ndio wanajua watu wanahitaji nini na wakati gani. Hii ndo maana Nasema kama tunahitaji uchumi wa viwanda lazima tuwekeze kwenye masomo ya biashara na sayansi kwa juhudi kubwa na sio kuwekeza zaidi kwenye masomo ya sayansi tu. Ujinga wetu unaweza kutufanya tuwe Masikini daima.
 
Hatuhitaji kumkumbuka Mkwere. Yeye ndiye chanzo chá janta hili
Mkuu kama nakuelewa vile.

Kwa mtazamo wangu wakati wa JK sekta za kifedha ziliwekeza sana kwenye non-liquidity assets.
eg. Majengo yaliyojengwa kama uyoga n.k.
Kama social funds zetu ziliwekeza kwenye kujenga majengo ambayo sasa hayaleti pesa kama ilivyotarajiwa na kuuzika ni shida. Huwezi kuyawekea dhamana ya mikopo mikubwa ya kufanyia uwekezaji mwingine, n.k.

Banks hazikuwa na mikakati mizuri katika kutoa mikopo yake. Sasa wakati huu yanapo jaribu kufanyika mapinduzi ya msingi ya usimamizi wa banks na sekta zingine za kifedha ndio wanajikuta wapo matatizoni na lazima kutokee mikopo mibaya iaiyolipika kwa wakati n.k.

Kulikuwa na kupika sana data za mapato na madeni ya kampuni zilizokuwa zinachukua mikopo na vitu kama LC(Letter of Credit). Unakuta kampuni zilichukua pesa ambayo kiuhalisia walikuwa hawawezi kulipa au walichukua pesa kwa ajili ya biashara fulani ambayo haipo kabisa au ipo lakini promised return ni ya uongo imepikwa ilimradi mkopaji apate pesa nyingi.

Sasa unapokuja kuimarisha namna ya kuzuia udanganyifu kama huu lazima hayo makampuni yashindwe kulipa na ndio yanaishia kuziletea shida banks, na yenyewe kufa au kufilisiwa, kushindwa kulipa kodi, kupunguza ajira n.k.

Mimi naona kama JK angeendelea vile miaka 10 mingine au angekuja Magufuli na kuendeleza mambo yale nchi ingejikuta inapitia njia ya Ugiriki, na Cyprus.

NB: Mimi sio mchumi. Naweza kuwa sipo sahihi lakini hii ni uchunguzi au mtazamo wangu mdogo hasa unao tokana na kuona haya madudu ya kupika data za kuombea mikopo. Kuona sasa watu wanavyoshindwa kuuza au kupangisha majengo yao au kuchukulia mikopo. Na hizi property kama hayo majumba na viwanja visivyouzika kirahisi ndio tunaita non-liquidit assets.
Cc: manumoo , PainKiller
 
Umesema wewe sio mchumi? Basi dont try to be a wise guy!Usinihubirie fake analysis kuhusu mambo ya kiuchumi. Serikali iwe ya mkwere au ******** walikuwa na wajibu wa kuhakiikisha hakuna makosa yanayotokea popote.
 
Back
Top Bottom