Mundali
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 749
- 164
Katika mchakato huu wa uchaguzi, mgombe wa chama cha mapinduzi amesikika akitoa ahadi kemkem, kule atawapa meli, wengine maji ya kudumu na kadhalika.
Kinachonishangaza ni kwamba utekelezaji wa ahadi zake unategemea wafadhili zaidi kuliko ubunifu wa vyanzo vya mapato vya ndani. Hali hii haina tofauti na mvulana anaemuahidi rafiki yake wa kike mkufu wa dhahabu akitegemea kuomba fedha kwa baba.
JK hayo ni mawazo ya kitumwa, amka ndugu yetu hakuna mjomba toka nje atakayewapa maji watanzania bila kuwachuna. Nakumbuka msemo wako "ukitaka kula sharti nawe uliwe" angalia usije ukaliwa wewe na ukaishia kunawa tu.
JK japo ubunifu kidogo tu, misamaha ya kodi inazidi makusanyo! Huoni haya mabo?
Ati elimu bure haiwezekani, bila aibu wewe na kinana mnatamka maneno hayo. Mnaweza kuwaonesha watanzania risiti mlizolipiwa ada na wazazi wenu? Mbona ninyi mlisoma tena si bure tu, na posho za kununulia sabuni na kadhalika mlipewa, bila kusahau usafiri bure kutoka na kwenda mashuleni. Mnafikiri wadanganyika wamesahau "TRC warranties".
Tena hata hamumwogopi Mungu ati Slaa anawadanganya wananchi, hapo nani hasa mwongo? Nyerere alitoa wapi pesa ya kuwasomesha bure JK?
Mmeshindwa kaeni pembeni waacheni wanaoweza waongoze!
Kinachonishangaza ni kwamba utekelezaji wa ahadi zake unategemea wafadhili zaidi kuliko ubunifu wa vyanzo vya mapato vya ndani. Hali hii haina tofauti na mvulana anaemuahidi rafiki yake wa kike mkufu wa dhahabu akitegemea kuomba fedha kwa baba.
JK hayo ni mawazo ya kitumwa, amka ndugu yetu hakuna mjomba toka nje atakayewapa maji watanzania bila kuwachuna. Nakumbuka msemo wako "ukitaka kula sharti nawe uliwe" angalia usije ukaliwa wewe na ukaishia kunawa tu.
JK japo ubunifu kidogo tu, misamaha ya kodi inazidi makusanyo! Huoni haya mabo?
Ati elimu bure haiwezekani, bila aibu wewe na kinana mnatamka maneno hayo. Mnaweza kuwaonesha watanzania risiti mlizolipiwa ada na wazazi wenu? Mbona ninyi mlisoma tena si bure tu, na posho za kununulia sabuni na kadhalika mlipewa, bila kusahau usafiri bure kutoka na kwenda mashuleni. Mnafikiri wadanganyika wamesahau "TRC warranties".
Tena hata hamumwogopi Mungu ati Slaa anawadanganya wananchi, hapo nani hasa mwongo? Nyerere alitoa wapi pesa ya kuwasomesha bure JK?
Mmeshindwa kaeni pembeni waacheni wanaoweza waongoze!