Je, Shisha ni nini? Madhara yake ni yepi?

Je, Shisha ni nini? Madhara yake ni yepi?

Habari wanajamvi,

Hivi sasa kuna mazongezonge yanaendelea kuhusu shisha. Huu mjadala wa shisha ni mpana na mrefu sana. Wakati hayo mazongezonge yakiendelea hebu ngoja tuulizane hivi shisha ni madawa ya kulevya au ni kweli shisha ina madhara makubwa kuliko bange au sigara? Mbona ilikuwa inavutwa hadharani? Hivi ni kiwango gani cha kilevi kilichoko kwenye shisha ambacho kinaruhusiwa au kisichoruhusiwa?


Mbona katika orodha ya madawa ya kulevya iliyo katika Sheria Kuu ya Madawa Na Uzuiaji Wa Usafirishaji Wa Madawa Haramu shisha haijaorodheshwa?
Kuna kipindi Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani ya mwili na mfumo wa hewa, Meshack Shimwela alisema madhara ya shisha ni kama yale yanayosababishwa na uvutaji wa sigara pengine na zaidi kutokana na kilevi hicho kuwa na tumbaku nyingi.
Mwanzoni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitangaza kupiga marufuku uvutaji wa shisha katika maeneo yote ya Jiji la Dar sambamba na hilo agizo lipo agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alivitaka Vyombo vya Dola nchini kuwachukulia hatua kali za kisheria watu watakaobainika kujihusisha na Matumizi ya Shisha.

Juzi hapa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema atamwajibisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda iwapo hatasimamia ipasavyo kukomesha matumizi ya dawa za kulevya aina ya shisha.

Hatua hiyo inatokana na kauli ya Makonda kuwatuhumu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Sirro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kamishna Msaidizi Suzan Kaganda, kulegalega kusimamia suala hilo huku akihofia wanaweza kuwa wamehongwa na watu waliotaka kumhonga lakini akakataa.

Binafsi ningeomba Mamlaka ya Chakula, Dawa na Lishe itufahamishe kama kweli hii shisha ni kilevi. Naona kama kuna jambo linalohusu matumizi ya shisha halijaeleweka vizuri na wahusika ambao ni TFDA, polisi na Mamlaka zingine.

Hizi taasisi zinaonekana zinafahamu kwamba kuna ombwe fulani katika kutekelezaji agizo la uzuiaji wa matumizi ya shisha na hawajatoa tamko lolote ila wameachiwa polisi wakamate watu. Hao polisi nafikiri wanajiuliza kama iwapo wanayo mamlaka ya kukamata kitu kisichojulikana wala kuelezwa kwamba ni madawa ya kulevya kwa mujibu wa sheria.

Vile vile nafikiri polisi wanajiuliza iwapo ukimkamata mtu na kumfikisha mahakamani pasi kuwepo kwa sheria itakuwa imetenda haki?
 
Ni kiburudisho kama Soda na unga wa soda unatokana na mmea aina ya Coke jamii ya ya cocaine upo hapo,shisha madhara yake kwanza ile kulamba mate ya mwenzako siyo vema huwa wanapokezana kale kamlija kutumia
 
Ndiyo, Kwa mujibu wa Serikali ya Viwanda, inayoamini Maendeleo bila Uhuru wa Habari na Demokrasia ya Vyama vingi.
 
Kwanza ipe heshima yke bangi

Bangi ni mmea 'herb'
Bangi haina chemicals

Bangi ni dawa ya saratani

Hakuna aliyewahi kuumwa kwa bangi ,hakuna nikotin mule

Herb
 
upload_2016-11-18_6-23-7-jpeg.435786

Shisha ni kiko tu ambacho kinaweza kutumiwa kuvutia tumbaku, ila kuna watu wachache wanaotumia kiko hicho kuvuta madawa ya kulevya kama ambavyo, watu haohao, wanavyotumia mabomba ya sindano kujidunga hayo madawa ya kulevya !

NB: Huwezi kupambana na wauza madawa ya kulevya kwa kuzuia uuzaji wa mabomba ya sindano wala viko vya maji, aka shisha!
TUSIDANGANYANE!
 
Shisha ni utamaduni wa kihindi na kiarabu ktk kuvuta na wala si madawa ya kulevya ila ni aina ya starehe huko kwao kama ulevi Fulani hivi.

Ila utundu wa bongo unaweza kukuta vijana wanaharibika.
 
Matatizo ya foleni mashimo barabarani mifereji michafu wanafunzi kukosa usafiri nakadhalika, ni makubwa katika jiji la Dar kuliko SHISHA.
 
Kumekuwa na mjadala mpana sana kwa siku za karibuni kuhusu Mapambano dhidi ya matumizi ya Shisha katika mkoa wa Dar.
Hoja ikiwa ni namna mapambano yalivyo, Msukumo wa vita hiyo unapotokea na Mafanikio ya vita hiyo.
Binafsi naunga mkono vita hii dhidi ya shisha.

Shisha ni aina ya starehe, ulevi au nakishi inayotumika kwa kunyonywa mvuke au moshi mdomoni kupitia kiko maalum kilichounganishwa na mrija mrefu kutoka kwenye Chungu au birika maalum linalochakata mchanganyiko fulani wa kemikali zenye kustarehesha, kulevyia au kusisimua.
Ni starehe ya gharama, ipo kwenye maeneo fulani ya kumbi za starehe na wateja wake wakubwa ni watu wenye Asili ya Kiasia. Nadhani huko kwao ni starehe ya Asili, ipo sana au kifahari.
Kwa hapa Tanzania ni jiji la Dar tu ndio ipo, labda na maeneo machache sana katika mikoa mingine.

Nimejaribu kufuatilia kwa kina sana kutaka kujua kuhusu kiini cha Shisha kupigwa marufuku, na mara zote sababu ikielezwa kuwa ni madhara ya Kiafya yanayotokana na Matumizi ya Shisha.
Bahati mbaya sana madhara yote ya Kiafya yanaelezwa kuletwa na Shisha pia huletwa pia na Pombe(Kilevi) na Sigara(Tumbaku).

Kwa kifupi kabisa Madhara ya Sigara ni makubwa zaidi na zaidi kuliko Pombe au Shisha. Lakini pia madhara ya Pombe ni makubwa zaidi kuliko shisha.

Mpaka sasa sijajua msingi wa Kuruhusu Pombe na Sigara kuwa halali hapa Tanzania na hapo hapo Shisha kuwa haramu.
 
Habari wanajamvi,

Hivi sasa kuna mazongezonge yanaendelea kuhusu shisha. Huu mjadala wa shisha ni mpana na mrefu sana. Wakati hayo mazongezonge yakiendelea hebu ngoja tuulizane hivi shisha ni madawa ya kulevya au ni kweli shisha ina madhara makubwa kuliko bange au sigara? Mbona ilikuwa inavutwa hadharani? Hivi ni kiwango gani cha kilevi kilichoko kwenye shisha ambacho kinaruhusiwa au kisichoruhusiwa?


Mbona katika orodha ya madawa ya kulevya iliyo katika Sheria Kuu ya Madawa Na Uzuiaji Wa Usafirishaji Wa Madawa Haramu shisha haijaorodheshwa?
Kuna kipindi Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani ya mwili na mfumo wa hewa, Meshack Shimwela alisema madhara ya shisha ni kama yale yanayosababishwa na uvutaji wa sigara pengine na zaidi kutokana na kilevi hicho kuwa na tumbaku nyingi.
Mwanzoni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitangaza kupiga marufuku uvutaji wa shisha katika maeneo yote ya Jiji la Dar sambamba na hilo agizo lipo agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alivitaka Vyombo vya Dola nchini kuwachukulia hatua kali za kisheria watu watakaobainika kujihusisha na Matumizi ya Shisha.

Juzi hapa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema atamwajibisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda iwapo hatasimamia ipasavyo kukomesha matumizi ya dawa za kulevya aina ya shisha.

Hatua hiyo inatokana na kauli ya Makonda kuwatuhumu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Sirro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kamishna Msaidizi Suzan Kaganda, kulegalega kusimamia suala hilo huku akihofia wanaweza kuwa wamehongwa na watu waliotaka kumhonga lakini akakataa.

Binafsi ningeomba Mamlaka ya Chakula, Dawa na Lishe itufahamishe kama kweli hii shisha ni kilevi. Naona kama kuna jambo linalohusu matumizi ya shisha halijaeleweka vizuri na wahusika ambao ni TFDA, polisi na Mamlaka zingine.

Hizi taasisi zinaonekana zinafahamu kwamba kuna ombwe fulani katika kutekelezaji agizo la uzuiaji wa matumizi ya shisha na hawajatoa tamko lolote ila wameachiwa polisi wakamate watu. Hao polisi nafikiri wanajiuliza kama iwapo wanayo mamlaka ya kukamata kitu kisichojulikana wala kuelezwa kwamba ni madawa ya kulevya kwa mujibu wa sheria.

Vile vile nafikiri polisi wanajiuliza iwapo ukimkamata mtu na kumfikisha mahakamani pasi kuwepo kwa sheria itakuwa imetenda haki?
Sinui hii kitu.. Tena kama ipo nionje maana hata taasisi ya tfda wapo kimyaaa... Je inatokana na mchicha?
 
Wataalaam wetu wamekua ghasi kutufahamisha madhara kati ya shisha na sigara ila wameacha majukumu yote kwa wanasiasa. Wananchi tunahitaji ufafanuzi wao.
 
Shisha ni KIKO ambacho hutumia kuvutumia tumbaku na kilianza kutumika tangu miaka 1600s huko arabun na nchi nyingne za ulaya.Kutoka katika KIKO kuja modern ambayo ni shisha inayotumia gas au umeme ili kurahisisha uvutaji wa tumbaku.POINT ya msingi je? SHISHA INAUHUSIANO GANI NA MADAWA YA KULEVYA? hakuna maana hapo jamii nying za kiarabu wanatumia shisha kama chombo cha kuvutia tumbaku na pia hotel kubwa kubwa zipo kwa ajili ya matumizi hayo tunapobadilisha maana tu pale inapotumika tofauti NA vijana wanaotumia unga na bange JE UNAMTHIBITISHAJE HUYO MTU KATUMIA SHISHA AU KIKO KAMA CHOMBO CHA KUVUTIA BANGI AU COCAINE?

Kuna michanganyiko mingi sana mpaka radha ya kitu ambacho utatumia katika shisha yako vitu vingi ni vya asili ya kiarabu mpaka kuna mchanganyiko wa ndizi na tikiti maji upo yote katika kuleta radha tu.

Point ya msingi ni hii hapa kiafya kama itatumika kwa mtu zaidi ya mmoja ile pipe yake HEPATITS,INFLUENZA,TUBERCLOSIS,INFLUENZA,H.PYLOL na magonjwa mengne hyo ndio point ya msingi hakuna kingne zaidi ya hicho
 
.................................
..........................
Point ya msingi ni hii hapa kiafya kama itatumika kwa mtu zaidi ya mmoja ile pipe yake HEPATITS,INFLUENZA,TUBERCLOSIS,INFLUENZA,H.PYLOL na magonjwa mengne hyo ndio point ya msingi hakuna kingne zaidi ya hicho

Hata mahotelini tunachangia sahani, vikombe, nyuma na vijiko! Cha msingi ni kanuni gani za usafi zinatumika!!!?
 
Back
Top Bottom