Mwenyezi Mungu amemuumba binadamu kama kiumbe bora kabisa dunia na kutenganisha kati ya Mwanaume na Mwanamke, na katika imani zilizonyingi zinatambua uhalisia huo.
Sasa basi ukiona jinsia moja inakuwa na kigeugeu katika jambo fulani mpaka kujitoa ufahamu wa kutokuwa sasa na jinsia yake halisi basi hapa si Mwenyezi Mungu ndiyo kakosea kumuumba binadamu huyu bali tu ni binadamu mwenyewe kutaka kupambana na tamaa za maisha yake ya kidunia, na adhabu kuwa utakuwa juu yake kama si duniani hapahapa basi itakuwa huko ahera ama kotekote.
Sakata la Richmond, hii ni moja kati ya Kashfa nyingi katika kumbukumbu ya Taifa letu na itaendelea kuwaandama Chama Tawala katika kipindi chote cha utawala wao mpaka pale wale wote wahusika wawekwe wazi na si kupiga kelele tu Mtaani kama Daktari wa sheria anavyopiga kelele popote pale asimamapo baada ya kuona kivuli cha mtu furani.
Mimi ninamuomba huyu Daktari wa sheria atoe yote hadharani, je ilikuwaje, nani alihusika, nani alikula pesa, kiasi gani nakadhalika. Ni aibu sana kama kweli mtu furani anasemwa alihusika lakini mpaka sana bado hajafikiswa mahakamani. Hii inamaanisha kwamba vile wanavyoubiri kwenye majukwaa si ya kweli kabisa.
Daktari wa Sheria kama kweli huyu mtu unaamini ni mtuhumiwa wa kashfa hii basi wewe kama mtalaamu wa sheria basi pigania juu chini kabla hata ya uchaguzi kuisha ufikishe mahakamani huyu Mtuhumiwa, KINYUME na hapo basi tulio wengi tunashaangaa na ulijari wako.