Je, Polisi wakiua ni sawa?

Je, Polisi wakiua ni sawa?

kilght

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2012
Posts
635
Reaction score
182
Naona tangu jana hakuna hata anayelaani mauaji ya walioitwa majambazi jana si raia wala si media wala si viongozi wa kisiasa na dini.

Polisi hana mamlaka wala reseni ya kutoa uhai wa mtu.

Pia tuseme tu kuwa inaonekana walifanya makusudi kulipiza kisasi na visasi haviishi.
 
Inaonekana unaamini kuwa hao jamaa ni majambazi. Sasa kama unaamini kuwa jambazi anayeweza kuvamia kituo cha polisi na kuua kila aliyemkuta anaweza kukamatwa kama kuku wa broiler bandani ni kuwa a bit naive.
 
Polisi wakiuwa sawa,wanapowauwa hao wanaohatarisha usalama wao na wetu inakuwa tatizo,hii nchi ina watu wa aina gani?

Aliyekudanganya polisi hana sababu ya kuua mwambie hakupendi. . . . .na kama unataka kufa kirahisi kabisa tafuta silaha kafanye mchezo na polisi
 
Polisi wakiuwa sawa,wanapowauwa hao wanaohatarisha usalama wao na wetu inakuwa tatizo,hii nchi ina watu wa aina gani?
polisi hana mamlaka hiyo mkuu hii ni ichi yenye kutii sheria na taratibu sasa kama tutauana kiivo sijui
 
Embu acheni kudhihaki kazi wanayo fanya askari wetu,inaonekana hata wewe ulie andika hii thread utakuwa ni mualifu,kwa watu kama hao amabo hawaogopi kutoa roho za watu bila huruma unataka waonewe huruma?na mimi natoa lai kwa askari wetu wagongeni bullet tu hao majambazi.
 
Inaonekana unaamini kuwa hao jamaa ni majambazi. Sasa kama unaamini kuwa jambazi anayeweza kuvamia kituo cha polisi na kuua kila aliyemkuta anaweza kukamatwa kama kuku wa broiler bandani ni kuwa a bit naive.
Kuwa objective! hata kama ni gaidi wa kutupwa, as long as amesurrender, huna ruhusu ya kumuua. Sawa walivamia kituo na kuua, lakini walipokwenda kuwakamata wakanyanyua mikono juu! Why kill them? Polisi imekuwa mahakama kutoa hukumu?
 
Kuwa objective! hata kama ni gaidi wa kutupwa, as long as amesurrender, huna ruhusu ya kumuua. Sawa walivamia kituo na kuua, lakini walipokwenda kuwakamata wakanyanyua mikono juu! Why kill them? Polisi imekuwa mahakama kutoa hukumu?

Chukulia aliyeuawa pale stakishari angekuwa ndugu yako jee ungekuwa na huruma na mtu aliyeua nduguyooo?? twende mbele na kurudi nyuma je hizo silaha walizokwenda kupora kituoni ni za kufanyia nini kama sio kuua raia wasiokuwa na hatia
 
na vp aliyeuwawa jana kama alikuwa nduguyo mtu ni mtu awe askari au mpiga debe kila mmoja ana dhaman kwenye familia yake na taifa pia
 
Chukulia aliyeuawa pale stakishari angekuwa ndugu yako jee ungekuwa na huruma na mtu aliyeua nduguyooo?? twende mbele na kurudi nyuma je hizo silaha walizokwenda kupora kituoni ni za kufanyia nini kama sio kuua raia wasiokuwa na hatia
Nakubaliana na wewe na ndio maana huwezi kusikiliza kesi inayokuhusu. Hutakuwa neutral. Ndio maana kesi hiyo anapewa mtu mwingine! Hivyo hivyo, polisi wasifanye hivyo, hawajafundishwa hivyo. Tukiruhusu hivyo, watatuua wengi kwa dhana tu!
 
Inaonekana unaamini kuwa hao jamaa ni majambazi. Sasa kama unaamini kuwa jambazi anayeweza kuvamia kituo cha polisi na kuua kila aliyemkuta anaweza kukamatwa kama kuku wa broiler bandani ni kuwa a bit naive.

ndiyo mwenye mamlaka ya kusema hivo ni mahakama tu
 
Tukiendekeza sana faya maswala ya human right jeshi lap polisi litakiwa like a toothless dog,,,
 
polisi hana mamlaka hiyo mkuu hii ni ichi yenye kutii sheria na taratibu sasa kama tutauana kiivo sijui


Umekosea mkuu ... hii si NCHI yenye KUTII sheria na taratibu ... hii ni nchi tu!
 
Wewe uliyezusha huu mjadala nawewe unapaswa upigwe risasi ufie mbele ya safari ,,,,,hauna uzalendo na nchi yako kabisa,,,hawa watu wakipelekwa mahakamani pengine wanaweza kutoka then wewe unategemea nini.usizungumze kabisa kama huelewi

sasa mm na ww nani haelewi ww huiamini mahakama ila unaiamini polisi
 
mtoa post uwezo wako kifikra ni mdogo sana nakufananisha na mtoto mdogo hivyo waache watu wakubwa wanaojielewa.

soma sheria mbalimbali ukatafute ushauri wa kisheria utaelimishwa.

ukumbuke kuwa ni katika kurushiana risasi, mara zote askari kwenye op.wamejihami wakiwa na mavazi maalum hivyo si rahisi wao kujeruhiwa.

acha bwebwe afu futa kauli polisi kazi yake ni kulinda raia na mali zake sio kuua na kupora
 
Ulikuepo eneo la tukio wakati wananyoosha mikono? ficha upumbavu wako, matumizi ya silaha unayajua? ni muda gani Police anatakiwa kutumia nguvu ya ziada na kawaida, ukijibu hili ntajua akili zako Zipo sawa.

mbona unakwenda mbali sana ndugu mara ulikuwepo jenga hoja basi
 
sasa mm na ww nani haelewi ww huiamini mahakama ila unaiamini polisi

Mahakamani kuna armoury??!!! Kuna mtu anajifunza target kule??!! Kuna mtu wa muzzle velocity??!!
Unajua bullet proof vest ina uzito na joto kiasi gani??!!! Wanaume wanashinda nazo hizo miilini nyie mmevaa body tights mnaenjoy tu. . . . .

Jambazi wa silaha yake chuma tu. . . . Haina mjadala
 
Mahakamani kuna armoury??!!! Kuna mtu anajifunza target kule??!! Kuna mtu wa muzzle velocity??!!
Unajua bullet proof vest ina uzito na joto kiasi gani??!!! Wanaume wanashinda nazo hizo miilini nyie mmevaa body tights mnaenjoy tu. . . . .

Jambazi wa silaha yake chuma tu. . . . Haina mjadala

kila idara iachiwe kazi yake ifanye hapo tutafika lkn kwa.mwendo huu hakuna kitu
 
Naona tangu jana hakuna hata anayelaani mauaji ya walioitwa majambazi jana si raia wala si media wala si viongozi wa kisiasa na dini.

Polisi hana mamlaka wala reseni ya kutoa uhai wa mtu.

Pia tuseme tu kuwa inaonekana walifanya makusudi kulipiza kisasi na visasi haviishi.

inategemea na mazingira. kuna mazingira anaruhusiwa kukutoa uhai na atapongezwa!!!!
 
Back
Top Bottom