- Source #1
- View Source #1
Wakuu
Nimekutana na hii taarifa huko X ikiambatana na huu ujumbe:
Kumbe maria alikua akiwauza dada zetu huko ughaibuni Ushahidi mzito umeibuka ukionyesha uhusika wa Maria Sarungi katika mafaili yanayohusishwa na kesi ya Jeffrey Epstein. Taarifa zinadai barua pepe kwa Epstein zilihusisha Miss Universe Tanzania katika biashara haramu.
Nimekutana na hii taarifa huko X ikiambatana na huu ujumbe:
Kumbe maria alikua akiwauza dada zetu huko ughaibuni Ushahidi mzito umeibuka ukionyesha uhusika wa Maria Sarungi katika mafaili yanayohusishwa na kesi ya Jeffrey Epstein. Taarifa zinadai barua pepe kwa Epstein zilihusisha Miss Universe Tanzania katika biashara haramu.
- Tunachokijua
- Jeffrey Epstein ni raia wa Marekani ambaye anahusishwa na kuwanyanyasa watoto kingongo, ubakaji, na kufanya biashara ya kuuza binadamu ambaye alijulikana pia kutokana na umaarufu wake pamoja ni utajri aliokuwa nao, alifariki Agosti 10, 2019.
Hivi karibuni kumekuwa na nyaraka, picha na video mbalimbali ambazo zinamuonesha Epstein akifanya vitendo hivyo huku akiwa pia na viongozi na watu wengine wengi mashuhuri duniani katika nyakati tofauti tofuti.
Madai
Mdau amehitaji kupata uhalisia wa picha iliyochapishwa Kupitia mtandao wa X ikimuonesha Maria Sarungi akiwa na Epstein pamoja na watu wengine. Picha hiyo imembatanishwa na ujumbe pia unaoeleza kuwa mwanaharakati huyo, anahusika pia katika yaliyotajwa kumuhusu Epstein.
Uhalisa wa Madai hayo
Ufuatiliaji wa JamiiCheck umejirirdhisha kuwa picha hiyo imehaririwa kwa teknolojia ya Akili Unde kutoka katika picha ya awali ambayo pia ilitengenezwa kwa akili Unde.
Kwa kutumia nyenzo za kidigitali ikiwemo google reverse image search imebaini kuwa picha hiyo imehaririwa kutoka katika picha ya awali iliyotengenezwa kwa Akili Unde na kumuondoa mtu mmoja ambaye nafasi yake amewekwa Maria Sarungi.
Picha ya awali iliyotengenezwa kwa AKili UndeKatika picha ya awali inamuonesha Diddy, Bill Gates, Jay-Z, Hillary na Bill Clinton, Stephen Hawking pamoja na Epstein mwenyewe, ambapo baada ya ufuatiliaji picha hiyo imeonesha kuwa imetengenezwa kwa AI.