Je ninahitaji kuwalipa maafisa Mifugo wa vijiji\kata

Tougher

JF-Expert Member
Jul 9, 2013
245
65
Wakuu naomba kujua kuhusu utaratibu wa kuwatumia maafisa Mifugo wa serikali. Je wakija kunitibia Mifugo yangu natakiwa kuwalipabei gani?
 
Kama hilo eneo unaloishi ni eneo lake la Kazi basi hutomlipa zaid ya kununua dawa.
Ila ni vizuri ukamotivate kidogo ili akuhudumie vizuri zaid
 
Kimsingi ni kazi yake kama upo kwenye kata yake, lakini hauzuiliwi kumpa "maji ya baridi" kwa ajili ya afya ya Koo lake wakati wa juakali.
 
Kama hilo eneo unaloishi ni eneo lake la Kazi basi hutomlipa zaid ya kununua dawa.
Ila ni vizuri ukamotivate kidogo ili akuhudumie vizuri zaid

Asante mkuu kwa ufafanuzi, nipo kwenye eneo lao la kazi ila kwenye hilo la maji ndio hasa limekuwa issue. wanadai hela ndefu hadi naona kama maradi hautakuwa na faida 200k kwa kila ninapowaita. sasa nikichanganya na gharama ya dawa naona kichwa kinapata moto
 
Kama hilo eneo unaloishi ni eneo lake la Kazi basi hutomlipa zaid ya kununua dawa.
Ila ni vizuri ukamotivate kidogo ili akuhudumie vizuri zaid
Sio kweli. Maafisa mifugo wameajiriwa kutoa ushauri na sio kutibu. Kwa hiyo bwana mifugo anapaswa amuandikie dawa mfugaji anunue na amwambie atafute mtaalam yeyote wa mifugo amtibie. Kama atatibu yeye sawa lakini kazi ya kutibu ni ya kibinafsi( private) haihusiani na ajira. Kwa hiyo akitibu anapaswa kulipwa hiyo sio fadhila. Tambua kuwa wanatibu wataalam mbalimbali hata wasio katika ajira ya serikali kwani wao hawapaswi kulipwa? Kwa hiyo akitibu yeye au akatafuta mtaalam mwingine wa kutibu katimiza wajibu wake.
Sawa na mtaalam wa kilimo. Sio kazi yake kubeba bomba la kunyunyizia dawa na kunyunyizia mazao ya mkulima. Yeye anapaswa kumuonyesha kwa vitendo jinsi ya kunyunyizia kisha amuachie aendelee mwenyewe. Hata wafugaji wapo waliofundishwa kuchoma sindano , kuhasi, nk. Hiyo ndio kazi rasmi ya bwana mifugo.
 
Sio kweli. Maafisa mifugo wameajiriwa kutoa ushauri na sio kutibu. Kwa hiyo bwana mifugo anapaswa amuandikie dawa mfugaji anunue na amwambie atafute mtaalam yeyote wa mifugo amtibie. Kama atatibu yeye sawa lakini kazi ya kutibu ni ya kibinafsi( private) haihusiani na ajira. Kwa hiyo akitibu anapaswa kulipwa hiyo sio fadhila. Tambua kuwa wanatibu wataalam mbalimbali hata wasio katika ajira ya serikali kwani wao hawapaswi kulipwa? Kwa hiyo akitibu yeye au akatafuta mtaalam mwingine wa kutibu katimiza wajibu wake.
Sawa na mtaalam wa kilimo. Sio kazi yake kubeba bomba la kunyunyizia dawa na kunyunyizia mazao ya mkulima. Yeye anapaswa kumuonyesha kwa vitendo jinsi ya kunyunyizia kisha amuachie aendelee mwenyewe. Hata wafugaji wapo waliofundishwa kuchoma sindano , kuhasi, nk. Hiyo ndio kazi rasmi ya bwana mifugo.
Kwa kuongezea matibabu sio dawa tu. Kuna vifaa kama syringe, thermometer, pamba, gloves, stethoscope, mikasi, visu vya kupasulia, dawa za kuosha vidonda, nk. Serikali haimpi chochote kati ya hivyo ananunua kwa mshahara wake. Halafu aje kutibu unasema utamlipa kwa fadhila tu? Hizo gharama za vifaa vya tiba atamrudishia nani?
 
Kwa kuongezea matibabu sio dawa tu. Kuna vifaa kama syringe, thermometer, pamba, gloves, stethoscope, mikasi, visu vya kupasulia, dawa za kuosha vidonda, nk. Serikali haimpi chochote kati ya hivyo ananunua kwa mshahara wake. Halafu aje kutibu unasema utamlipa kwa fadhila tu? Hizo gharama za vifaa vya tiba atamrudishia nani?
Mkuu Coral angalia kwenye post yangu pale juu, Gharama zote hizo unazozisema ninagharamia mimi. Kuanzia dawa hadi hizo syringes na gloves, wao ni kuja shambani na kutoa ushauri/utabibu kwa gharama ya shilingi laki 2 (200,000/-) kila wanapokuja. hiyo ndio hoja yangu na swali langu je kiwango hiki cha malipo ni cha kawaida kwa watu wote? au wamenifuma mimi tu?
 
Mkuu Unadai Jamaa Wakija Lazima Wachukue Laki Mbili Kila Baada Ya Mda Gani ... Je, Idadi Ya Mifugo Uliyonayo Ni Kiasi Gani ... Je, Shughuli Zako Za Ufugaji Unafanyia Maeneo Gani ...
 
Mkuu Coral angalia kwenye post yangu pale juu, Gharama zote hizo unazozisema ninagharamia mimi. Kuanzia dawa hadi hizo syringes na gloves, wao ni kuja shambani na kutoa ushauri/utabibu kwa gharama ya shilingi laki 2 (200,000/-) kila wanapokuja. hiyo ndio hoja yangu na swali langu je kiwango hiki cha malipo ni cha kawaida kwa watu wote? au wamenifuma mimi tu?
Wanakuibia kama ni hivyo. Siwezi kuelewa mfugaji uwe na vifaa tiba vya nini? Mfano forceps, stethoscope, mfugaji atafanyia nini? Lazima akasome huo utaalam.
Kimsingi Tougher nilikuwa na respond kwenye majibu mepesi waliyotoa hao wengine
 
sasa nini kazi ya hawa watu kama ni hvyo hakuna mkataba mbovu walouingia serikali na waajiriwa wa kada hyo yani ana uwezo wakutibu kwasababu tuu iko nje na mkataba wa ajira atashauri tu napinga kitu kama hichi
 
for life suala hapa sio bwana mifugo kutibu au kutokutibu suala ni je walipwe wanapotibu au wasilipwe?. Kutibu ni kazi yao lakini haipo kwenye "job discription".
Ili uelewe tutoe mfano wa wafanyakazi wa TANESCO. Kazi ya shirika ni kusambaza umeme na kuunganisha hadi kwenye mita . Kusuka nyumba sio kazi ya shirika. Unaweza kutumia fundi yeyote mwenye sifa akusukie nyumba. Anaweza kuwa mwajiriwa wa tanesco au sio. Vyovyote iwavyo lazima umlipe hata kama ni fundi wa tanesco kwa sababu kazi ya kisuka ni private sio ya shirika.
Ndivyo ilivyo na kazi ya kutibu mifugo ni private.
 
Kwanza hao maafisa mifugo kazi yao ni kutoa ushauri pamoja na kutibu sasa kwa kuwa wanatoa huduma kwa wafugaji wa kata/kijiji kizima inakuwa kazi ngumu kuhudumia wafugaaji(wateja) ndani ya mda wazi hivyo mara nyingine watafanya kazi nje ya mda wa kazi, pili serikali haiwapatii/haiwatimizii vitendea kazi kama usafiri(pikipiki) hata kama wakiwa nazo haitoi bageti ya mafuta hivyo linakubidi kuchangi hizo gharama.
Tatu njinsi nilivyo kuelewa wewe unafuga kwa biashara hivyo inahitaji uangarizi wa karibu na itamhitaji mtaaramu akutembelee wewe tu wakati na wafungaji wengine wanamhitaji hinyo kama ashakutembelea anaweze kukupa ushauli tu atakuwa ametelekeleza wajibu wake, hivyo unatakiwa ummotivate maana usipo fanya hivyo itakuwa kama umemuajiri wewe au atakuwa kama kibarua wako swala la kukucharge gharama za juu hilo ni swala la kuongea nao na kubargain/kuelewana tu.
 
Kama unafuga kuku wa mayai laki mbili kutoa ni alali kabisa' mfano kuchanja chanjo ya CORYZA au SALMONELLA tunafanya kuku 1 sh. 150 had 200 sasa wewe una kuku 3000 unataka ufanyiwe bure' kwanza ujasema unamifugo gani unakuja kulialia huku.
 
Kama unafuga kuku wa mayai laki mbili kutoa ni alali kabisa' mfano kuchanja chanjo ya CORYZA au SALMONELLA tunafanya kuku 1 sh. 150 had 200 sasa wewe una kuku 3000 unataka ufanyiwe bure' kwanza ujasema unamifugo gani unakuja kulialia huku.

Pole kwa jinsi unavyojichanganya ni wazi kabisa una msongo kiasi
 
Mleta mada anachanganya mambo, sawa kuna kaukweli flani lakini hujajieleza in details
 
Back
Top Bottom