Waziri wa Mifugo usipohukumiwa na Serikali utahukumiwa na Mungu

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Ni kama nchi haina Wizara ya Mifugo au inayo lakini bila Waziri na Watendaji wake.

Kuna tabia imekita mizizi na kuwa sugu ya wasafirishaji wa mifugo (kwenye malori) kwenda machinjioni kutesa wanyama hao kwa viwango vilivyopitiliza na hakuna anayediriki kupaza sauti kupinga ukatili huu unaowafanya binadamu wanaowasafirisha kuwa ni wanyama zaidi na halisi kuliko mifugo hiyo.

Wavuta bangi ya Arumeru hawa wamekuwa wakipiga ng'ombe hawa kwa kutaka sifa kwenye kadamnasi. Wanapopita karibu nami huwa nafunga macho au nakimbia uchochoroni nisishuhudie mateso hayo.

Ile kwamba ng'ombe hao wanaenda kuchinjwa haiwaondolei haki ya kufikishwa sokoni wakiwa katika hali salama kama bidhaa zingine.

Wasukuma hawa, Wagogo hawa na Wamang'ati hawa huwa wanapofika kwenye satellite towns (na mijini huko wapitako) kama Mbezi Msigani, Marambamawili, Kifuru, Kinyerezi, Segerea huwapiga ng'ombe hao kipigo cha Pakamwizi kwa sifa ili waonekane kwa watu waliojaa senta hizo huku wahuni wakiwashangilia kwa nderemo na vifijo utadhani timu fulani imefunga magoli 5.

Ng'ombe wameshonwa kwenye lori bila mpangilio bila nafasi huku wengine wakichomwa na kutobolewa kwa mapembe yale ya Ankole na wengine wakinyea midomo ya wenzao, shingo za ng'ombe zimekunjana hawawezi kuzinyoosha, jua kali la utosini (huenda wana kiu) turubai likiwa limekaliwa na wavuta bangi hawa bila kulifungua kuwakingia jua ili ng'ombe hawa wasiendelee kuwa de-hydrated (kupoteza maji mwilini).

Binadamu tu akiwashwa bila kujikuna anaweza kupiga mayowe (ukunga), vidole vya ng'ombe kujikunia ni mkia wake, sasa anajikunaje kwenye hali ile? Kwa siku nzima ng'ombe hujikuna kwa mkia wake zaidi ya mara 500.

Akisafirishwa kwa siku 2 bila uhuru au ruhusa ya kutumia mkia wake ni mateso kama mateso mengine na ni sawa na kumzuia binadamu kujikuna ukurutu wake unaomuwasha sana.

Wanasafirishwa masafa marefu bila majani kiasi kwamba hata ubora wa nyama yenyewe unapotea, hata uzito wao unapunguzwa na ukatili huu.

Kwa kuwa na mzigo moyoni na jambo hili mara mbili kwa nyakati tofauti niliamua kwenda kuweka ambush Mbezi Msigani (njia wanayoipenda kufika Vingunguti) nikiwa na pikipiki nyuma yao hadi Vingunguti nikabaini kwamba wala ngada hawa huwa wanapanda mori na midadi ya kuwafanyia viumbe hawa ukatili uliopindukia pale wanapofika kwenye maeneo ya senta yenye watu wengi kama nilivyozitaja hapo na maeneo wanayokumbana na foleni.

Waziri wa Mifugo ajuwe kwamba usafirishaji mifugo kwa kutumia malori ni utaratibu ambao dunia imeisha achana nao miongo mingi tu ili kulinda ubora wa mazao ya mifugo hiyo kama nyama, kwato, pembe na ngozi lakini pia kukinga viumbe hawa na mateso wasiyostahili lakini pia kuokoa barabara zetu na shinikizo la shehena kubwa ya mifugo hii zikiwemo bidhaa zingine.

Matrafiki wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maaskari wa doria wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maafisa Mifugo wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Waziri na watendaji wake wanayajuwa haya hawakemei, wakati fulani Waziri na watendaji wao wanapishana na malori hayo ya mifugo njiani watokapo au waendapo Dodoma na kuwapigia king'ora tu kuwapa ishara kwamba wawapishe wanawahi.

Kwa staili hii mbovu na kwa sifa kwamba Tz ni ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika nyuma ya Ethiopia na ikifuatiwa namba 3 na Cameroon tutaweza kuishi kwenye dunia hii ya ushindani wa ubora wa bidhaa na huduma?

Kutoa tu tamko la kukemea ukatili huu inahitaji kusomea digrii na kuomba bajeti ya posho ya kukemea?

Enzi za Mwl. Nyerere ambapo nchi haikuwa na barabara nzuri mifugo ilisafirishwa kwa garimoshi kwenye mabehewa maalum yenye majani na maji ya kunywa ambapo hawawakiwi jua wala kupigwa mvua ya mawe toka Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kaskazini hadi Dar.

Ni kipindi hicho mazao ya mifugo toka Tz yalitamalaki masoko ya ng'ambo ya bahari kutokana na ubora wake.

Sasa barabara zimekuwa nzuri ili mateso na ukatili vishamiri kwa mifugo?.

Mifugo hii ndiyo inamhudumia kila mtu katika nchi hii anayefuga na asiyefuga. 90% ya kilimo nchini Tz kinalimwa na ng'ombe kwa kuwa wakulima wengi hawewezi kumudu bei kubwa ya matrekta.

Hivyo kwenye kapu la chakula (food basket) nchi hii ng'ombe wanachangia kwa 90% kuliko binadamu wanaolima kwa mikono na kuliko matrekta ambayo ni machache kutokana na bei zake kuwa ghali.

Asilimia kubwa ya maboresho ya afya zetu zinategemea mifugo hii je, tunaweza kuwa na afya bila nyama, maziwa na bila damu za mifugo?

Je, jamii za wafugaji kama Maasai na Datooga (wasiokula nafaka na mazao ya mimea) zinaweza kuwepo kwenye sayari bila mifugo?

Kiwango cha ukatili huu unanifanya wakati fulani kudhani kwamba serikali ipige marufuku kusafirisha mifugo kwa malori ili TRC irejee kwenye biashara hiyo ili pia ijipatie mapato humo lakini pia tupate mazao bora yatokanayo na mifugo hiyo ambayo tunaweza kuuza hata kwenye masoko ya ng'ambo ya bahari.

Sheria kama zipo kudhibiti hali hii na hazifanyi kazi kuna haja gani kuwa nazo?

Nchini Kenya hapo Punda anakatiwa leseni kama gari (anachukuliwa kama chombo cha usafirishaji), leseni ina masharti yake ikiwemo kutobeba shehena (mzigo) uliozidi uwezo wake.

Askari akikuta Punda anafanyiwa ukatili anakuchukulia hatua kali za kisheria. Kwenda kujifunza hapo Kenya tunahitaji mabilioni mangapi ya pesa?

Ujumbe huu ukifikia mamlaka za uteuzi wa watendaji hao naomba uwajibikaji uwepo hima.
 
Huu ndo uungwana siyo kila siku kujadili wafanya siasa uchwara.
Profesa Wangari Maathai alimuadabisha rais Moi kwa kuvuna mimea ya mlima Kenya.

Kwake alikuwa hatumii mkaa kwa kuwa hiyo ingehitaji miti kufa kwanza ili mkaa upatikane.

Aliwahi kucharaza mamamboga mtaani kwa kuwa wanasababisha jangwa kama alivyoamini.

Aliamuru atapokufa (ameishakufa) mwili wake uchomwe ili kusalimisha miti ya mbao ya kutengeneza jeneza lake.

Maseremala waliwahi kumfungulia kesi akawashinda.

Sasa ng'ombe hawa wanaoteswa na wavuta bangi hawa si ni zaidi ya mimea aliyotetea Prof. Wangari Maathai?

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Nakubaliana na wewe, hii wizara ni kama haipo na kila kitu kinaenda kienyeji tuu. Juzi nimeshangaa kuona kwenye mitandao chama cha wafugaji Tanzania wakiendesha zoezi la kuhesabu mifugo, jambo ambalo lilitakiwa lifanywe kitaalam na wizara.

Kingine ukiangalia sekta kama misitu huko vijijini mipango ya matumizi bora ya ardhi za vijiji inapokamilika unakuta wanaenda vijijini kuwezesha vijiji kutenga misitu yake na kuwaelimisha namna ya kuisimamia.

Hawa wizara ya mifugo badala na wao waende kusaidia vijiji kuendeleza maeneo yaliyotengwa kama malisho, wao hawana habari, matokeo yake malisho yanavamiwa kwa matumizi mengine.

Haya njoo kwenye kusaidia kujenga malambo ya maji na huduma za ugani, kiukweli sijui wanafanya nini.
 
Hoja yako ina mashiko sana, lakini ungeweza kusema kwamba, kuwe na vituo viwili au vitatu vya kuwashusha hao ng'ombe kwaajili ya maji na nyasi au kuwe na malori special kwaajili ya kiwasafirisha hao mifugo yenye maji na nyasi kwa wakati wote wa safari

Lakini mimi naona kuliko kusomba mangombe mazima kwanini wasichinjwe wanakotoka dar iende nyama tuu
 
Hoja yako ina mashiko sana, lakini ungeweza kusema kwamba, kuwe na vituo viwili au vitatu vya kuwashusha hao ng'ombe kwaajili ya maji na nyasi au kuwe na malori special kwaajili ya kiwasafirisha hao mifugo yenye maji na nyasi kwa wakati wote wa safari

Lakini mimi naona kuliko kusomba mangombe mazima kwanini wasichinjwe wanakotoka dar iende nyama tuu
Mkuu chukuwa taji yako . Umewaza kimkakati na kwa tija. Hakuna haja ya kujenga viwanda vya kuchinjia mifugo Dar na Kibaha, vingejengwa kule kule maeneo ya wafugaji.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Nakubaliana na wewe, hii wizara ni kama haipo na kila kitu kinaenda kienyeji tuu. Juzi nimeshangaa kuona kwenye mitandao chama cha wafugaji Tanzania wakiendesha zoezi la kuhesabu mifugo, jambo ambalo lilitakiwa lifanywe kitaalam na wizara.

Kingine ukiangalia sekta kama misitu huko vijijini mipango ya matumizi bora ya ardhi za vijiji inapokamilika unakuta wanaenda vijijini kuwezesha vijiji kutenga misitu yake na kuwaelimisha namna ya kuisimamia.

Hawa wizara ya mifugo badala na wao waende kusaidia vijiji kuendeleza maeneo yaliyotengwa kama malisho, wao hawana habari, matokeo yake malisho yanavamiwa kwa matumizi mengine.

Haya njoo kwenye kusaidia kujenga malambo ya maji na huduma za ugani, kiukweli sijui wanafanya nini.
SSH anamteua Abdallah Ulega ambaye asili yake hakuna mifugo. Mboga kuu iliyomkuza ni kisamvu.

Magufuli hakuwa mjinga kumteua Luhaga Joelsen Mpina Waziri wa Mifugo ambaye anatoka kwenye asili ya ufugaji.

Abdallah Ulega amekaa Wizara ya Mifugo kama Naibu Waziri na sasa Waziri kamili lakini inadhihiri hajajifunza kuhusu ufugaji na labda haki za wanyama, vinginevyo anafanya kazi kimazoea.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Sijui ni bangi nazomoka ila naamini ipo siku wanyama wata revenge Kwa tuliyo watendea,maybe am paranoid ila sijawahi piga hata kuku tangu nisome "Fikiri na jogoo"
 
Mbaya zaidi ikitokea Ng'ombe akifa yule mtu aliye paswa kuangalia Ng'ombe apewi ata mia maana kafanya uzembe lakini kumbuka dereva anasema kwamba gari yangu inabeba Ng'ombe 30 kumbe inabeba Ng'ombe 25 tuu ivyo vifo lazima vitokee au Ng'ombe kuumia
Ng'ombe akifa kwenye gari anashushwa Kisha inatafutwa center ya karibu Kisha anachinjwa nyama inaingia buchani usiku ivyo ukiamka asubuhi nyama ipo inakusubili ivyo wale Ndugu zetu katika Imani tunakuwa tumedhulumiwa Imani zetu
Nini kifanyike ili Ng'ombe waondokane na hii kadhia
✓Kuwe na vituo vya kumpumzikia Ng'ombe angalau kimoja kwa Kila mkoa
✓Ng'ombe wapakiwe kwa idadi sahihi kutokana na ukubwa wa gari na maumbile ya Ng'ombe
✓ kuwe na maranda ya mbao au pumba za mpunga kwenye sakafu ya gari ili kuzuia Ng'ombe kuteleza
✓ kijana anaye angalia Ng'ombe asitumie nguvu sana kuliko akili najua anachoka maana yeye inabid aning'inie kwenye machuma ya gari mwanzo wa safari hadi mwisho
 
Mbaya zaidi ikitokea Ng'ombe akifa yule mtu aliye paswa kuangalia Ng'ombe apewi ata mia maana kafanya uzembe lakini kumbuka dereva anasema kwamba gari yangu inabeba Ng'ombe 30 kumbe inabeba Ng'ombe 25 tuu ivyo vifo lazima vitokee au Ng'ombe kuumia
Ng'ombe akifa kwenye gari anashushwa Kisha inatafutwa center ya karibu Kisha anachinjwa nyama inaingia buchani usiku ivyo ukiamka asubuhi nyama ipo inakusubili ivyo wale Ndugu zetu katika Imani tunakuwa tumedhulumiwa Imani zetu
Nini kifanyike ili Ng'ombe waondokane na hii kadhia
✓Kuwe na vituo vya kumpumzikia Ng'ombe angalau kimoja kwa Kila mkoa
✓Ng'ombe wapakiwe kwa idadi sahihi kutokana na ukubwa wa gari na maumbile ya Ng'ombe
✓ kuwe na maranda ya mbao au pumba za mpunga kwenye sakafu ya gari ili kuzuia Ng'ombe kuteleza
✓ kijana anaye angalia Ng'ombe asitumie nguvu sana kuliko akili najua anachoka maana yeye inabid aning'inie kwenye machuma ya gari mwanzo wa safari hadi mwisho
Duh! Mkuu wewe ni mtaalam aisee. Nimekukubali 100%

Haya mawazo yako lazima wizara iyachukuwe kama siyo yote.

Waislamu waandamane kupinga usafirishaji huu wa mifugo ili wasilishwe vibudu vinavyokufa njiani kwa vipigo vya ukatili.

Nadhani BAKWATA itoe tamko na kwenye tamko impe Waziri ultimatum.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Kinyume cha haki za wanyama....
Mifugo hii ndiyo inamhudumia kila mtu katika nchi hii anayefuga na asiyefuga. 90% ya kilimo nchini Tz kinalimwa na ng'ombe kwa kuwa wakulima wengi hawewezi kumudu bei kubwa ya matrekta.

Hivyo kwenye kapu la chakula (food basket) nchi hii ng'ombe wanachangia kwa 90% kuliko binadamu wanaolima kwa mikono na kuliko matrekta ambayo ni machache kutokana na bei zake kuwa ghali.

Asilimia kubwa ya maboresho ya afya zetu zinategemea mifugo hii je, tunaweza kuwa na afya bila nyama, maziwa na bila damu za mifugo?

Je, jamii za wafugaji kama Maasai na Datooga (wasiokula nafaka na mazao ya mimea) zinaweza kuwepo kwenye sayari bila mifugo?

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Mifugo hii ndiyo inamhudumia kila mtu katika nchi hii anayefuga na asiyefuga. 90% ya kilimo nchini Tz kinalimwa na ng'ombe kwa kuwa wakulima wengi hawewezi kumudu bei kubwa ya matrekta.

Hivyo kwenye kapu la chakula (food basket) nchi hii ng'ombe wanachangia kwa 90% kuliko binadamu wanaolima kwa mikono na kuliko matrekta ambayo ni machache kutokana na bei zake kuwa ghali.

Asilimia kubwa ya maboresho ya afya zetu zinategemea mifugo hii je, tunaweza kuwa na afya bila nyama, maziwa na bila damu za mifugo?

Je, jamii za wafugaji kama Maasai na Datooga (wasiokula nafaka na mazao ya mimea) zinaweza kuwepo kwenye sayari bila mifugo?

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Nimeelewa hoja zako
 
Magari ya kubeba ng'ombe yapo ila kodi yake ndio maana huu mfumo upo hivyo matatizo mengi tuliyonayo chanzo chake ni kodi kubwa kwenye magari inapelekea bidhaa na mifugo kusafirishwa bila ustaarabu hata hizo bus kwa baadhi ya maeneo ukiziangalia ni balaa abiria walifika salama kwanza wanaanza kufuta vumbi kwenye nguo zao na mabegi...
 
Ni kama nchi haina Wizara ya Mifugo au inayo lakini bila Waziri na Watendaji wake.

Kuna tabia imekita mizizi na kuwa sugu ya wasafirishaji wa mifugo (kwenye malori) kwenda machinjioni kutesa wanyama hao kwa viwango vilivyopitiliza na hakuna anayediriki kupaza sauti kupinga ukatili huu unaowafanya binadamu wanaowasafirisha kuwa ni wanyama zaidi na halisi kuliko mifugo hiyo.

Wavuta bangi ya Arumeru hawa wamekuwa wakipiga ng'ombe hawa kwa kutaka sifa kwenye kadamnasi. Wanapopita karibu nami huwa nafunga macho au nakimbia uchochoroni nisishuhudie mateso hayo.

Ile kwamba ng'ombe hao wanaenda kuchinjwa haiwaondolei haki ya kufikishwa sokoni wakiwa katika hali salama kama bidhaa zingine.

Wasukuma hawa, Wagogo hawa na Wamang'ati hawa huwa wanapofika kwenye satellite towns (na mijini huko wapitako) kama Mbezi Msigani, Marambamawili, Kifuru, Kinyerezi, Segerea huwapiga ng'ombe hao kipigo cha Pakamwizi kwa sifa ili waonekane kwa watu waliojaa senta hizo huku wahuni wakiwashangilia kwa nderemo na vifijo utadhani timu fulani imefunga magoli 5.

Ng'ombe wameshonwa kwenye lori bila mpangilio bila nafasi huku wengine wakichomwa na kutobolewa kwa mapembe yale ya Ankole na wengine wakinyea midomo ya wenzao, shingo za ng'ombe zimekunjana hawawezi kuzinyoosha, jua kali la utosini (huenda wana kiu) turubai likiwa limekaliwa na wavuta bangi hawa bila kulifungua kuwakingia jua ili ng'ombe hawa wasiendelee kuwa de-hydrated (kupoteza maji mwilini).

Binadamu tu akiwashwa bila kujikuna anaweza kupiga mayowe (ukunga), vidole vya ng'ombe kujikunia ni mkia wake, sasa anajikunaje kwenye hali ile? Kwa siku nzima ng'ombe hujikuna kwa mkia wake zaidi ya mara 500.

Akisafirishwa kwa siku 2 bila uhuru au ruhusa ya kutumia mkia wake ni mateso kama mateso mengine na ni sawa na kumzuia binadamu kujikuna ukurutu wake unaomuwasha sana.

Wanasafirishwa masafa marefu bila majani kiasi kwamba hata ubora wa nyama yenyewe unapotea, hata uzito wao unapunguzwa na ukatili huu.

Kwa kuwa na mzigo moyoni na jambo hili mara mbili kwa nyakati tofauti niliamua kwenda kuweka ambush Mbezi Msigani (njia wanayoipenda kufika Vingunguti) nikiwa na pikipiki nyuma yao hadi Vingunguti nikabaini kwamba wala ngada hawa huwa wanapanda mori na midadi ya kuwafanyia viumbe hawa ukatili uliopindukia pale wanapofika kwenye maeneo ya senta yenye watu wengi kama nilivyozitaja hapo na maeneo wanayokumbana na foleni.

Waziri wa Mifugo ajuwe kwamba usafirishaji mifugo kwa kutumia malori ni utaratibu ambao dunia imeisha achana nao miongo mingi tu ili kulinda ubora wa mazao ya mifugo hiyo kama nyama, kwato, pembe na ngozi lakini pia kukinga viumbe hawa na mateso wasiyostahili lakini pia kuokoa barabara zetu na shinikizo la shehena kubwa ya mifugo hii zikiwemo bidhaa zingine.

Matrafiki wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maaskari wa doria wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maafisa Mifugo wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Waziri na watendaji wake wanayajuwa haya hawakemei, wakati fulani Waziri na watendaji wao wanapishana na malori hayo ya mifugo njiani watokapo au waendapo Dodoma na kuwapigia king'ora tu kuwapa ishara kwamba wawapishe wanawahi.

Kwa staili hii mbovu na kwa sifa kwamba Tz ni ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika nyuma ya Ethiopia na ikifuatiwa namba 3 na Cameroon tutaweza kuishi kwenye dunia hii ya ushindani wa ubora wa bidhaa na huduma?

Kutoa tu tamko la kukemea ukatili huu inahitaji kusomea digrii na kuomba bajeti ya posho ya kukemea?

Enzi za Mwl. Nyerere ambapo nchi haikuwa na barabara nzuri mifugo ilisafirishwa kwa garimoshi kwenye mabehewa maalum yenye majani na maji ya kunywa ambapo hawawakiwi jua wala kupigwa mvua ya mawe toka Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kaskazini hadi Dar.

Ni kipindi hicho mazao ya mifugo toka Tz yalitamalaki masoko ya ng'ambo ya bahari kutokana na ubora wake.

Sasa barabara zimekuwa nzuri ili mateso na ukatili vishamiri kwa mifugo?.

Mifugo hii ndiyo inamhudumia kila mtu katika nchi hii anayefuga na asiyefuga. 90% ya kilimo nchini Tz kinalimwa na ng'ombe kwa kuwa wakulima wengi hawewezi kumudu bei kubwa ya matrekta.

Hivyo kwenye kapu la chakula (food basket) nchi hii ng'ombe wanachangia kwa 90% kuliko binadamu wanaolima kwa mikono na kuliko matrekta ambayo ni machache kutokana na bei zake kuwa ghali.

Asilimia kubwa ya maboresho ya afya zetu zinategemea mifugo hii je, tunaweza kuwa na afya bila nyama, maziwa na bila damu za mifugo?

Je, jamii za wafugaji kama Maasai na Datooga (wasiokula nafaka na mazao ya mimea) zinaweza kuwepo kwenye sayari bila mifugo?

Kiwango cha ukatili huu unanifanya wakati fulani kudhani kwamba serikali ipige marufuku kusafirisha mifugo kwa malori ili TRC irejee kwenye biashara hiyo ili pia ijipatie mapato humo lakini pia tupate mazao bora yatokanayo na mifugo hiyo ambayo tunaweza kuuza hata kwenye masoko ya ng'ambo ya bahari.

Sheria kama zipo kudhibiti hali hii na hazifanyi kazi kuna haja gani kuwa nazo?

Ujumbe huu ukifikia mamlaka za uteuzi wa watendaji hao naomba uwajibikaji uwepo hima.
Asante bro wewe ndio Mimi. Niliwah kumkata jamaa mmoja mtama katikat ya mji kisa alimpiga mbwa kwa jiwe. Naumia sana mtu akimtesa mnyama aisee
 
Unafkiii acha kunywa supu ya utumbo

Mambo ya wazungu ayo afrika hatutaweza kamwe haki za binadam afrika bado kizungukuti itakuaje za wanyama.......
 
Ni kama nchi haina Wizara ya Mifugo au inayo lakini bila Waziri na Watendaji wake.

Kuna tabia imekita mizizi na kuwa sugu ya wasafirishaji wa mifugo (kwenye malori) kwenda machinjioni kutesa wanyama hao kwa viwango vilivyopitiliza na hakuna anayediriki kupaza sauti kupinga ukatili huu unaowafanya binadamu wanaowasafirisha kuwa ni wanyama zaidi na halisi kuliko mifugo hiyo.

Wavuta bangi ya Arumeru hawa wamekuwa wakipiga ng'ombe hawa kwa kutaka sifa kwenye kadamnasi. Wanapopita karibu nami huwa nafunga macho au nakimbia uchochoroni nisishuhudie mateso hayo.

Ile kwamba ng'ombe hao wanaenda kuchinjwa haiwaondolei haki ya kufikishwa sokoni wakiwa katika hali salama kama bidhaa zingine.

Wasukuma hawa, Wagogo hawa na Wamang'ati hawa huwa wanapofika kwenye satellite towns (na mijini huko wapitako) kama Mbezi Msigani, Marambamawili, Kifuru, Kinyerezi, Segerea huwapiga ng'ombe hao kipigo cha Pakamwizi kwa sifa ili waonekane kwa watu waliojaa senta hizo huku wahuni wakiwashangilia kwa nderemo na vifijo utadhani timu fulani imefunga magoli 5.

Ng'ombe wameshonwa kwenye lori bila mpangilio bila nafasi huku wengine wakichomwa na kutobolewa kwa mapembe yale ya Ankole na wengine wakinyea midomo ya wenzao, shingo za ng'ombe zimekunjana hawawezi kuzinyoosha, jua kali la utosini (huenda wana kiu) turubai likiwa limekaliwa na wavuta bangi hawa bila kulifungua kuwakingia jua ili ng'ombe hawa wasiendelee kuwa de-hydrated (kupoteza maji mwilini).

Binadamu tu akiwashwa bila kujikuna anaweza kupiga mayowe (ukunga), vidole vya ng'ombe kujikunia ni mkia wake, sasa anajikunaje kwenye hali ile? Kwa siku nzima ng'ombe hujikuna kwa mkia wake zaidi ya mara 500.

Akisafirishwa kwa siku 2 bila uhuru au ruhusa ya kutumia mkia wake ni mateso kama mateso mengine na ni sawa na kumzuia binadamu kujikuna ukurutu wake unaomuwasha sana.

Wanasafirishwa masafa marefu bila majani kiasi kwamba hata ubora wa nyama yenyewe unapotea, hata uzito wao unapunguzwa na ukatili huu.

Kwa kuwa na mzigo moyoni na jambo hili mara mbili kwa nyakati tofauti niliamua kwenda kuweka ambush Mbezi Msigani (njia wanayoipenda kufika Vingunguti) nikiwa na pikipiki nyuma yao hadi Vingunguti nikabaini kwamba wala ngada hawa huwa wanapanda mori na midadi ya kuwafanyia viumbe hawa ukatili uliopindukia pale wanapofika kwenye maeneo ya senta yenye watu wengi kama nilivyozitaja hapo na maeneo wanayokumbana na foleni.

Waziri wa Mifugo ajuwe kwamba usafirishaji mifugo kwa kutumia malori ni utaratibu ambao dunia imeisha achana nao miongo mingi tu ili kulinda ubora wa mazao ya mifugo hiyo kama nyama, kwato, pembe na ngozi lakini pia kukinga viumbe hawa na mateso wasiyostahili lakini pia kuokoa barabara zetu na shinikizo la shehena kubwa ya mifugo hii zikiwemo bidhaa zingine.

Matrafiki wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maaskari wa doria wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Maafisa Mifugo wanashuhudia ukatili huu hawakemei. Waziri na watendaji wake wanayajuwa haya hawakemei, wakati fulani Waziri na watendaji wao wanapishana na malori hayo ya mifugo njiani watokapo au waendapo Dodoma na kuwapigia king'ora tu kuwapa ishara kwamba wawapishe wanawahi.

Kwa staili hii mbovu na kwa sifa kwamba Tz ni ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika nyuma ya Ethiopia na ikifuatiwa namba 3 na Cameroon tutaweza kuishi kwenye dunia hii ya ushindani wa ubora wa bidhaa na huduma?

Kutoa tu tamko la kukemea ukatili huu inahitaji kusomea digrii na kuomba bajeti ya posho ya kukemea?

Enzi za Mwl. Nyerere ambapo nchi haikuwa na barabara nzuri mifugo ilisafirishwa kwa garimoshi kwenye mabehewa maalum yenye majani na maji ya kunywa ambapo hawawakiwi jua wala kupigwa mvua ya mawe toka Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kaskazini hadi Dar.

Ni kipindi hicho mazao ya mifugo toka Tz yalitamalaki masoko ya ng'ambo ya bahari kutokana na ubora wake.

Sasa barabara zimekuwa nzuri ili mateso na ukatili vishamiri kwa mifugo?.

Mifugo hii ndiyo inamhudumia kila mtu katika nchi hii anayefuga na asiyefuga. 90% ya kilimo nchini Tz kinalimwa na ng'ombe kwa kuwa wakulima wengi hawewezi kumudu bei kubwa ya matrekta.

Hivyo kwenye kapu la chakula (food basket) nchi hii ng'ombe wanachangia kwa 90% kuliko binadamu wanaolima kwa mikono na kuliko matrekta ambayo ni machache kutokana na bei zake kuwa ghali.

Asilimia kubwa ya maboresho ya afya zetu zinategemea mifugo hii je, tunaweza kuwa na afya bila nyama, maziwa na bila damu za mifugo?

Je, jamii za wafugaji kama Maasai na Datooga (wasiokula nafaka na mazao ya mimea) zinaweza kuwepo kwenye sayari bila mifugo?

Kiwango cha ukatili huu unanifanya wakati fulani kudhani kwamba serikali ipige marufuku kusafirisha mifugo kwa malori ili TRC irejee kwenye biashara hiyo ili pia ijipatie mapato humo lakini pia tupate mazao bora yatokanayo na mifugo hiyo ambayo tunaweza kuuza hata kwenye masoko ya ng'ambo ya bahari.

Sheria kama zipo kudhibiti hali hii na hazifanyi kazi kuna haja gani kuwa nazo?

Ujumbe huu ukifikia mamlaka za uteuzi wa watendaji hao naomba uwajibikaji uwepo hima.
Animal rights activist 👍👍👍
 
Back
Top Bottom