Je, nimuache au nimvumilie?

Je, nimuache au nimvumilie?

Crimea Bridge

Member
Joined
Oct 8, 2022
Posts
51
Reaction score
152
Nina mke wa ndoa ambaye nina watoto naye watatu, umri wangu sasa ni miaka 32 na umri wa mke wangu ni miaka 28. Zamani nilikua na uwezo mkubwa na alinipenda sana, ila tokea pesa zimepungua ndiyo nimeona mapungufu yake. Kuna kipindi alitoroka akaniachia watoto, nikapambana kumrudisha maisha yakaendelea ila sasa hivi naona tena dharau na maneno yameanza tena.

Anawadharau wazazi wangu, yeye anasikiliza sana maneno kutoka kwa mama yake, mimi hata niseme nini sisikilizwi, ila mama yake chochote anachomwambia ndiyo anakifuata.

je nini nifanyeje, nimuache aendelee na maisha yake, au nifanyeje ili akae sawa? Na je, vipi kuhusu watoto wetu watatu, mkubwa miaka 5 (Ke), wa kati ana miaka 3 (Me) na wa mwisho ana mwaka mmoja (Me)?
 
Pole sana ndugu yangu una mapenzi ya dhati kwa mwandani wako lakini yeye ni tofauti kwako
Ushauri wangu kwako. Usimfukuze mwache ifike mahali aondoke mwenyewe.. Kila anachokufanyia simama imara na Mungu wako.. Yeye ndio ataamua huu ugomvi

Chukua muda mwingi kuwa na watoto, wajali, wapende sana hawana na hawatakuwa na baba mwingine wa damu zaidi yako! Mke akiondoka leo akaenda kuolewa kwingine huyo sio wako tena! Lakini wewe utabaki kuwa baba wa wanao mpaka kiama

Wekeza nguvu, muda na chochote ulichonacho kwao.. Wanahitaji ulinzi wako hasa katika kipindi hiki ambapo hakuna wa kumwamini hata ndugu

Simama imara na Mungu wako HATOKUACHA
 
Kosa lilianzia pale alipotoroka alaf "ukapambana" kumrudisha.
Tayari hapo ulikua udhaifu sana. Kama mwanamke aliweza kuwaacha watoto wake aliowazaa mwenyewe kwa uchungu, wewe ni nan asikuache? Shtuka negro, ushaonekana kupe a.k.a king'ang'anizi.
Wanawake hua wanajitahd kuficha madhambi yao, lakn kama anakuonyesha wazi na dharau juu, unapoteza muda tu hapo.
Watoto wasikupe shida, utapata solution tu na watakua bila shida yoyote. Lakini kwa spidi hii ya mke wako, jiandae kufa na kuwaacha watoto
 
Ni lazima mke amheshimu mume kama ilivyo kwa mume kumsikiliza mke. Huyo kafuata hela yako tu bado hajakomaa katika sekta ya ndoa. Hata ukimvumilia kwa namna yyt ile mbeleni upo uwezekano Mkubwa sana atakuacha akadange ili apate hela.

Fanya hima bado mapema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri mbaya
Kaanga chumvi ya mawe kwenye jiko la mkaa, chombo kiwe kigae cha chungu kilivyovunjika, changanya na picha yake ya passport size,jina kwenye karatasi, changanya na pilipili manga huku ukinuizia utakayo(yasiwe mema) chumvi ikipaparika mpaka ikatulia chukua kipande cha kaniki funga hiyo mixer na uzi mwekundu kisha katupe njia panda ama chooni
 
Bwana kaka kiukweli haya ni maisha tu,ushauri wangu nakushauri uwe Ignorer kama utakuwa na uwezo,yan Don't care. Kwasababu naona hii ni tiba nzuri sana ya kuweza kumtibu mtu wa namna hiyo,lakini kila anachokitanya wewe unagomba yeye ndio anaona Raha anajiskia amani sana. We cha kufanya muwache afanye upuuzi wake woote alafu you just shows no any negative reactions to her. Alafu utakuja kutupa majibu. Cha kuzingatia ni wewe kuwa na amani saa zote,tafuta pesa,pendeza. Usishinde nae maskani we shinda harakati.(Yani muda mwingi usikae nae alafu waka kinoma yani) Utakuja Kutupa Mrejesho . Tafadhali fuata huu ushauri.


#Don't care . Ishi humo Brother wetu
 
Ushauri mbaya
Kaanga chumvi ya mawe kwenye jiko la mkaa, chombo kiwe kigae cha chungu kilivyovunjika, changanya na picha yake ya passport size,jina kwenye karatasi, changanya na pilipili manga huku ukinuizia utakayo(yasiwe mema) chumvi ikipaparika mpaka ikatulia chukua kipande cha kaniki funga hiyo mixer na uzi mwekundu kisha katupe njia panda ama chooni
We bwana em toa ushauri wa kisomi. Uchawi huo sio mzuri bhn. Ifute tu hii Boss Kubwa. Utawafanya wengi wakafanye jambo hili ambalo ni Shirki alafu wasijue hatima yake inakuwaje
 
Wanawake ni pasua kichwa.. kilichonifanya nimrudishe ni kwa sababu ya watoto lakini pia niliona hata nikiwa na mwingine huenda na yeye huko mbeleni akabadilika ndio nikaona bora kumrudisha nilomzoea kumbe ndio ilikua nachochoea moto.. ila asanteni sana kwa maoni na ushauri..
 
Naheshimu ushauri uliopewa hapo juu na wasomaji wenzangu, lkn chukua huu wa kwangu.

Kama anakudharau kwasabb umefulia, piga chini oa mwingine. Kwasabb siku ukiugua, let say ukipooza ama ukipata ajali halafu madaktari wakakukata miguu yote utatelekezwa kisha utaachwa.

BTW, kwani yeye ndiye mgawa oxygen? Au k yake Ina bando? Acha uoga mtoto wa kiume mpige chini oa mfuliaji mwenzio e.g muuza mchicha.

Kama vipi njoo unioe mm ambaye kazi yangu ni baa medi.
 
Jukumu kubwa kwa Sasa ulilonalo ni Kuwalinda hao watoto wako

Hakikisha unawapenda Sana watoto wako.
Hakikisha unamu ignore kabisa huyo mwanamke na asiwe kabisa kwenye ratiba za maisha yako.

Fanya mpango uwe na mwanamke wa pembeni ambaye ndiye atakuwa mwandani wako.

Hakikisha huongezi tena mtoto mwingine na huyo mama.

Hakikisha huteteleki kwenye kipato.

Hakikisha unafanya Maendeleo yako kimya kimya bila kumuhusisha kabisa.

Huyo tayari ameshakuwa adui yako. Tatizo kubwa tulio nalo sisi wanaume tunachukulia poa Sana mwanamke akishabadilika kwa namna hiyo.

Usichukulie poa kabisa.
 
Bila shaka atakuwa amelelewa na single mother. Narudia tena kutoa ushauri usijichanganye kuoa mwanamke aliyelelewa na single mother. Kwa.maneno mengine usioe mwanamke ambae mama yake ni single mother. Ukibisha shauri yako
 
Iyo tayar ni nyoka ilishakimbilia kwenye majani,achana nayo itaja kukung'ata bure,unapigana kuirudisha ndani?!
 
Ushauri mbaya
Kaanga chumvi ya mawe kwenye jiko la mkaa, chombo kiwe kigae cha chungu kilivyovunjika, changanya na picha yake ya passport size,jina kwenye karatasi, changanya na pilipili manga huku ukinuizia utakayo(yasiwe mema) chumvi ikipaparika mpaka ikatulia chukua kipande cha kaniki funga hiyo mixer na uzi mwekundu kisha katupe njia panda ama chooni
Kaka... Naona umerudia Tena kazi yako.
 
Back
Top Bottom