Je, nimruhusu aje kunitembelea mkoa nilipo?

Je, nimruhusu aje kunitembelea mkoa nilipo?

Habari wakuu katika Jukwaa Pendwa!

Niwarudishe nyuma kidogo. Mwaka 2011 nilibahatika kua na Mahusiano na binti Aliekua anaitwa Asha (sio jina halisi) tuliweza kudumu katika mahusiano yale kwa miaka miwili lakini nilipata safari familia yetu tukahama kwa sababu za kazi upande wa wazazi wangu.

Huyu binti alikua ananipenda sana kila Aliyekua karibu yangu alikua anajua ni jinsi gani napendwa na huyu Binti ilifika kipindi mpaka alikua hawezi kusoma asiponiona mimi. Alitumia Muda wake mwingi kuwa na mimi karibu,Zawadi za hapa na pale zilikua nyingi sana.

Wakuu kipindi hicho mimi bado nilikua young sana na tulikua shule na hata maswala ya Mahusiano ya kimapenzi nilikua sijaanza kabisa"yaani sumu ya penzi nilikua sijailamba" hivyo huyu binti nilikua namuogopa sana although alikua ananipa nafasi nyingi sana ila nilikua nazikwepa sana.

Washkaji zangu walikua wananicheka sana. Muda mwingine hadi walitani wao wawe mimi ila binti alikua anawachomolea nje na baadae ananiambia kila kitu.

Baada ya kuwa mbali kwa muda kidogo (kupotezana) .mwaka 2017 huyu binti Asha alinipata kupitia Mtandao wa facebook na tukabadilishana mawazo na mawasiliano pia. Niliitaji kufahamu kiundani kuusu anapatikana wapi na anajishughulisha na nini. Alinipa ushirikiano nikaweza kufahamu yote hayo kuwa alikua Anafanyakazi kampuni moja ya Madini kama Kama Mwasibu huko Mwanza.

Basi tukawa tunajuliana hali mara kwa mara. Siku moja aliniomba muda niweze kuongea nae jambo(Via phone call)Nikampa nafasi tuliongea Mengi sana ila Nilishangaa sana alianza kuniomba Msamaha kuwa alipata ujauzito na Aliempa Ujauzito alimkataa. Hii ishu iliniumiza sana nikamfariji sana.

Mawasiliano yetu kupitia simu yaliendelea mpaka hivi majuzi ambapo Binti huyu amekua akicheki mara kwa mara huku akinitumia Miamala ya kifedha. Nikiuliza ya nini anasema anafurahi kuona nakua sina mawazo haswa napokua na jambo linalohitaji utatuzi wakifedha. Amekua akiniita kila jina La kimahaba ila anapenda sana kuniita "My Boss.." . Pia amekua akimpa mwanae simu niongee nae na akimwambia "msalimie baba" Mtoto amekua akijua kua mimi ndio baba yake na ana miaka mitatu pia amekua akiniuliza sana lini narudi nyumbani. Mimi huwa napenda sana Watoto hivyo kuhusu hili jambo linakua linaniumiza sana kama binadamu bila kujali uhusiano wa mm na mtoto.

Binti huyu anajua fika niko ktk mahusiano lakini amekua akiamini kua mimi ndio furaha yake na ndio Mfariji wake mkuu ktk kila jambo. Yaani wakuu haipiti masaa matano najuliwa khali. Binti amekua akionesha dhahiri kua bado ana ndoto na mimi,Leo amenipigia simu akiniomba ruhusa nimruhusu aje Mkoani Mbeya Tuonane.

Wakuu naombeni ushauri Nimkataze asimwambie mtoto asiniite Baba? Pia Nimruhusu aweze kufika Mbeya au nimkatalie. Mpaka sasa bado sjampa majibu sahihi!

●Wakuu Mwanamke akikupenda kapenda. Yaani hajali lolote.

●Mwanaume ukimfanya mwanamke mliechana ktk mahusiano kua rafiki Atakuheshimu sana.

●Mwanaume ukiwa na Busara Mwanamke atakuheshimu pia.
Kama unapenda kubadilisha jia angani na kumwacha ulie naye kwa sasa mwambie aje mwaze maisha upya.
Ila kama una rafiki mwingine na una future naye na hutaki kumwacha basi huyo wa kwanza mwambie ukweli hauko tayari kubadisha msimamo wako tena.
Kama hutafanya hivyo basi endelea kujichanganya. Kuna siku utaomba ushauri mara oh kapata mimba mara oh wote wananipenda ..
 
Akija mwambie ashukie Nanenane afu mm ntakuletea mpaka home kwako usisahau kunitumia no yake pm ahsante
 
Hayo mapitio yako yamefanana exactly na yangu ila mimi nilikua naitwa uncle na pia akawa anakuja mkoa niliikua ninaishi tukawa tunafanya yetu na alikua sio mchoyo yeye mda wote tukikutana lazima aseme anataka mambo mpaka akaanza kutoelewana na jamaa ake wa huko mkoa aliopo na nikapata ushauri kwa watu mbalimbali ila kumuelezea kwamba inabidi tuache ilikua shughuli nzito aliumia sana hadi leo najutia kwa nin niliingia kwenye mahusiano na yeye
 
Naona dalili ya kumuumiza uliyenaye sasa ili umfurahishe ex wako then mwisho utakuja kuumizwa wewe na huyo ex wako.Baba mtoto atakuja na kuungana na family yake.
 
Kwanza iko hivi, ningekuwa mm ningeangalia kati ya hao2 ni yupi nampenda zaidi, na lingine ambalo ningechunguza kati ya hao 2 ni yupi ananipenda zaidi. Dogo ukioa mwanamke ambaye unampenda ila yeye hakupendi nakwambia utalia kila siku. Kama kuna mwanamke yuporadhi kupoteza kila kitu kwa ajili yako basi huyo ndo kila kitu kwako. Yaan huyo dada ni wale ambao anamnunulia gari mumewe huku yeye akipanda boda. Ningekuwa mimi ningemwoa bila hata ya kumuuliza maswali mengi.
 
Back
Top Bottom