Je, nimekosea kuwapotezea baadhi ya ndugu zangu? Naomba ushauri tafadhali

Tatizo Mzee wangu hanielewi. Ila yeye nimemsamehe. Matatizo yake na marehemu mama yangu niliyaweka pembeni. Ninasimamia hali yake ya afya na matunzo ya kila siku
Umemdekeza huyo mzee sana pia
 
Maisha ya tabu uliyoyapitia ndio sababu kuu ya wewe kufanikiwa,ulifight kwa nguvu zako zote ili ufanikiwe kutokana na ubaya uliyofanyiwa,

Hapo ina maanisha kua,hao waliokufanyia ubaya nao pia wana mchango wao kwenye mafanikio yako,bila shaka kama wasingekufanyia ubaya usingepata ujasiri wa kufight na kufanikiwa,

Unaweza kuwasaidia tu haina shida ila kua nao mbali na usijenge mazowea nao,ila kama wamekuomba msamaha basi potezea tu mkuu na uwasamehe,huwezi jua kua pengine Mungu alikupitisha kwenye mtihani ule ili iwe ndio sababu ya wewe kufanikiwa leo.
 
Nimesoma reply za mleda mada ila inaonekana kabisa kua yeye tayari anayo maamuzi yake na kumshauri hapa ni kazi bure tu,sijui hata ni ushauri upi alioutaka hapa!

Au hii thd nayo ni tangazo? Kama ni tangazo basi watakuja PM.
😀😀
 
Labda niseme hv, nimesoma na kukuelewa fika ila kikubwa nachotaka kugusia mm kwenye hii historia yako ni kuhusiana na jeraha ulilonalo moyoni mwako. Kama mtu niliyekwisha pitia psychological trauma ktk makuzi yangu tena kutokea kwenye familia au niseme watu wa karibu ni ngumu kusahau hata kama ukijaaliwa kutimiza malengo yako maishani. Kuhusiana na kuwasaidia au kutowasaidia ndugu zako hapo ni bora ufuate moyo wako, najua hali unayopitia sasa inakuweka njia panda lakn fuata mwitiko wa nafsi na moyo wako, it would make you happy and no regrets. Bila kusahau kumuomba Mungu.
Mungu akubariki na familia yako
 
Nawasalimu nyote!

Moja kwa moja kwenye mada, historia yangu ina changamoto nyingi. Naamini kila mmoja ana changamoto yake. Kwa kifupi ni kwamba nimezaliwa kwenye familia ya wake wawili.

Mama yangu ni mke wa pili kwa Mzee. Aliolewa na Mzee baada ya mamkubwa kufariki miaka ya sabini. Nikiwa mdogo sana sikuona sikujua tofauti mpaka nilivyokuwa na umri wa kupambanua mambo. Mama yangu (sasa marehemu) alikuwa mpole sana na aliwapokea wototo wa mumewe bila shida.

Tatizo ni kwamba mama yangu alikuja kupatwa na ugonjwa mmoja mbaya sana, sitalitaja lakini ule ungonjwa ukawa ndiyo mwanzo wa matatizo yooote. Kwanza Mzee wangu anaonekana alimind Kwanini babu yangu alimuozesha mama yangu huku akijua binti yake anaumwa. Nilivyokuja kufanya utafiti, nilikuja kuambiwa kwamba mama yangu hakuwahi kuumwa kabla ya kuolewa na hata alipoolewa ilichukua miaka kadhaa ndo ugonjwa ukazuka.

Huu ugonjwa ulepelekea mama yangu kuwa kama mlemavu fulani hivi. Ikawa chanzo cha unyanyapaa usiyomithilika. Katika ukoo wetu baadhi hawakusema moja kwa moja kwa heshima ya Mzee lakini chini chini tuliishia kudharauliwa sana, mama yangu alidharauliwa sana. Kibaya zaidi ni kwamba mtoto wa kiume wa kwanza kwa mamkubwa alikuwa sehemu ya waliotudharau. Baadae alivyooa mke wake akawa ndo kabisaaaaaa. Kwake hata uji kunywa ilikuwa mbinde.

Kipindi hicho Mzee anapata vijisenti kidoog kidoog akafanikiwa kuwasomesha watoto wa Nyumba kubwa kwa alivyoweza. Kaka yangu mkubwa akapelekwa chuo cha ualimu baadae akaajiriwa na serikali, mtu wa kwanza kwenye ukoo kuajiriwa serikalini. Kichwa kikavimba. Mdogo wake pia wakiume akapelekwa naye chuo cha ualimu akapata ajira. Mdogo wao wa mwisho akapelekwa mpaka sekondari akaja kuolewa na mwanaume mwenye kipato cha wastani hivyo kiburi ikaongezeka.

Sisi kwa upande wetu, dada yangu mkubwa nakumbuka alikimbilia kuolewa akiwa mdogo sana kutokana na manyanyaso ya wana ukoo. Mimi nikaja kusoma sekondari kwa kujilipia. Kila wikendi nilikuwa narudi kijijini kukata miti ambayo Mzee alikuja kuingia dili na shule kununua kwa matumizi ya jikoni hivyo ikawa kama ada yangu.

Nakumbuka Mzee aliwahi kutoa kauli kwamba sisi watoto wa mke mdogo tunamsumbua na hatuna manufaa kama walivyo wale wa mamkubwa. Nilimind sana ila sikuwa na jinsi. Kwa watoto wa kiume upande wa mama, mimi ndiye mkubwa.

Nilivyomaliza sekondari sikufaulu vizuri na Mzee akawa hana mpango wa kunipeleka chuo. Bahati mbaya sijui niseme bahati nzuri. Wakati namaliza sekondari, dada yangu upande wa mamkubwa akawa anahitimu naye ualimu Ekenford Tanga. Alipokuwa anasoma Tanga, alijenga urafiki na familia moja ya kisambaa ambayo walimpa binti yao aje kumtembelea kwetu kujenga undugu.

Huyu binti nilikutana naye kwa wito wa dada yangu aliyenitaka nimuonyeshe mji wetu kidogo. Bahati mbaya tukapendana. Tatizo likawa naye amemaliza form four na alikuwa na mpango wa kuendelea na form five.

Nilichofanya ni kutafuta sababu ya kuja Dar ili niwe Karibu naye. Baadae akajiunga na high school Mpwapwa. Mtoto alikuwa mbichi, utepe niliukata mimi. Tatizo ni kwamba dada yangu alipogundua tupo serious hakupenda na mpaka leo sijajua ni kwanini na sikuwahi kumuuliza kwani alichofanya ni kuja Dar akakutana na familia ile, wakati huo mama wa huo binti na dada zake walikuja Dar, alinichafua sana.

Kilichofuata ni kwamba yule binti alipigwa biti sana na ndugu zake kiasi cha yeye kuchanganyikiwa. Wakati huo yeye bahati mbaya alikuwa shuleni hivyo hakuweza kunitetea dhidi ya uwongo ulokuwa unasemwa juu yangu.

Siku fanya lolote, nilichomuambia dada baada ya kupata zile taarifa ni “mwisho wa ubaya ni aibu” nikatulia.

Yule binti tulikuja kuachana kwani maji yalichafuka sana. Sasa baada ya pale shemeji yangu (mume wa dada) biashara ikabuma. Akafilisika kabisa mpaka kesho.

Katika kufilisika huko, ikabidi dada atafute kazi akahitaji kwenda kusomea kozi ya kufundisha shule maalumu. Nikaombwa kupitia dada yangu tumbo moja nimchukue binti yake aje anisaidie kukaa na mtoto badala ya kumuajiri mtu mwingine. Hii hoja ilikuwa ni kumsaidia dada yangu (mfini ni wangu) apate ada. Bila hiyana nilitoa ushirikiano na kumlipa hela kiasi ambacho asingepata kwa mwingine. Nilimpiga sound mke wangu (Mzungu) aelewe Kwanini tunamlipa dada kiasi kikubwa vile.

Cha ajabu baadae yule mpwa wangu akawa na tabia za kijinga tu ambazo hazieleweki hususani kwa namna ambavyo alikuwa ana relate na mimi ila nikapotezea. Baada ya yeye kuondoka na miaka ikapita nilishangaa kumbe kipindi yupo kwangu, mama yake alianza tena kuingilia ndoa yangu. Akatia fitina za kutosha. Haya nilikuja kujua siku moja tulikuwa na ugomvi wa nyumbani na mke wangu, kwa hasira akafunguka yote aliyokuwa akiambiwa na dada yangu kupitia mpwa wangu. Kumbuka hapo nimempa hela ndefu tu ya kulipia ada akanipa binti yake anisaidie kwa wakati ule.

Sasa mimi historia ya kunyanyapaliwa mama yangu na sisi watoto wake, bahati mbaya sana mambo yamebadilika mimi kusema kweli ndo nina kipato cha kueleweka, upande wa nyumba kubwa wanataka niwape tafu. Jambo hili sijaliafiki kwani hawakunipa hata pocket money wakati nasoma, hawakunilipia ada ila mafanikio yangu wanataka kuyafaidi.

Mzee ninamtunza kwa kidogo nachopata, niliwajengea nyumba ya uhakika ila kwa ndugu hawa nimekataa kabisa.

Sasa leo nimekuja hapa kupata ushauri, Mzee wangu amenitafuta kwamba dada (mfitini) amemuomba amsaidie kuniomba 5m ana shida kubwa. Hata kama ni kukopa. Nafsi inagoma kabisa. Yeye mwenyewe hawezi kuniomba moja kwa moja.

Nikiri kwamba alishaniomba msamaha mwaka 2018. Ila huu msamaha uliombwa kimkakati kwasababu uchumi wao ulishayumba ikawa jeuri haipo tena. So ilikuwa ni kama kutafuta njia ya kunirudisha kwenye anga zake.

Nisaidieni ushauri.
Achana nao hao. Watakuloga. Mchawi siku zote hawezi kukuloga mkiwa mmechukizana lazima aweke urafiki ili hata anakuharibia anakupa pole. Potezea kabisa. Ishi maisha yako waishi maisha yao. Hela hiyo nyingi sana.
 
Nakushauri Dala.... tumia lugha nzuri yenye diplomasia kwa ndg zako... kama hutaki kusaidia. tafuta sbb ya kueleweka ili waridhie.. usikatae ili mradi tu.. kuwa muungwana na mpole.
Akatae kutoa msaada kiakili ila siyo kwa uwazi. Kuwa mlifajya hivi au vile. Misaada atoe midogo midogo isiyo umiza
 
Nimesoma reply za mleda mada ila inaonekana kabisa kua yeye tayari anayo maamuzi yake na kumshauri hapa ni kazi bure tu,sijui hata ni ushauri upi alioutaka hapa!

Au hii thd nayo ni tangazo? Kama ni tangazo basi watakuja PM.

Mkuu, mimi nilijifanya kudharau kitu kinaitwa trauma mpaka nilipokuja kujitathmini baadae sana. Hawa watu walinifanya nimpuuzie hata mama yangu kabla sijajitambua.

Nakumbuka siku moja nikiwa ghetto ninatafakari uhusiano wangu na mama yangu na namna inavyomuathiri. Nililia sana usiku ule. Asubuhi nilichukua simu nikampigia mama, kuanzia siku ile, niliapa kumtetea mama yangu kwa silaha zangu zote. Hakika, mama amefariki akiwa na amani na furaha kwamba nilimtetea inavyotakiwa.

Kuhusu uamuzi inawezekana nikaonekana nimeshaamua kutokuwasaidia ila bado kuna presha na kujihoji kama nachofanya ni sahihi. Kuna mengi sijayataja kwasababu ya muda.
 
Msamehe mzee na umtunze,hao wengine ukianza tu kuwasaidia ndo wanaweza kuwa your downfall!binadamu wabaya,tena wanaweza kwenda kwa mganga wakuroge ufilisike,acha mazoea nao kabisa
Akufaaye kwa dhiki ndie rafiki,usisahau hilo
Huyo mzee naye ni wa kumchana. Kumsaheme mtu as if nothing happen hapana. Watu hawajifunzi.
 
Mzee siku hizi kama piriton maana nyumba mimi ndo nilikuja kumjengea wakati mwanaye aliyemsomesha na kupata kazi serikali hakujali.

Siku hizi anatambua kwamba mimi ndo nipo kwa ajili yake. Ila kumkumbusha naona siyo Sawa. Nafanya yangu nasubiri afe tu zake maana umri umeenda
Kaa naye umkumbushe ajue fika alifanya ujinga...

Mambo ya kusamehe as if nothing happen hapana.
 
Nawasalimu nyote!

Moja kwa moja kwenye mada, historia yangu ina changamoto nyingi. Naamini kila mmoja ana changamoto yake. Kwa kifupi ni kwamba nimezaliwa kwenye familia ya wake wawili.

Mama yangu ni mke wa pili kwa Mzee. Aliolewa na Mzee baada ya mamkubwa kufariki miaka ya sabini. Nikiwa mdogo sana sikuona sikujua tofauti mpaka nilivyokuwa na umri wa kupambanua mambo. Mama yangu (sasa marehemu) alikuwa mpole sana na aliwapokea wototo wa mumewe bila shida.

Tatizo ni kwamba mama yangu alikuja kupatwa na ugonjwa mmoja mbaya sana, sitalitaja lakini ule ungonjwa ukawa ndiyo mwanzo wa matatizo yooote. Kwanza Mzee wangu anaonekana alimind Kwanini babu yangu alimuozesha mama yangu huku akijua binti yake anaumwa. Nilivyokuja kufanya utafiti, nilikuja kuambiwa kwamba mama yangu hakuwahi kuumwa kabla ya kuolewa na hata alipoolewa ilichukua miaka kadhaa ndo ugonjwa ukazuka.

Huu ugonjwa ulepelekea mama yangu kuwa kama mlemavu fulani hivi. Ikawa chanzo cha unyanyapaa usiyomithilika. Katika ukoo wetu baadhi hawakusema moja kwa moja kwa heshima ya Mzee lakini chini chini tuliishia kudharauliwa sana, mama yangu alidharauliwa sana. Kibaya zaidi ni kwamba mtoto wa kiume wa kwanza kwa mamkubwa alikuwa sehemu ya waliotudharau. Baadae alivyooa mke wake akawa ndo kabisaaaaaa. Kwake hata uji kunywa ilikuwa mbinde.

Kipindi hicho Mzee anapata vijisenti kidoog kidoog akafanikiwa kuwasomesha watoto wa Nyumba kubwa kwa alivyoweza. Kaka yangu mkubwa akapelekwa chuo cha ualimu baadae akaajiriwa na serikali, mtu wa kwanza kwenye ukoo kuajiriwa serikalini. Kichwa kikavimba. Mdogo wake pia wakiume akapelekwa naye chuo cha ualimu akapata ajira. Mdogo wao wa mwisho akapelekwa mpaka sekondari akaja kuolewa na mwanaume mwenye kipato cha wastani hivyo kiburi ikaongezeka.

Sisi kwa upande wetu, dada yangu mkubwa nakumbuka alikimbilia kuolewa akiwa mdogo sana kutokana na manyanyaso ya wana ukoo. Mimi nikaja kusoma sekondari kwa kujilipia. Kila wikendi nilikuwa narudi kijijini kukata miti ambayo Mzee alikuja kuingia dili na shule kununua kwa matumizi ya jikoni hivyo ikawa kama ada yangu.

Nakumbuka Mzee aliwahi kutoa kauli kwamba sisi watoto wa mke mdogo tunamsumbua na hatuna manufaa kama walivyo wale wa mamkubwa. Nilimind sana ila sikuwa na jinsi. Kwa watoto wa kiume upande wa mama, mimi ndiye mkubwa.

Nilivyomaliza sekondari sikufaulu vizuri na Mzee akawa hana mpango wa kunipeleka chuo. Bahati mbaya sijui niseme bahati nzuri. Wakati namaliza sekondari, dada yangu upande wa mamkubwa akawa anahitimu naye ualimu Ekenford Tanga. Alipokuwa anasoma Tanga, alijenga urafiki na familia moja ya kisambaa ambayo walimpa binti yao aje kumtembelea kwetu kujenga undugu.

Huyu binti nilikutana naye kwa wito wa dada yangu aliyenitaka nimuonyeshe mji wetu kidogo. Bahati mbaya tukapendana. Tatizo likawa naye amemaliza form four na alikuwa na mpango wa kuendelea na form five.

Nilichofanya ni kutafuta sababu ya kuja Dar ili niwe Karibu naye. Baadae akajiunga na high school Mpwapwa. Mtoto alikuwa mbichi, utepe niliukata mimi. Tatizo ni kwamba dada yangu alipogundua tupo serious hakupenda na mpaka leo sijajua ni kwanini na sikuwahi kumuuliza kwani alichofanya ni kuja Dar akakutana na familia ile, wakati huo mama wa huo binti na dada zake walikuja Dar, alinichafua sana.

Kilichofuata ni kwamba yule binti alipigwa biti sana na ndugu zake kiasi cha yeye kuchanganyikiwa. Wakati huo yeye bahati mbaya alikuwa shuleni hivyo hakuweza kunitetea dhidi ya uwongo ulokuwa unasemwa juu yangu.

Siku fanya lolote, nilichomuambia dada baada ya kupata zile taarifa ni “mwisho wa ubaya ni aibu” nikatulia.

Yule binti tulikuja kuachana kwani maji yalichafuka sana. Sasa baada ya pale shemeji yangu (mume wa dada) biashara ikabuma. Akafilisika kabisa mpaka kesho.

Katika kufilisika huko, ikabidi dada atafute kazi akahitaji kwenda kusomea kozi ya kufundisha shule maalumu. Nikaombwa kupitia dada yangu tumbo moja nimchukue binti yake aje anisaidie kukaa na mtoto badala ya kumuajiri mtu mwingine. Hii hoja ilikuwa ni kumsaidia dada yangu (mfini ni wangu) apate ada. Bila hiyana nilitoa ushirikiano na kumlipa hela kiasi ambacho asingepata kwa mwingine. Nilimpiga sound mke wangu (Mzungu) aelewe Kwanini tunamlipa dada kiasi kikubwa vile.

Cha ajabu baadae yule mpwa wangu akawa na tabia za kijinga tu ambazo hazieleweki hususani kwa namna ambavyo alikuwa ana relate na mimi ila nikapotezea. Baada ya yeye kuondoka na miaka ikapita nilishangaa kumbe kipindi yupo kwangu, mama yake alianza tena kuingilia ndoa yangu. Akatia fitina za kutosha. Haya nilikuja kujua siku moja tulikuwa na ugomvi wa nyumbani na mke wangu, kwa hasira akafunguka yote aliyokuwa akiambiwa na dada yangu kupitia mpwa wangu. Kumbuka hapo nimempa hela ndefu tu ya kulipia ada akanipa binti yake anisaidie kwa wakati ule.

Sasa mimi historia ya kunyanyapaliwa mama yangu na sisi watoto wake, bahati mbaya sana mambo yamebadilika mimi kusema kweli ndo nina kipato cha kueleweka, upande wa nyumba kubwa wanataka niwape tafu. Jambo hili sijaliafiki kwani hawakunipa hata pocket money wakati nasoma, hawakunilipia ada ila mafanikio yangu wanataka kuyafaidi.

Mzee ninamtunza kwa kidogo nachopata, niliwajengea nyumba ya uhakika ila kwa ndugu hawa nimekataa kabisa.

Sasa leo nimekuja hapa kupata ushauri, Mzee wangu amenitafuta kwamba dada (mfitini) amemuomba amsaidie kuniomba 5m ana shida kubwa. Hata kama ni kukopa. Nafsi inagoma kabisa. Yeye mwenyewe hawezi kuniomba moja kwa moja.

Nikiri kwamba alishaniomba msamaha mwaka 2018. Ila huu msamaha uliombwa kimkakati kwasababu uchumi wao ulishayumba ikawa jeuri haipo tena. So ilikuwa ni kama kutafuta njia ya kunirudisha kwenye anga zake.

Nisaidieni ushauri.
follow your heart boss, a day will come utadrop pia, jipange ila wakazie we humans ain't good
 
Labda niseme hv, nimesoma na kukuelewa fika ila kikubwa nachotaka kugusia mm kwenye hii historia yako ni kuhusiana na jeraha ulilonalo moyoni mwako. Kama mtu niliyekwisha pitia psychological trauma ktk makuzi yangu tena kutokea kwenye familia au niseme watu wa karibu ni ngumu kusahau hata kama ukijaaliwa kutimiza malengo yako maishani. Kuhusiana na kuwasaidia au kutowasaidia ndugu zako hapo ni bora ufuate moyo wako, najua hali unayopitia sasa inakuweka njia panda lakn fuata mwitiko wa nafsi na moyo wako, it would make you happy and no regrets. Bila kusahau kumuomba Mungu.
Mungu akubariki na familia yako

Ninajenga familia yangu ndo nguzo yangu
 
Halafu watu mnaenda kanisani na msikitini, hivi huwa mnaenda kwa dhumuni gani kama hamuwezi kujenga upatanishi ?
Nimejifunza hspa kua watanzanua wamejaa roho za visasi na chuki.
Ngoja niendelee kusoma maoni.
 
Halafu watu mnaenda kanisani na msikitini, hivi huwa mnaenda kwa dhumuni gani kama hamuwezi kujenga upatanishi ?
Nimejifunza hspa kua watanzanua wamejaa roho za visasi na chuki.
Ngoja niendelee kusoma maoni.

Mkuu hawa ndugu zangu niliyowataja ni walokole, kaka ni mchungaji kabisa na dada ni mlokole huwezi kuamini kama ni yeye alinifanyia vile. Hivyo hoja ya imani hapa inapoteza mashiko. Actually mimi peke yangu ndo sina ushirikiano na dini kabisa.
 
Mimi yupo jamaangu alipata matatizo nadhani wewe unasubiri mbali mno mno na ana kipato cha ukweli alisema mkuu mimi hawa nawasamehe ni umasikini tuu ndio ulikua unawasumbua kwa kuwajengea roho mbaya na mimi hii roho nisipobadilika tutakua na ukoo wenye roho mbaya aliwasaidia wote na maisha yanaenda ingawaje mpaka kesho hawaamini...hata mimi hao ningewasamehe tuu ila sio kuwa nao karibu ki vile maisha yaendelee hakuna kitu kizuri kama upo njema harafu familia ina furaha pia...
 
Back
Top Bottom