Ndugu wana JF, jana na leo nimekua nikifuatilia vyombo vya habari na ususani tamko alilotoa Waziri wa Ulinzi kua wanajeshi hawatakiwi kutoa nauli. Mpaka sasa najaribu kuwaza ni kigezo kipi kimetumika kutoa msamaha hua na hasa pale wanajeshi wanapopanda magari ya watu binafsi.
Kwa upande wangu mimi nadhani si sahihi kwa wanajeshi na polisi kutolipa nauli. Hapa nchini tuna wafanyakazi wa aina nyingi kama walimu, madakitari, polisi, wanajeshi, wahasibu, mahakimu n.k. Sasa iweje hawa maaskari wasilipe nauli wao tu? Haiingi akilini kwa kusema ukweli. Hata kama wanalinda taifa sii sahihi kutolipa nauli pale wanapotumia vyombo vya usafiri vya watu binafsi, kama ni magari ya serikali hapo sawa.
Nadhani ingekua busara sana kumpigania mwanafunzi ambaye hana kipato chochote kutolipa nauli, inashangaza mwanafunzi asiye na kazi kulipa nauli halafua askari wetu wenye kazi na mishahara hawalipi nauli. Tunamganadamiza mfanyabiashara wa usafiri, mwanafunzi atoe mia moja, askari asilipe, Je! Atarudishaje gharama za uendeshaji? Chukulia kwa mfano Hiace moja ipande askari 8 na wanafunzi 8 je gari si imeshajaa hapo? Yaani uende tripu kwa sh 800.
Ni muhimu sana askari wetu kulipa nauli kama wafanyakazi wengine, wanafunzi na vilema wanavyolipa.
Je wewe mwana JF una Maoni Gani?
Naomba kuwasilisha hoja
Kwa upande wangu mimi nadhani si sahihi kwa wanajeshi na polisi kutolipa nauli. Hapa nchini tuna wafanyakazi wa aina nyingi kama walimu, madakitari, polisi, wanajeshi, wahasibu, mahakimu n.k. Sasa iweje hawa maaskari wasilipe nauli wao tu? Haiingi akilini kwa kusema ukweli. Hata kama wanalinda taifa sii sahihi kutolipa nauli pale wanapotumia vyombo vya usafiri vya watu binafsi, kama ni magari ya serikali hapo sawa.
Nadhani ingekua busara sana kumpigania mwanafunzi ambaye hana kipato chochote kutolipa nauli, inashangaza mwanafunzi asiye na kazi kulipa nauli halafua askari wetu wenye kazi na mishahara hawalipi nauli. Tunamganadamiza mfanyabiashara wa usafiri, mwanafunzi atoe mia moja, askari asilipe, Je! Atarudishaje gharama za uendeshaji? Chukulia kwa mfano Hiace moja ipande askari 8 na wanafunzi 8 je gari si imeshajaa hapo? Yaani uende tripu kwa sh 800.
Ni muhimu sana askari wetu kulipa nauli kama wafanyakazi wengine, wanafunzi na vilema wanavyolipa.
Je wewe mwana JF una Maoni Gani?
Naomba kuwasilisha hoja