Je, ni sahihi kuomba uchangiwe mahari?

Je, ni sahihi kuomba uchangiwe mahari?

Lovehate

Member
Joined
Apr 26, 2018
Posts
52
Reaction score
75
Huwa mnafanyaje katika hali kama hii.

Uwezo wa kuhudumia mke na mtoto mmoja upo lakini ukisema usubiri ujichange hadi uwe na mahari inayotakiwa ni parefu. (1,000,000)

Je ni sahihi kuomba uchangiwe mahari??? Si inaweza kuwa mwanzo wa dharau mahari uchangiwe utaweza kutunza mke na mtoto. (watu gani sahihi kuwaambia wanisaidie)

Au niende ukweni nikawaambie ukweli nia ya kuoa ipo na ya ukweli wa dhati ila mahari kwa sasa sina ila nitawalipa kidogo kidigo. (Nitapewa mke kweli ??)

Nilimpa mimba akarudi kwao Mama yake alielewa Baba yake alikasirika sana na mimi nikawekeza nguvu na akili katika kumuhudumia ili aweze kujifungua salama na mtoto aje angalau akute hakuna shida ya kuja duniani.

Amejifungua salama Mungu ni mwema sasa natamani sana kuwa nao karibu mama na mtoto wake kama familia.
 
Ukichangiwa mahari basi kubali kuchapiwa, mahari unaweza kulipa kidogo kidogo mpaka unamaliza
 
Kama mnapendana mwambie mwanamke akutolee mahari Ila Uwe na roho ngumu haswa
 
Back
Top Bottom