Je, alichofanya ni sahihi kuondoka na mtoto bila kuniambia?

trudie

JF-Expert Member
Jan 15, 2014
3,335
7,662
Habari wana JF,

Mimi ni mama wa mtoto mmoja binti wa miaka 4. Mtoto akiwa na miezi 3 tulishindwana na baba wa mtoto hivyo nikaondoka kwake, tulikuwa tunaishi pamoja (alinitolea mahari, hatukufunga ndoa).

Yeye anaishi Mwanza mimi nipo Dar, katika kipindi chote alikuwa anatoa matunzo ya mtoto bila shida na tulikuwa na mawasiliano mazuri kabisa. Mwaka jana alikuja Dar kumsalimia mtoto na akakaa naye wiki moja kwa ndugu zake, akamrudisha, sikuwa na shida maana bado ni baba yake.

Mwezi uliyopita akapata likizo amekuja Dar, kama kawaida akaomba kumwona mtoto na nikamruhusu. Akamchukua, akaa naye siku 3, nikamwomba mtoto nitoke nae mtoko, jioni akamchukua tena.

Sikutaka kuwa namsumbua sana, nikamwachia nafasi akae na binti yake likizo anavyoenda Mwanza amrudishe. Wiki iliyoisha nikampigia simu naomba nitoke mtoko na mtoto wikiendi kama bado upo likizo utaendelea kukaa naye, akawa ananipiga chenga.

Ikabidi nimshirikishe mdogo wake ambapo ndiyo alifikia hapa Dar Madale, ndiyo jana napata taarifa baba mtoto kaondoka na mtoto kaenda naye Mwanza bila kuniambia. Mtoto ana miaka 4 kiukweli nilipaniki na sikupenda.

Je, alichofanya ni sahihi kuondoka na mtoto bila kuniambia? Kisheria imekaa vipi? Naombeni maoni yenu.

NOTE: Bado hajaoa na anaishi peke yake. Yeye anaona kama kafanya kitu sahihi. Yupo humu JF, najua atasoma pia hapa.

UPDATE: Mtoto nimeshamchukua na amesharudi Dar baada ya muda mrefu. Namshukuru Mungu wote tupo salama na pande zote tupo sawa.
 
Miaka 7 ndio ruksa mtoto kwenda kwa baba kisheria.

Amefanya makosa, nenda ustawi wa jamii watakupa mwongozo.

Ila mara nyingi wanaofanya vitendo vya kukimbia na watoto wanasukumwa na mazingira anayoishi mtoto, huenda wanahisi mtoto anateseka au hakai sehemu nzuri ndio hupelekea kuwanyakua kama mwewe.
 
Miaka 7 ndio ruksa mtoto kwenda kwa baba kisheria.
Amefanya makosa, nenda ustawi wa jamii watakupa mwongozo.

Ila mara nyingi wanaofanya vitendo vya kukimbia na watoto wanasukumwa na mazingira anayoishi mtoto, huenda wanahisi mtoto anateseka au hakai sehemu nzuri ndio hupelekea kuwanyakua kama mwewe.
Mtoto anaishi mazingira mazuri na ninajimudu pia na yeye anajua hilo. Shida ilianzia toka wakati kichanga mama yake alitaka kuninyang'anya ili aishi nae yeye.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata hivyo una moyo mzuri mimi ningekua nshafika Mwanza kabla ya kuomba ushauri!

Alichokifanya sio sawa,yeye anaishi mwenyewe ataleaje huyo mtoto tena wa miaka 4 tu?

Wewe baba tumeambiwa unasoma humu rudisha huyo mtoto kwa mama yake wewe ujikite kutafuta pesa kama ni kumuona mbona anakupa unakaa nae?
 
Au ulikua unampiga pesa za matunzo na matumizi ya kughushi akaona isiwe kesi achukue mwanae kibabe
Hapana mkuu hata yeye aje kushudia hapa kama nasema uwongo. Sijawahi kumsumbua wala kumpiga matumizi.

Yeye ndio alipanga kiwango cha kutoa kwa mwezi kutokana na mshahara wake na sijawahi kuomba kabla ya tarehe. Na pia huwa simwombi matumizi terehe aliyopanga ikifika huwa anatuma yeye mwenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata hivyo una moyo mzuri mimi ningekua nshafika mwanza kabla ya kuomba ushauri!
Alichokifanya sio sawa,yeye anaishi mwenyewe ataleaje huyo mtoto tena wa miaka 4 tu?
Wewe baba tumeambiwa unasoma humu rudisha huyo mtoto kwa mama yake wewe ujikite kutafuta pesa kama ni kumuona mbona anakupa unakaa nae?
Mimi binafsi jana nilienda dawati la jinsia akapigiwa simu amrudishe mtoto. Naumia sana mkuu
 
Wewe mwanamke umeamua kuja kunianzishia Uzi huku jf ,huyu ni mwanangu sitaki awe na tabia zako za kilevi na umalaya ,mwanangu nitamlea Mimi .....na usijaribu kuja mwanza ,maana hutampata ..
Acha kutafuta kiki kwenye mambo yasiyokuhusu. Wewe sio baba mtoto wangu.

Hata yeye anajua mama mtoto wake sio malaya wala mlevi hata kwenye nyuzi zake huwa anawashauri wenzie waje kuoa kabila letu. Sijui unafaidika nini kujiproud uongo.
 
Ujue nyie wanawake kinachowaponza ni ubestie....yani unakuta umeolewa vizuri tu....lakini marafiki zako ukaona wao ni wa muhimu kuliko mumeo au familia yako.


I mean,....kujazwa na maneno na marafiki...kisha unaanza kudharau Ndoa yako....kutomheshimu mumeo...uzinzi wa wazi kabisa.

Afu ujue , wanawake wengi huwa hamjui hii kitu...."mwanamke akichepuka then akaja kumeet na Mume wake...hata kama alikua anapendwa vipi...lazima upendo utashuka tu...dharau zitajionyesha wazi"


Note: Kama wewe ndio chanzo cha kuharibika kwà Mahusiano yako....nakwambia kweli hutatoboa. Utaishia kugongwa tu kwasababu laana ya mtu ambae alikua anakupenda kwà dhati ishakupata,..unless utubu.

Ningekua Mimi ndio wewe...nisingejali Sheria za Nchi....bali ningejali nature. Ningemuachia tu na kutizama movie inavyokwenda kimyaaaa....koz KILA jambo lina mwisho. Kuliko kutaka kujiabisha kukimbilia mahakamani.
 
Back
Top Bottom