Je, ni nani mmiliki wa hawa wanyama wakati wa enzi za Yesu?

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,059
24,451
Wadau wote wa humu na wale ambao wamebarikiwa kuwa na ujuzi wa masuala mbalimbali hasa kwenye mambo ya imani n.k ningependa kufahamu na si mimi peke yangu hata wengine pia wangependa kujua je, ni nani aliyekuwa mmiliki wa;-
1.Punda aliyepanda Yesu wakati anaenda Yerusalemu
2.Jogoo aliyewika wakati Petro anamkana Yesu.
 
Wadau wote wa humu na wale ambao wamebarikiwa kuwa na ujuzi wa masuala mbalimbali hasa kwenye mambo ya imani n.k ningependa kufahamu na si mimi peke yangu hata wengine pia wangependa kujua je, ni nani aliyekuwa mmiliki wa;-
1.Punda aliyepanda Yesu wakati anaenda Yerusalemu
2.Jogoo aliyewika wakati Petro anamkana Yesu.

Punda hakuwa na mwenyewe, japo yesu alitoa tahadhari kama mwenyewe atajitokeza basi aambiwe BWANA ANAMHITAJI.
Jogoo yule alikuwa mali ya KAYAFA, ambaye kwa kipindi kile alikuwa kuhani mkuu.
 
Yesu alikuwa na uwezo kutumia usafiri wa kifahari lakini alitumia punda. Leo hii askofu anatumia gari za bei mbaya , imekaaje ? Sawa wakati ule hapakuwa na magari ila kwa kuwa ni mwana wa Mungu angetumia Umungu wake kutumia gari nzuri !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee, kuhani alikuwa anamiliki mali kweli? Maana Mungu aliwataka wale sadaka tu na wasiwe na urithi wowote! Kama niko wrong tukosoane.
Punda hakuwa na mwenyewe, japo yesu alitoa tahadhari kama mwenyewe atajitokeza basi aambiwe BWANA ANAMHITAJI.
Jogoo yule alikuwa mali ya KAYAFA, ambaye kwa kipindi kile alikuwa kuhani mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfano usafiri gani wa kifahari uliokuwapo wakati wa Yesu jamani tuache kudanganyana


Yesu alikuwa na uwezo kutumia usafiri wa kifahari lakini alitumia punda. Leo hii askofu anatumia gari za bei mbaya , imekaaje ? Sawa wakati ule hapakuwa na magari ila kwa kuwa ni mwana wa Mungu angetumia Umungu wake kutumia gari nzuri !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom