Je, ni kweli watu weusi tuna akili ndogo?

FAHAD KING

JF-Expert Member
Sep 14, 2017
301
373
James Watson,mwanasayansi maarufu duniani na mshindi wa nishani ya noble katika tiba mwaka 1962, ameleta mjadala mkubwa kwa madai kwamba inaelekea mtu mweusi ana akili ndogo kuliko mtu mweupe. Kauli hiyo imeshikiliwa bango na wapinzani wa ubaguzi wa rangi kwa madai kwamba inamdhalilisha mtu mweusi.

Hata hivyo Watson si mtu wa kwanza kusema hivyo isipokuwa yeye kaisema kisayansi zaidi. Siku za nyuma Waziri Mkuu mmoja wa Japan alipata kusema maneno kama hayo kwamba anatilia mashaka uwezo wa mtu mweusi. Waziri mwingine pia alishanukuliwa anasema hivyo. Wote baadaye waliomba radhi ila ujumbe ulifika.

Chika Onyeani katika kitabu chake cha The Capitalist Nigger naye anashangaa ni kwanini Mwafrika atukanwe namna hiyo na mawaziri wa Japan, lakini bado waendelee kununua bidhaa kutoka japan. Pia anasema jamii nyingi za watu Weusi zinafanana kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano ukikutana na Muamerika mweusi aliyezaliwa marekani au carribean au afrika kwenyewe bado wanatabia zilezile ambazo zinatia shaka kama kweli akili za mtu mweusi si ndogo kwa kiasi fulani.

Ukianza kuangalia matokeo mbalimbali yaliyotokea Afrika enzi za miaka ya nyuma utaanza kuwa na wasiwasi kuhusu hali ya uelewa wa mtu mweusi.Historia inaonyesha kwamba ,hadi karne ya 16 kiwango cha maendeleo kati ya nchi za Afrika na ulaya kilikuwa sawa

Tunaambiwa pia kwamba miaka ya 1960 baadhi ya nchi za Afrika zilikuwa zimeendelea kimaendeleo au sawa na nchi za Asia ambazo leo ziko mbali kimaendeleo.Bado unajiuliza ni wapi kwenye matatizo? Kwanini waafrika tuachwe kila leo?

Ripoti za umaskini duniani zinaonesha kwamba umaskini umepungua kwa kiasi kikubwa lakini kwa Afrika unaonyesha kuongezeka.Mbaya zaidi maskini wa Afrika wapo kwenye dimbwi zito ambalo si rahisi kujinasua.Utafiti huu unafanywa kulinganisha na nchi za India na China ambazo zina idadi kubwa sana ya watu

Ukipima baadhi ya kauli za hawa tunaowaita wabaguzi utagundua kuna ujumbe wanawasilisha.Ukichukua Tanzania kama mwakilishi wa Afrika utaweza kugundua haya.Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi lakini si nufaishi kwa mwananchi wake isipokuwa wawekezaji wanakuwa na mamlaka makubwa juu ya rasilimali hizi.Kuna mito,Madini na misimu lakini bado tunaagizia dawa kutoka nje.SHAME!!

Watu wanajilundikia mabilioni ya Fedha kwenye akaunti zao za benki zilizopo nchini au hata nje ulaya wakati shule ya AZANIA iliyoko katikati ya jiji kuu la nchi ina wastani wa tundu moja la choo kwa wanafunzi 300

Bado tunazipa likizo ya kodi kampuni kubwa huku tukifuatilia vikodi vidogo vidogo.Kampuni kubwa zinaruhusiwa kubeba hasara na kuipeleka kwenye mahesabu ya mwaka ujao kwa miaka KADHAA lakini hiyo hiyo kampuni inaendelea kufanya biashara.Hapa sisi ni wakusanyaji wazuri wa kodi au wakwepaji wazuri wa makampuni makubwa?

Inafaa tujiulize kunani kwenye akili zetu?Tunasema tuna mafuta lakini tukitaka kuyachimba tunamwita mzungu japokuwa tumekuwa tukizalisha wakandarasi na wanajiorojia kila mwaka.Lazima tujiulize kama elimu yetu ina mushikeli au la!Sasa hivi tunajigamba kuwa na vyuo vikuu 30 lakini bado tunaagizia vijiti vya kuchokonolea meno toka Malaysia. Kweli??

Kabla ya kushika mabango na kuwalaani wabaguzi wa rangi lazima tujiulize kwanza ni wapi tumekosea na sababu za kukwama kwetu.Tusikimbilie kulaumu wazungu kwa kuleta ukoloni na ukoloni mambo leo.Malaysia na Ghana zote zilikuwa koloni za muingereza na zilipata uhuru mwaka 1957 kwa pamoja lakini leo hali ni tofauti.

Wamalaysia walikuwa wanakwenda Ghana kujifunza kilimo cha mawese. Leo hii Ghana wanajifunza kila kitu toka Malaysia kikiwemo kilimo cha mawese.Wazungu wanaopinga kauli za WATSON sio kwamba wanasikitika sana bali wanaonesha kukasirika usoni lakini moyoni wanasema ni kweli hawa wanaujinga wao mkubwa.Wanatutetea ili waendelee kutuvuna.Hawataki tukaechini na kujitathmini tulipoenda mrama.

Nachukia kuitwa kiumbe dhaifu hasa kiakili.Nachukia kwa sababu naupenda uafrika na WEUSI wangu.Nawapenda waafrika wenzangu.Nachukia wanapoambiwa kwamba wanaubongo dhaifu. Lakini nahisi kuna mahali kama watu WEUSI tumekosea

Kama mtu anaiba mabilioni ya fedha za umma kwenye nchi maskini na kuyaweka ulaya au kewekeza mahali popote,huku kukiwa na wananchi wanakufa kwa kukosa madawa hospitalini basi kuna ulazima wa kujiuliza tuliko na kasoro.Kama viongozi wanawaibia wananchi wao waliowachagua kuwawakilisha bila aibu yoyote inabidi tuhoji akili zetu.Kama wananchi wanaridhika na hila za viongozi wao bila ya kuchukua hatua madhubuti basi tuhoji akili zetu

JE? Watson aombe radhi

Hata kama Watson ataomba radhi kama mawaziri wa Japan atakuwa amepeleka ujumbe mzito kwa watu WEUSI kujichunguza.Huu ni ujumbe mzito kwa taifa letu la Tanzania.Mimi ni miongoni mwa wasioamini upuuzi wa James Watson, kwamba waafrika tuna akili ndogo.

Historia inaonyesha kwamba chuo kikuu cha kwanza duniani kilikuwa Afrika,kule Mali.Uvumbuzi wa hisabati ulitoka Afrika,hata mtu wa kwanza duniani anaaminika kuishi Afrika.Pia MAAJABU mengi yapo kule misri (pyramids)

Wapo waliokwenda mbali na kusema kwamba hata YESU KRISTO alikuwa mtu mweusi wa misri na kwamba ndiyo sababu SIMON WA KRENE,ambaye alikuwa mtu mweusi alimsaidia YESU kubeba msalaba.Ilikuwa ni huruma ya kuona mtu mweusi mwezake anateswa.

Jamani ni wapi tumekosea??

Sasa je,ni kweli watu WEUSI tuna akili ndogo??
IMG-20191215-WA0018.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi naamini wote tuna akili sawa; I mean, generally hakuna mwenye akili ndogo wala kubwa kati ya mtu mweusi na mtu mweupe. Isipokuwa nitakubaliana na yule atakaesema sisi watu weusi akili zetu hatuzitumii ipasavyo, kwa uwezo wake unaotakiwa. We don't usually unlock our fully mental capabilities ila akili tunazo sawa tu na whites.

Sasa swali ni kwanini hatuzitumii akili zetu ipasavyo? Ukiniuliza mimi nitakwambia ni matokeo ya kimkakati ya waliotutawala. Walihakikisha wanatubadili kiakili kwanza, once and for all, ndo maana walitumia mbinu za kiimani, kupandikiza hofu. It's all about mind game. Walijua mtu mwenye hofu ni rahisi sana kumpeleka kama unavyotaka.

Ukitaka kuamini kuwa ni mchezo wa akili tu - Chunguza utagundua kuwa South Africans wanajiona bora kuliko mataifa ya nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, North African wanajiona bora kuliko South Africans, Waingereza wanajiona bora kuliko Wamarekani, Wajapan wanajiona bora kuliko Wakorea and the list goes on. Na sababu si kwamba wana akili kubwa... naaaaah... - bali ni maendeleo. Baada ya kutawaliwa kiakili tulishindwa kufanya maendeleo na tunashindwa kufanya maendeleo kwasababu nyingi. Mfano walituletea dini ili tuwe submissive; matokeo yake mpaka leo watu tuko busy na dini ambazo wao waliozileta hawana habari nazo. Wao wako busy viwandani wanaunda magari, sisi tuko busy makanisani tunaomba miujiza ya magari. Wao wako busy na cloud seeding sisi tunaamini mvua inaletwa au kuzuiwa na mwenyezi Mungu.

Sisi mtu ana PhD lakini bado anaenda kwa mganga wa kienyeji ili mambo yake yaende,... tatizo hapo sio akili ndogo bali matumizi ya akili ni madogo. Kama unabisha... tuingie mtaani leo tufanye utafiti ni Watanzania wangapi wanaamini kuwa wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. I am sure, wengi wana ile 'hofu ya Mungu' waliyofundishwa kanisani ambayo sote tunajua inakukataza usizitegemee akili zako. Now, do you expect mtu mwenye imani hii ataitumia akili yake sawasawa? Never.

Kafanye utafiti huo huo kwa whites; kawaulize kama wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. You'll be surprised brother.

Kwa hiyo, hii notion itabadilika siku tuki-catch up to their speed of development. Otherwise sisi wenyewe tutaendelea kujidharau hata kabla wao hawajatudharau. Jiulize, kwanini kila kitu kinachoonekana ni bora tunakiita 'cha kizungu' - yaani mpaka kuna panzi wa kizungu eti... seriously?!!!!???

Tuache woga, tutumie akili zetu sawa sawa. It is "THINK AND GROW RICH"... sijawahi sikia "BELIEVE AND GROW RICH" au "PRAY AND GROW RICH". Sisemi watu wasisali au kuamini, ila ni vyema tukatumia akili zetu hata katika imani pia.

They are not born better than us, but they use their minds to the max to become better than us. So it's NURTURE not NATURE.
 
Kwanza kabisa binaadamu wote tumewekewa ubongo sawa, nikimaanisha kua kilakitu nilichonacho kwenye ubongo wangu basi nawewe unacho na mwanasayansi Leonardo da vinci alikua nacho.

Sasa kwanini inaonekana da vinci alikua na akili kuuubwa kuliko wengine? kinachotutofautisha ni jinsi ubongo wetu tunavyoutumia katika kufikiria, pia vipaumbele vya matumizi ya ubongo wetu. Lakin kuuubwa zaidi tulilotofautiana na mwanasayansi da vinci ni kujaliwa karama/vipaji vingii katika uwezo wa hali ya juu, na hapo ndipo alipotupiga bao da vinci.

(aliitumia akili yake vizuri pia alijaliwa karama nyiingi) leo hii mimi nawewe tunaweza kufuata nyendo za da vinci tukamfikia na kumpita mbali kabisa mfano Arristotle alimuona Plato ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu na kweli plato alikua na akili kuubwa sana ila mwanafunzi wake arristotle aliweka commitment hadi akamshinda mwalimu wake plato uwezo.
 
Mtoa mada nimemuelewa sanaa.

Ila hata mimi nilisha wahi post ishu ndogo tuu kipindi mwendo kasi zinazinduliwa na kutumika.

Nikasema kuwa zile campuni zilizo jenga mwendo kasi zilishirikiana na ma injinia wetu.
Je tukitaka kujenga mwendo kasi tena Dodoma na mikoa mingine tutaitaji kichukua injinia kutoka nje..? Lihali kila tunaweza nunua mashine baadhi ambazo hatuna na kwenda kujenga sehemu nyingine.

Lakini sio tuu mwendo kasi
Mataifa yanayo endelea yana mfumo wa kubadilishana teknologia na resoses za nchi. Kwamba sio kila mkataba basi tulipwe dola. Tumaweza baadhi ya mikataba tukawapeleka wasomi wetu nje kwa wingi kwa ajili ya kupata technology mpya zinazo toka kila siku.

Inachosha mpaka leo hii syllabus ya Physics bado haitofautiani na sana na urithi kutoka kwa wakoloni wetu.Wakati Dunia ishabadilika sehem kubwa.

Kikubwa zaidi hata ukitoa dini. Mfumo mkubwa wa utawala una simamia sana kutoka kwa wakoloni.

Siwezi sema tuna baguliwa bali tuna jibagua wenyewe.

Unakuta tunaanzisha vyuo vingi sana mtaani ambavyo vinaenda kuwa mti majungu kwa vijana wengi.Nawakati tunaweza Jenga chuo kimoja clasic kwa ajili ya watu ambao wapo seriously na kusoma kwa ajili ya maendeleo kwa watu.
Wale wengine msio weza kusoma wenzangu na mimi tuna piga kazi kwa kufata akili za wale wenzetu wachache wasomi na kujikomboa wenyewe.

Lakini mwanaume na nguvu zake anafanya biashara ndogo ya mtaji mdogo miaka yote huku tunaitaji watu wa kichimba wakulima mashamba makibwa ya materials na wakuendeshea viwanda.

Wakati mwengine tunabembelezana sana na mwisho we tunaweza hata sababisha umaskini kwa kuoneana uruma.

Mi huwa roho inaniuma sana kama mtu anapoteza miaka yake kwa kusoma mpaka kufukia Degree alafu anaishia pabaya kwa kukosa maarifa kazi za kujiajiri na kutokuwa mbunifu wa kusoma alama na code za nyakati huwa inanipa wakati mgumu sana.

Sisi tunapenda sana mapenzi ngono.Ndio vitu ambavyo wengi vinatudumaza kimawazo.ukiendekeza ngono sana lazima upeo wako wa akili ushuke maana mwili utatumia nguvu nyingi sana kutawala tendo lile na kuacha kufikiria maisha.

Waafrica tuna safari ndefu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza lazima ujue hao wadadisi walikua wanapima akili kwa kutumia vigezo gani? Mathalani vitu kama utambuzi, ugunduzi, usimamizi wa uchumi, usimamizi wa mazingira, maenendeleo ya technology na nguvu za kijeshi pengine ni vitu ambavyo watu weusi tuko nyuma.

Ila ukifikiria nje ya box, unaweza ukajiuliza maisha ya mwanadamu ni nini?na thamani ya vitu hivyo vyote nilivyovitaja hapo juu ikiwa mwanadamu atakufa na kuingia kaburini pengine na sanda tu kama watakao kuzika wakikuheshimu.

Hivyo basi, mapambano ya maisha na namna ya kuishi inaweza ikawa ni ya furaha au ya shida ikiwa unapambana ili uishi kama hautakufa au ukiishi ukijua utakufa lakini ukafurahi mema kidogo ya dunia hii.

Mababu zetu walilitambua hili, wakarahisisha mahitaji yako, wakaishi kwa furaha, wakiwa wanafanya kazi na bata. Hivyo bado nina amini mtu mweusi ana akili zaidi kwasababu anaishi kiasili na kufurahi maisha tofauti na hao wenzetu ambao maisha yao yamechukuliwa na mifumo ambayo ni complex yenye kuwaletea stress ili hali wanakufa nakuzikwa bila kuondoka na kitu chochote duniani.

Kwa kuanzia naomba niwasilishe hii dhana yangu kwa ufupi ila nita expand siku za usoni
 
Nimekuelewa Chief
Binafsi naamini wote tuna akili sawa; I mean, generally hakuna mwenye akili ndogo wala kubwa kati ya mtu mweusi na mtu mweupe. Isipokuwa nitakubaliana na yule atakaesema sisi watu weusi akili zetu hatuzitumii ipasavyo, kwa uwezo wake unaotakiwa. We don't usually unlock our fully mental capabilities ila akili tunazo sawa tu na whites.

Sasa swali ni kwanini hatuzitumii akili zetu ipasavyo? Ukiniuliza mimi nitakwambia ni matokeo ya kimkakati ya waliotutawala. Walihakikisha wanatubadili kiakili kwanza, once and for all, ndo maana walitumia mbinu za kiimani, kupandikiza hofu. It's all about mind game. Walijua mtu mwenye hofu ni rahisi sana kumpeleka kama unavyotaka.

Ukitaka kuamini kuwa ni mchezo wa akili tu - Chunguza utagundua kuwa South Africans wanajiona bora kuliko mataifa ya nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, North African wanajiona bora kuliko South Africans, Waingereza wanajiona bora kuliko Wamarekani, Wajapan wanajiona bora kuliko Wakorea and the list goes on. Na sababu si kwamba wana akili kubwa... naaaaah... - bali ni maendeleo. Baada ya kutawaliwa kiakili tulishindwa kufanya maendeleo na tunashindwa kufanya maendeleo kwasababu nyingi. Mfano walituletea dini ili tuwe submissive; matokeo yake mpaka leo watu tuko busy na dini ambazo wao waliozileta hawana habari nazo. Wao wako busy viwandani wanaunda magari, sisi tuko busy makanisani tunaomba miujiza ya magari. Wao wako busy na cloud seeding sisi tunaamini mvua inaletwa au kuzuiwa na mwenyezi Mungu.

Sisi mtu ana PhD lakini bado anaenda kwa mganga wa kienyeji ili mambo yake yaende,... tatizo hapo sio akili ndogo bali matumizi ya akili ni madogo. Kama unabisha... tuingie mtaani leo tufanye utafiti ni Watanzania wangapi wanaamini kuwa wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. I am sure, wengi wana ile 'hofu ya Mungu' waliyofundishwa kanisani ambayo sote tunajua inakukataza usizitegemee akili zako. Now, do you expect mtu mwenye imani hii ataitumia akili yake sawasawa? Never.

Kafanye utafiti huo huo kwa whites; kawaulize kama wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. You'll be surprised brother.

Kwa hiyo, hii notion itabadilika siku tuki-catch up to their speed of development. Otherwise sisi wenyewe tutaendelea kujidharau hata kabla wao hawajatudharau. Jiulize, kwanini kila kitu kinachoonekana ni bora tunakiita 'cha kizungu' - yaani mpaka kuna panzi wa kizungu eti... seriously?!!!!???

Tuache woga, tutumie akili zetu sawa sawa. It is "THINK AND GROW RICH"... sijawahi sikia "BELIEVE AND GROW RICH" au "PRAY AND GROW RICH". Sisemi watu wasisali au kuamini, ila ni vyema tukatumia akili zetu hata katika imani pia.

They are not born better than us, but they use their minds to the max to become better than us. So it's NURTURE not NATURE.
Crucial Points to note...We Move

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza lazima ujue hao wadadisi walikua wanapima akili kwa kutumia vigezo gani? Mathalani vitu kama utambuzi, ugunduzi, usimamizi wa uchumi, usimamizi wa mazingira, maenendeleo ya technology na nguvu za kijeshi pengine ni vitu ambavyo watu weusi tuko nyuma.

Ila ukifikiria nje ya box, unaweza ukajiuliza maisha ya mwanadamu ni nini?na thamani ya vitu hivyo vyote nilivyovitaja hapo juu ikiwa mwanadamu atakufa na kuingia kaburini pengine na sanda tu kama watakao kuzika wakikuheshimu.

Hivyo basi, mapambano ya maisha na namna ya kuishi inaweza ikawa ni ya furaha au ya shida ikiwa unapambana ili uishi kama hautakufa au ukiishi ukijua utakufa lakini ukafurahi mema kidogo ya dunia hii.

Mababu zetu walilitambua hili, wakarahisisha mahitaji yako, wakaishi kwa furaha, wakiwa wanafanya kazi na bata. Hivyo bado nina amini mtu mweusi ana akili zaidi kwasababu anaishi kiasili na kufurahi maisha tofauti na hao wenzetu ambao maisha yao yamechukuliwa na mifumo ambayo ni complex yenye kuwaletea stress ili hali wanakufa nakuzikwa bila kuondoka na kitu chochote duniani.

Kwa kuanzia naomba niwasilishe hii dhana yangu kwa ufupi ila nita expand siku za usoni
Hongera pia...nasubiri kwa upanaa zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza lazima ujue hao wadadisi walikua wanapima akili kwa kutumia vigezo gani? Mathalani vitu kama utambuzi, ugunduzi, usimamizi wa uchumi, usimamizi wa mazingira, maenendeleo ya technology na nguvu za kijeshi pengine ni vitu ambavyo watu weusi tuko nyuma.

Ila ukifikiria nje ya box, unaweza ukajiuliza maisha ya mwanadamu ni nini?na thamani ya vitu hivyo vyote nilivyovitaja hapo juu ikiwa mwanadamu atakufa na kuingia kaburini pengine na sanda tu kama watakao kuzika wakikuheshimu.

Hivyo basi, mapambano ya maisha na namna ya kuishi inaweza ikawa ni ya furaha au ya shida ikiwa unapambana ili uishi kama hautakufa au ukiishi ukijua utakufa lakini ukafurahi mema kidogo ya dunia hii.

Mababu zetu walilitambua hili, wakarahisisha mahitaji yako, wakaishi kwa furaha, wakiwa wanafanya kazi na bata. Hivyo bado nina amini mtu mweusi ana akili zaidi kwasababu anaishi kiasili na kufurahi maisha tofauti na hao wenzetu ambao maisha yao yamechukuliwa na mifumo ambayo ni complex yenye kuwaletea stress ili hali wanakufa nakuzikwa bila kuondoka na kitu chochote duniani.

Kwa kuanzia naomba niwasilishe hii dhana yangu kwa ufupi ila nita expand siku za usoni
Mkuu kwa hiyo unataka kusema kwamba sisi tumeamua kuishi bila kuwa na uhitaji katika hayo mambo (ugunduzi, usimamizi wa uchumi, uvumbuzi, nguvu za kijeshi, usimamimizi wa mazingira n.k.)?

Bila shaka jibu litakuwa hapana kwa sababu..

tumeona jinsi gani nguvu za kijeshi tumekuwa tukizihitaji hasa pale tunapo kutana na adui ambae sio wa mazingira ya kwetu huwa tunanyanyasika sana (ref jinsi walivyo mzingua canal muamar gadafi)

nguvu ya ugunduzi au uvumbuzi nayo inahitajika kwa kiasi kikubwa sana kwa sababu tumeona jinsi gan watu wa magharibi wanaitufanya miili yetu kama speciemen za kujaribu magonjwa na tiba mbalimbali kwa hiyo bila kuwa na wachunguzi walio bobea tutateseka mpaka pumzi yetu ya mwisho mkuu

Nguvu ya uchumi nayo inahitajika kwa sababu kama tulivyo dhoofu kwenye hii sekta ndio sababu inayo pelekea mpaka tunapangiwa hata bajeti zetu (indirect way), tunapangiwa sheria kwamba fanyeni hiki hiki hakifai, chukueni vyandarua tupeni dhahabu n.k

Nguvu ya kiutawala au kisiasa nazani ndio janga kubwa linalo takiwa kufanyiwa maboresho hapa kwetu maana kila uchwao Africa tunauana wenyew kw wenyewe kwa ajili ya tamaa za madaraka na bora ingekuwa taifa moja na taifa lingine labda tungesema wanatafuta kutanua mipaka, la hasha hii inatokea kwa watu wa taifa moja yan Africa ni marufuku kuwa na mawazo tofauti au mpinzani basi ujue utakufa, kiufupi bado hatuna sera za utawala bora ndio maana ni rahisi sana kwa watu weupe kupandikiza chuki na kutengeneza maadui wa ndani kwa ndani.

Naomba niishie hapa mkuu na kuhitimisha kwamba tusiseme hatutaki hivyo vitu hapa juu na tuchague kuishi kama watu wa zama za mawe kwa kisingizio kwamba sio sehem ya furaha zetu wakati tunajua fika tunanyanyaswa tunatukanwa na kudharaulika dunian kwa ajili ya hivyo vitu hapo tutakuwa tunadanganya mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa hiyo unataka kusema kwamba sisi tumeamua kuishi bila kuwa na uhitaji katika hayo mambo (ugunduzi, usimamizi wa uchumi, uvumbuzi, nguvu za kijeshi, usimamimizi wa mazingira n.k.)?

Bila shaka jibu litakuwa hapana kwa sababu..

tumeona jinsi gani nguvu za kijeshi tumekuwa tukizihitaji hasa pale tunapo kutana na adui ambae sio wa mazingira ya kwetu huwa tunanyanyasika sana (ref jinsi walivyo mzingua canal muamar gadafi)

nguvu ya ugunduzi au uvumbuzi nayo inahitajika kwa kiasi kikubwa sana kwa sababu tumeona jinsi gan watu wa magharibi wanaitufanya miili yetu kama speciemen za kujaribu magonjwa na tiba mbalimbali kwa hiyo bila kuwa na wachunguzi walio bobea tutateseka mpaka pumzi yetu ya mwisho mkuu

Nguvu ya uchumi nayo inahitajika kwa sababu kama tulivyo dhoofu kwenye hii sekta ndio sababu inayo pelekea mpaka tunapangiwa hata bajeti zetu (indirect way), tunapangiwa sheria kwamba fanyeni hiki hiki hakifai, chukueni vyandarua tupeni dhahabu n.k

Nguvu ya kiutawala au kisiasa nazani ndio janga kubwa linalo takiwa kufanyiwa maboresho hapa kwetu maana kila uchwao Africa tunauana wenyew kw wenyewe kwa ajili ya tamaa za madaraka na bora ingekuwa taifa moja na taifa lingine labda tungesema wanatafuta kutanua mipaka, la hasha hii inatokea kwa watu wa taifa moja yan Africa ni marufuku kuwa na mawazo tofauti au mpinzani basi ujue utakufa, kiufupi bado hatuna sera za utawala bora ndio maana ni rahisi sana kwa watu weupe kupandikiza chuki na kutengeneza maadui wa ndani kwa ndani.

Naomba niishie hapa mkuu na kuhitimisha kwamba tusiseme hatutaki hivyo vitu hapa juu na tuchague kuishi kama watu wa zama za mawe kwa kisingizio kwamba sio sehem ya furaha zetu wakati tunajua fika tunanyanyaswa tunatukanwa na kudharaulika dunian kwa ajili ya hivyo vitu hapo tutakuwa tunadanganya mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakubaliana na hoja yako kwa kuwa hayo yote kama nilivyoyaainisha ndiyo mambo ambayo yanatutofautisha sisi na watu weupe, hii ni kwasababu mfumo wa maisha yao ndiyo ulivyojengwa na ndiyo wanavyoamini baada ya kupitia mambo mengi huko kwao.

Msingi wa hoja yangu ni kwamba je huu ndiyo mfumo sahihi wa maisha ya mwanadamu na hakuna mfumo mwingine unaoweza kuleta haki na furaha kwa wanadamu.

Kwa watu wa imani watauliza je ulikua ni mpango wa Mungu kumfanya mwanadamu aishi kwenye hizi tafrani zote zinazoletwa na watu weupe?

Mimi bado naamini watu weusi ni wenye akili zaidi kwani wanajua maana halisi ya maisha na nini kinatakiwa kifanywe maishani.
 
Binafsi naamini wote tuna akili sawa; I mean, generally hakuna mwenye akili ndogo wala kubwa kati ya mtu mweusi na mtu mweupe. Isipokuwa nitakubaliana na yule atakaesema sisi watu weusi akili zetu hatuzitumii ipasavyo, kwa uwezo wake unaotakiwa. We don't usually unlock our fully mental capabilities ila akili tunazo sawa tu na whites.

Sasa swali ni kwanini hatuzitumii akili zetu ipasavyo? Ukiniuliza mimi nitakwambia ni matokeo ya kimkakati ya waliotutawala. Walihakikisha wanatubadili kiakili kwanza, once and for all, ndo maana walitumia mbinu za kiimani, kupandikiza hofu. It's all about mind game. Walijua mtu mwenye hofu ni rahisi sana kumpeleka kama unavyotaka.

Ukitaka kuamini kuwa ni mchezo wa akili tu - Chunguza utagundua kuwa South Africans wanajiona bora kuliko mataifa ya nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, North African wanajiona bora kuliko South Africans, Waingereza wanajiona bora kuliko Wamarekani, Wajapan wanajiona bora kuliko Wakorea and the list goes on. Na sababu si kwamba wana akili kubwa... naaaaah... - bali ni maendeleo. Baada ya kutawaliwa kiakili tulishindwa kufanya maendeleo na tunashindwa kufanya maendeleo kwasababu nyingi. Mfano walituletea dini ili tuwe submissive; matokeo yake mpaka leo watu tuko busy na dini ambazo wao waliozileta hawana habari nazo. Wao wako busy viwandani wanaunda magari, sisi tuko busy makanisani tunaomba miujiza ya magari. Wao wako busy na cloud seeding sisi tunaamini mvua inaletwa au kuzuiwa na mwenyezi Mungu.

Sisi mtu ana PhD lakini bado anaenda kwa mganga wa kienyeji ili mambo yake yaende,... tatizo hapo sio akili ndogo bali matumizi ya akili ni madogo. Kama unabisha... tuingie mtaani leo tufanye utafiti ni Watanzania wangapi wanaamini kuwa wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. I am sure, wengi wana ile 'hofu ya Mungu' waliyofundishwa kanisani ambayo sote tunajua inakukataza usizitegemee akili zako. Now, do you expect mtu mwenye imani hii ataitumia akili yake sawasawa? Never.

Kafanye utafiti huo huo kwa whites; kawaulize kama wanaweza kutegemea akili zao kwa 100% pasipo kutegemea kitu kingine chochote katika kufanikisha mambo yao. You'll be surprised brother.

Kwa hiyo, hii notion itabadilika siku tuki-catch up to their speed of development. Otherwise sisi wenyewe tutaendelea kujidharau hata kabla wao hawajatudharau. Jiulize, kwanini kila kitu kinachoonekana ni bora tunakiita 'cha kizungu' - yaani mpaka kuna panzi wa kizungu eti... seriously?!!!!???

Tuache woga, tutumie akili zetu sawa sawa. It is "THINK AND GROW RICH"... sijawahi sikia "BELIEVE AND GROW RICH" au "PRAY AND GROW RICH". Sisemi watu wasisali au kuamini, ila ni vyema tukatumia akili zetu hata katika imani pia.

They are not born better than us, but they use their minds to the max to become better than us. So it's NURTURE not NATURE.
Kutotumia akili ipasavyo ni ukosefu wa akili.
 
Sasa mkuu unahitaji nini kujua kuwa waafrika hatupo sawa kiakili na wazungu..?
Mbona vitu ni dhahiri kabisa!,Kama tunapigana kwa dini na ukabila unafikiri zinatosheleza kichwani..?
Sisi tunajua uchawi tu na pamoja na uchawi huo bado rangi nyeupe inatupiga bao!!
Teknolojia kubwa inatoka kwa went rangi nyeupe! Unataka uambiwe kitu gani ili ujue kuwa tupo chini..?
Takwimu tu zinaonyesha kuwa tupo chini kiutendaji,kiimani,kifikra na kiteknolojia pia! Hata shuka malaika kuja kukuambia hilo.. na huenda ukishindwa kuliona hili basi jua tu unadhihirisha tu kuwa waafrika tuna peo ndogo zaidi!

Alasivyo tujitetee kwa kutafuta mfumo wetu wa maisha! Tusiige mifumo ya kizungu, huenda inatushinda.. sisi sio watu wa teknolojia labda!,viwanda navyo hapana no business,no electricity tutumie Moto tu unatutosha!.
Huenda tunatembea ktk mifumo tusioiweza na kushindwa kwetu na matokeo yake! Ni kama vile unamlazimisha mtu fulani kuishi aina fulani ya maisha ila ndo vile sasa anaenda ki utwana! Ukimuuliza upo amakujibu NIPO!! Anakujibu huku kachoka kachakaa!.
 
Nakubaliana na hoja yako kwa kuwa hayo yote kama nilivyoyaainisha ndiyo mambo ambayo yanatutofautisha sisi na watu weupe, hii ni kwasababu mfumo wa maisha yao ndiyo ulivyojengwa na ndiyo wanavyoamini baada ya kupitia mambo mengi huko kwao.

Msingi wa hoja yangu ni kwamba je huu ndiyo mfumo sahihi wa maisha ya mwanadamu na hakuna mfumo mwingine unaoweza kuleta haki na furaha kwa wanadamu.

Kwa watu wa imani watauliza je ulikua ni mpango wa Mungu kumfanya mwanadamu aishi kwenye hizi tafrani zote zinazoletwa na watu weupe?

Mimi bado naamini watu weusi ni wenye akili zaidi kwani wanajua maana halisi ya maisha na nini kinatakiwa kifanywe maishani.
Watu weusi wangekuwa wanajua maana halisi ya maisha wasingekuwa wanakufa kwa kukosa chakula ambayo ni basic needs ya kila mwanadamu kama kungekuwa na mashindano ya ngono mweusi ata shinda
 
Watu weusi wangekuwa wanajua maana halisi ya maisha wasingekuwa wanakufa kwa kukosa chakula ambayo ni basic needs ya kila mwanadamu kama kungekuwa na mashindano ya ngono mweusi ata shinda
Mkuu wanakufa kwa njaa kwasababu mashamba yao yalichukuliwa na wakoloni, hivyo hawana ardhi ya kulima, fuatilia vizuri
 
Back
Top Bottom