Je, ni halali bei ya nauli ya SGR kupanda kila mara?

Je, ni halali bei ya nauli ya SGR kupanda kila mara?

Ngurumbizi

Member
Joined
Aug 8, 2011
Posts
97
Reaction score
114
Nauli kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro yapanda kimya kimya kutoka Sh 13,000 hadi Sh 13,500 – licha ya kutumia umeme badala ya mafuta

Soma Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba anawasilisha Bajeti Kuu ya Serikali 2025/2026

Sehemu ya hotuba ya bajeti kuu ya serikali 2025/2026.
"Kutoza shilingi 500 kwa kila tiketi inayotolewana mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya treni."
"Kutoza shilingi 1000 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya anga. Hatua hizi kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 586,404.9.

Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali.

Ikumbukwe kuwa moja ya hoja kuu ya ujenzi wa reli ya kisasa ilikuwa ni kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutumia treni za umeme, ambazo ni rafiki kwa mazingira na nafuu zaidi kwa uendeshaji ukilinganisha na treni au mabasi yanayotumia mafuta. Kwa hiyo, ikiwa gharama za mafuta duniani zimepanda, hiyo haiwezi kuwa sababu ya moja kwa moja kwa SGR, kwani injini zake hazitegemei dizeli wala petroli.

Katika mazingira hayo, swali linabaki: Kwanini nauli inapanda? Na kama kweli umeme ndio sababu, je, kuna ongezeko la bei ya umeme kwa kiwango hicho kikubwa kiasi cha kuathiri nauli? Tanesco haijatangaza mabadiliko makubwa ya bei kwa wateja wa viwandani kama TRC.

Wananchi wana haki ya kuelewa vigezo vinavyotumika. Je, TRC imeongeza ubora wa huduma? Imepunguza muda wa safari? Imeongeza mabehewa? Kama hakuna mabadiliko yoyote ya kiutendaji au huduma, basi ongezeko hili linaweza kutafsiriwa kama mzigo wa kimyakimya kwa wananchi wa kawaida.

Kwa kuzingatia kwamba SGR ni mradi mkubwa wa kimkakati, uliogharimu mabilioni ya fedha za mkopo na kodi ya wananchi, haipaswi kuwa chanzo cha faida kwa bei ya juu, bali suluhisho la usafiri nafuu. Uhalali wa kuongeza nauli unapaswa kuambatana na:

Uwazi wa gharama za uendeshaji

Ushirikishwaji wa wadau, hususan abiria

Taarifa rasmi kwa umma kabla ya mabadiliko


Je, kuna mamlaka huru inayodhibiti viwango vya nauli ya SGR, kama ilivyo EWURA kwa mafuta au LATRA kwa mabasi? Au TRC inaamua yenyewe na kutekeleza?

Kupanda kwa bei kimya kimya huku kukitumia umeme kama chanzo cha nishati kunaashiria uwepo wa sintofahamu katika mfumo mzima wa upangaji wa bei. Hali hii si tu inaleta kero kwa wasafiri, bali pia inapunguza imani ya umma kwa taasisi zinazohusika.

Wakati wananchi wanapongeza kasi, usalama na unafuu wa SGR, ni muhimu pia kuweka bayana kuwa huduma bora haimaanishi lazima iwe ya gharama kubwa, hasa kwa miundombinu inayotegemea nishati nafuu kama umeme.

Tunahitaji majibu. Tunahitaji mjadala wa wazi. Tunahitaji uwazi.
SGR ni mali ya Watanzania wote – nauli yake pia ni suala la umma.
 
Wakati wa wasilisho la bajeti ya mwaka wa fedha wa serikali 2025/2026 taarifa ya ongezeko la tsh 500 ama 1000 kwenye ticket za usafiri wa SGR / Ndege lilitolewa
 
Kipindi bajeti inapitishwa ulikuwa wapi izo tozo zimeogezeka had kwa wasafiri wa ndege wao wameongezwa 1000

Lipa Kodi kwa maendeleo ya nchi yako
 
Nauli itapandishwa mpaka pale watakapoona wengi hawawezi kulipa, hiyo ndio kanuni ya price, demand and supply.
 
Nauli kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro yapanda kimya kimya kutoka Sh 13,000 hadi Sh 13,500 – licha ya kutumia umeme badala ya mafuta

Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali.

Ikumbukwe kuwa moja ya hoja kuu ya ujenzi wa reli ya kisasa ilikuwa ni kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutumia treni za umeme, ambazo ni rafiki kwa mazingira na nafuu zaidi kwa uendeshaji ukilinganisha na treni au mabasi yanayotumia mafuta. Kwa hiyo, ikiwa gharama za mafuta duniani zimepanda, hiyo haiwezi kuwa sababu ya moja kwa moja kwa SGR, kwani injini zake hazitegemei dizeli wala petroli.

Katika mazingira hayo, swali linabaki: Kwanini nauli inapanda? Na kama kweli umeme ndio sababu, je, kuna ongezeko la bei ya umeme kwa kiwango hicho kikubwa kiasi cha kuathiri nauli? Tanesco haijatangaza mabadiliko makubwa ya bei kwa wateja wa viwandani kama TRC.

Wananchi wana haki ya kuelewa vigezo vinavyotumika. Je, TRC imeongeza ubora wa huduma? Imepunguza muda wa safari? Imeongeza mabehewa? Kama hakuna mabadiliko yoyote ya kiutendaji au huduma, basi ongezeko hili linaweza kutafsiriwa kama mzigo wa kimyakimya kwa wananchi wa kawaida.

Kwa kuzingatia kwamba SGR ni mradi mkubwa wa kimkakati, uliogharimu mabilioni ya fedha za mkopo na kodi ya wananchi, haipaswi kuwa chanzo cha faida kwa bei ya juu, bali suluhisho la usafiri nafuu. Uhalali wa kuongeza nauli unapaswa kuambatana na:

Uwazi wa gharama za uendeshaji

Ushirikishwaji wa wadau, hususan abiria

Taarifa rasmi kwa umma kabla ya mabadiliko


Je, kuna mamlaka huru inayodhibiti viwango vya nauli ya SGR, kama ilivyo EWURA kwa mafuta au LATRA kwa mabasi? Au TRC inaamua yenyewe na kutekeleza?

Kupanda kwa bei kimya kimya huku kukitumia umeme kama chanzo cha nishati kunaashiria uwepo wa sintofahamu katika mfumo mzima wa upangaji wa bei. Hali hii si tu inaleta kero kwa wasafiri, bali pia inapunguza imani ya umma kwa taasisi zinazohusika.

Wakati wananchi wanapongeza kasi, usalama na unafuu wa SGR, ni muhimu pia kuweka bayana kuwa huduma bora haimaanishi lazima iwe ya gharama kubwa, hasa kwa miundombinu inayotegemea nishati nafuu kama umeme.

Tunahitaji majibu. Tunahitaji mjadala wa wazi. Tunahitaji uwazi.
SGR ni mali ya Watanzania wote – nauli yake pia ni suala la umma.
Huo ni mwanzo tu.. Nawapa miaka mitatu mtaona maajabu
 
Nauli kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro yapanda kimya kimya kutoka Sh 13,000 hadi Sh 13,500 – licha ya kutumia umeme badala ya mafuta

Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali.

Ikumbukwe kuwa moja ya hoja kuu ya ujenzi wa reli ya kisasa ilikuwa ni kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutumia treni za umeme, ambazo ni rafiki kwa mazingira na nafuu zaidi kwa uendeshaji ukilinganisha na treni au mabasi yanayotumia mafuta. Kwa hiyo, ikiwa gharama za mafuta duniani zimepanda, hiyo haiwezi kuwa sababu ya moja kwa moja kwa SGR, kwani injini zake hazitegemei dizeli wala petroli.

Katika mazingira hayo, swali linabaki: Kwanini nauli inapanda? Na kama kweli umeme ndio sababu, je, kuna ongezeko la bei ya umeme kwa kiwango hicho kikubwa kiasi cha kuathiri nauli? Tanesco haijatangaza mabadiliko makubwa ya bei kwa wateja wa viwandani kama TRC.

Wananchi wana haki ya kuelewa vigezo vinavyotumika. Je, TRC imeongeza ubora wa huduma? Imepunguza muda wa safari? Imeongeza mabehewa? Kama hakuna mabadiliko yoyote ya kiutendaji au huduma, basi ongezeko hili linaweza kutafsiriwa kama mzigo wa kimyakimya kwa wananchi wa kawaida.

Kwa kuzingatia kwamba SGR ni mradi mkubwa wa kimkakati, uliogharimu mabilioni ya fedha za mkopo na kodi ya wananchi, haipaswi kuwa chanzo cha faida kwa bei ya juu, bali suluhisho la usafiri nafuu. Uhalali wa kuongeza nauli unapaswa kuambatana na:

Uwazi wa gharama za uendeshaji

Ushirikishwaji wa wadau, hususan abiria

Taarifa rasmi kwa umma kabla ya mabadiliko


Je, kuna mamlaka huru inayodhibiti viwango vya nauli ya SGR, kama ilivyo EWURA kwa mafuta au LATRA kwa mabasi? Au TRC inaamua yenyewe na kutekeleza?

Kupanda kwa bei kimya kimya huku kukitumia umeme kama chanzo cha nishati kunaashiria uwepo wa sintofahamu katika mfumo mzima wa upangaji wa bei. Hali hii si tu inaleta kero kwa wasafiri, bali pia inapunguza imani ya umma kwa taasisi zinazohusika.

Wakati wananchi wanapongeza kasi, usalama na unafuu wa SGR, ni muhimu pia kuweka bayana kuwa huduma bora haimaanishi lazima iwe ya gharama kubwa, hasa kwa miundombinu inayotegemea nishati nafuu kama umeme.

Tunahitaji majibu. Tunahitaji mjadala wa wazi. Tunahitaji uwazi.
SGR ni mali ya Watanzania wote – nauli yake pia ni suala la umma.
Wakati Miswada ya fedha Mwigulu anasoma bungeni, mlikuwa busy na VISUNGURA.

Kenya wanapoandamana kwasababu ya FINANCIAL BILL mnadhani wajinga.

Anyway, hiyo 500 imeongezwa kwenye Tiketi za SGR, na 1,000 kwenye tiketi za Ndege kusaidia Afya maana TRUMP amekata MISAADA.

Hivyo ni jambo jema tu, na wala siyo kwamba limekuja kimya kimya.

Shida hamfuatilii bunge la budget wala mambo ya msingi.
 
Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali
Watakuambia hata daraja la Kigamboni linapandishwa nauli
 
Nauli kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro yapanda kimya kimya kutoka Sh 13,000 hadi Sh 13,500 – licha ya kutumia umeme badala ya mafuta

Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali.

Ikumbukwe kuwa moja ya hoja kuu ya ujenzi wa reli ya kisasa ilikuwa ni kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutumia treni za umeme, ambazo ni rafiki kwa mazingira na nafuu zaidi kwa uendeshaji ukilinganisha na treni au mabasi yanayotumia mafuta. Kwa hiyo, ikiwa gharama za mafuta duniani zimepanda, hiyo haiwezi kuwa sababu ya moja kwa moja kwa SGR, kwani injini zake hazitegemei dizeli wala petroli.

Katika mazingira hayo, swali linabaki: Kwanini nauli inapanda? Na kama kweli umeme ndio sababu, je, kuna ongezeko la bei ya umeme kwa kiwango hicho kikubwa kiasi cha kuathiri nauli? Tanesco haijatangaza mabadiliko makubwa ya bei kwa wateja wa viwandani kama TRC.

Wananchi wana haki ya kuelewa vigezo vinavyotumika. Je, TRC imeongeza ubora wa huduma? Imepunguza muda wa safari? Imeongeza mabehewa? Kama hakuna mabadiliko yoyote ya kiutendaji au huduma, basi ongezeko hili linaweza kutafsiriwa kama mzigo wa kimyakimya kwa wananchi wa kawaida.

Kwa kuzingatia kwamba SGR ni mradi mkubwa wa kimkakati, uliogharimu mabilioni ya fedha za mkopo na kodi ya wananchi, haipaswi kuwa chanzo cha faida kwa bei ya juu, bali suluhisho la usafiri nafuu. Uhalali wa kuongeza nauli unapaswa kuambatana na:

Uwazi wa gharama za uendeshaji

Ushirikishwaji wa wadau, hususan abiria

Taarifa rasmi kwa umma kabla ya mabadiliko


Je, kuna mamlaka huru inayodhibiti viwango vya nauli ya SGR, kama ilivyo EWURA kwa mafuta au LATRA kwa mabasi? Au TRC inaamua yenyewe na kutekeleza?

Kupanda kwa bei kimya kimya huku kukitumia umeme kama chanzo cha nishati kunaashiria uwepo wa sintofahamu katika mfumo mzima wa upangaji wa bei. Hali hii si tu inaleta kero kwa wasafiri, bali pia inapunguza imani ya umma kwa taasisi zinazohusika.

Wakati wananchi wanapongeza kasi, usalama na unafuu wa SGR, ni muhimu pia kuweka bayana kuwa huduma bora haimaanishi lazima iwe ya gharama kubwa, hasa kwa miundombinu inayotegemea nishati nafuu kama umeme.

Tunahitaji majibu. Tunahitaji mjadala wa wazi. Tunahitaji uwazi.
SGR ni mali ya Watanzania wote – nauli yake pia ni suala la umma.
Ni muhimu kufahamu kwamba nauli ya TZS 13,500 kwa safari ya SGR kutoka Dar hadi Moro umbali wa takribani kilomita 200 haipaswi kuangaliwa kwa jicho la gharama za mafuta pekee bali kwa muktadha mpana wa huduma inayotolewa, uendelevu wa mradi na mifano ya kimataifa.
1. Uendeshaji wa SGR unahitaji fedha kubwa:
Ni kweli kuwa gharama za kuendesha treni ya kisasa ya umeme kama SGR ni kubwa. Zinajumuisha mishahara ya watumishi, matengenezo ya mabehewa na reli, gharama za nishati (umeme), usalama wa abiria na mifumo ya udhibiti wa kidijitali. Haya yote yanahitaji fedha za uhakika kila siku.

2. Ruzuku na sekta binafsi
Hivi sasa, serikali ndiyo inayochukua mzigo mkubwa wa awali wa uwekezaji kwenye miundombinu. Hata hivyo, endapo huduma hii ingeachiwa sekta binafsi moja kwa moja bila ruzuku yoyote, kuna uwezekano mkubwa nauli ingekuwa juu zaidi kutokana na azma ya sekta binafsi kutafuta faida ya haraka. Mifumo ya usafiri kama SGR huwa ni ya kimkakati – hivyo siyo rahisi kuiacha mikononi mwa soko huria pekee bila kuathiri upatikanaji wake kwa wananchi wa kawaida.

3. Tuangalie mifano ya kimataifa kwa umbali wa kilomita 200-500

Ufaransa (TGV): Safari ya takriban 300km kutoka Paris hadi Lille hutozwa kati ya EUR 30 hadi 60 (\~TZS 85,000 - 170,000), kutegemea muda wa kununua tiketi.
Uchina (High-Speed Rail): Safari ya km 350 kutoka Beijing hadi Shijiazhuang hutozwa takriban CNY 100 (\~TZS 35,000).
Kenya (SGR): Safari ya 472km kutoka Nairobi hadi Mombasa ni Ksh 1,000 (\~TZS 19,000) kwa daraja la kawaida,sema hii ni ya dizeli.
Japan (Shinkansen): Safari ya 370km kutoka Tokyo hadi Nagoya ni takriban JPY 10,500 (\~TZS 170,000).

Kwa mantiki hii, Tanzania bado imo kwenye kiwango cha chini sana cha bei kulinganisha na huduma zinazotolewa.

4. Uendelevu wa mradi:
Hakuna mradi wa kimkakati unaoweza kujiendesha bila mapato ya kutosha. Ikiwa tunataka huduma bora ziendelee kwa muda mrefu, tunapaswa kuruhusu nauli ambazo angalau zinagharamia sehemu ya uendeshaji huku serikali ikiendelea kufidia maeneo muhimu kama uboreshaji wa miundombinu au punguzo kwa makundi maalum.

5. Faida kwa abiria:
Kwa sasa, SGR inatoa faida ya:

  • Safari ya haraka (saa 2 hadi Moro)
  • Faraja na usalama
  • Gharama ndogo ikilinganishwa na magari binafsi au mabasi ya haraka
  • Kupunguza msongamano barabarani
  • Unafuu wa gharama ya fedha na muda. Kumbuka muda ni mali.

Hitimisho:
Kwa kuzingatia yote haya – kasi, usalama, ustaarabu wa huduma, na muktadha wa kujiendesha kibiashara – bei ya TZS 13,500 kwa umbali huo si tu kwamba ni ya haki, bali ni ya gharama nafuu kulinganisha na huduma zinazotolewa. Nauli hii ni sehemu ya kuhakikisha mradi unakuwa endelevu badala ya kutegemea ruzuku milele.

Mbadala kwa mwananchi ni kudaka basi la Abood Dar-Moro unafika saafi, treni wanapanda wenye 13,500 yao!

N'yadikwa
 
Ni muhimu kufahamu kwamba nauli ya TZS 13,500 kwa safari ya SGR kutoka Dar hadi Moro umbali wa takribani kilomita 200 haipaswi kuangaliwa kwa jicho la gharama za mafuta pekee bali kwa muktadha mpana wa huduma inayotolewa, uendelevu wa mradi na mifano ya kimataifa.
1. Uendeshaji wa SGR unahitaji fedha kubwa:
Ni kweli kuwa gharama za kuendesha treni ya kisasa ya umeme kama SGR ni kubwa. Zinajumuisha mishahara ya watumishi, matengenezo ya mabehewa na reli, gharama za nishati (umeme), usalama wa abiria na mifumo ya udhibiti wa kidijitali. Haya yote yanahitaji fedha za uhakika kila siku.

2. Ruzuku na sekta binafsi
Hivi sasa, serikali ndiyo inayochukua mzigo mkubwa wa awali wa uwekezaji kwenye miundombinu. Hata hivyo, endapo huduma hii ingeachiwa sekta binafsi moja kwa moja bila ruzuku yoyote, kuna uwezekano mkubwa nauli ingekuwa juu zaidi kutokana na azma ya sekta binafsi kutafuta faida ya haraka. Mifumo ya usafiri kama SGR huwa ni ya kimkakati – hivyo siyo rahisi kuiacha mikononi mwa soko huria pekee bila kuathiri upatikanaji wake kwa wananchi wa kawaida.

3. Tuangalie mifano ya kimataifa kwa umbali wa kilomita 200-500

Ufaransa (TGV): Safari ya takriban 300km kutoka Paris hadi Lille hutozwa kati ya EUR 30 hadi 60 (\~TZS 85,000 - 170,000), kutegemea muda wa kununua tiketi.
Uchina (High-Speed Rail): Safari ya km 350 kutoka Beijing hadi Shijiazhuang hutozwa takriban CNY 100 (\~TZS 35,000).
Kenya (SGR): Safari ya 472km kutoka Nairobi hadi Mombasa ni Ksh 1,000 (\~TZS 19,000) kwa daraja la kawaida,sema hii ni ya dizeli.
Japan (Shinkansen): Safari ya 370km kutoka Tokyo hadi Nagoya ni takriban JPY 10,500 (\~TZS 170,000).

Kwa mantiki hii, Tanzania bado imo kwenye kiwango cha chini sana cha bei kulinganisha na huduma zinazotolewa.

4. Uendelevu wa mradi:
Hakuna mradi wa kimkakati unaoweza kujiendesha bila mapato ya kutosha. Ikiwa tunataka huduma bora ziendelee kwa muda mrefu, tunapaswa kuruhusu nauli ambazo angalau zinagharamia sehemu ya uendeshaji huku serikali ikiendelea kufidia maeneo muhimu kama uboreshaji wa miundombinu au punguzo kwa makundi maalum.

5. Faida kwa abiria:
Kwa sasa, SGR inatoa faida ya:

  • Safari ya haraka (saa 2 hadi Moro)
  • Faraja na usalama
  • Gharama ndogo ikilinganishwa na magari binafsi au mabasi ya haraka
  • Kupunguza msongamano barabarani
  • Unafuu wa gharama ya fedha na muda. Kumbuka muda ni mali.

Hitimisho:
Kwa kuzingatia yote haya – kasi, usalama, ustaarabu wa huduma, na muktadha wa kujiendesha kibiashara – bei ya TZS 13,500 kwa umbali huo si tu kwamba ni ya haki, bali ni ya gharama nafuu kulinganisha na huduma zinazotolewa. Nauli hii ni sehemu ya kuhakikisha mradi unakuwa endelevu badala ya kutegemea ruzuku milele.

Mbadala kwa mwananchi ni kudaka basi la Abood Dar-Moro unafika saafi, treni wanapanda wenye 13,500 yao!

N'yadikwa
Hiyo 500, na 1,000 zimewekwa ili kugharamia afya.

Hili lundo looooote la maelezo halina maana yoyot.
 
Hiyo 500, na 1,000 zimewekwa ili kugharamia afya.

Hili lundo looooote la maelezo halina maana yoyot.
Leta hoja acha kurukaruka. Huwezi kulipa hiyo panda basi Lupila Express. Sio lazima upande treni
 
Ogopa sana matapeli wanaitwa ccm na bunge lao. Wameshafanya yao bungeni kimya kimya. Na bunge lilivyokuwa limejaa wale wa la saba C hawakuona kama kuna ongezeko la nauli linapitishwa kimya kimya
 
Kipindi bajeti inapitishwa ulikuwa wapi izo tozo zimeogezeka had kwa wasafiri wa ndege wao wameongezwa 1000

Lipa Kodi kwa maendeleo ya nchi yako
Kapitie kwanza taarifa ya CAG ndiyo uje utoe hiyo kauli Yako ya mwisho
 
Wakati wa wasilisho la bajeti ya mwaka wa fedha wa serikali 2025/2026 taarifa ya ongezeko la tsh 500 ama 1000 kwenye ticket za usafiri wa SGR / Ndege lilitolewa
Wakati bajeti inasomwa, yeye alikuwa busy kufuatilia Simba na Yanga!
 
Unataka Trilioni 40 zilizokopwa zilipwe na hela gani?

Dokta Mwigulu na Msomi nguli tena mbobezi wa uchumi aongeze kidogo ifike 20 ili tulipe madeni na tuweze kukopa sana.
 
Utakuwa Jisukuma. Wewe maana huna akili hata kidogo.

Umeshachukua baiskeli yako?
Hahaha haya mapovu yako ndio nayafurahia. Jibu hoja pale huna hoja panda basi SGR train waachie wenye hela
 
Nauli kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro yapanda kimya kimya kutoka Sh 13,000 hadi Sh 13,500 – licha ya kutumia umeme badala ya mafuta

Soma Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba anawasilisha Bajeti Kuu ya Serikali 2025/2026





Katika hali ya kimya isiyoambatana na maelezo kwa wananchi, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepandisha nauli ya treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kutoka shilingi 13,000 hadi 13,500. Ongezeko hili la shilingi 500 linaweza kuonekana dogo kwa macho ya juu juu, lakini linazua maswali makubwa kuhusu mchakato, mantiki na uhalali wa kupandisha bei za usafiri wa umma – hasa kwa huduma inayotumia nishati ya umeme badala ya mafuta ghali.

Ikumbukwe kuwa moja ya hoja kuu ya ujenzi wa reli ya kisasa ilikuwa ni kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutumia treni za umeme, ambazo ni rafiki kwa mazingira na nafuu zaidi kwa uendeshaji ukilinganisha na treni au mabasi yanayotumia mafuta. Kwa hiyo, ikiwa gharama za mafuta duniani zimepanda, hiyo haiwezi kuwa sababu ya moja kwa moja kwa SGR, kwani injini zake hazitegemei dizeli wala petroli.

Katika mazingira hayo, swali linabaki: Kwanini nauli inapanda? Na kama kweli umeme ndio sababu, je, kuna ongezeko la bei ya umeme kwa kiwango hicho kikubwa kiasi cha kuathiri nauli? Tanesco haijatangaza mabadiliko makubwa ya bei kwa wateja wa viwandani kama TRC.

Wananchi wana haki ya kuelewa vigezo vinavyotumika. Je, TRC imeongeza ubora wa huduma? Imepunguza muda wa safari? Imeongeza mabehewa? Kama hakuna mabadiliko yoyote ya kiutendaji au huduma, basi ongezeko hili linaweza kutafsiriwa kama mzigo wa kimyakimya kwa wananchi wa kawaida.

Kwa kuzingatia kwamba SGR ni mradi mkubwa wa kimkakati, uliogharimu mabilioni ya fedha za mkopo na kodi ya wananchi, haipaswi kuwa chanzo cha faida kwa bei ya juu, bali suluhisho la usafiri nafuu. Uhalali wa kuongeza nauli unapaswa kuambatana na:

Uwazi wa gharama za uendeshaji

Ushirikishwaji wa wadau, hususan abiria

Taarifa rasmi kwa umma kabla ya mabadiliko


Je, kuna mamlaka huru inayodhibiti viwango vya nauli ya SGR, kama ilivyo EWURA kwa mafuta au LATRA kwa mabasi? Au TRC inaamua yenyewe na kutekeleza?

Kupanda kwa bei kimya kimya huku kukitumia umeme kama chanzo cha nishati kunaashiria uwepo wa sintofahamu katika mfumo mzima wa upangaji wa bei. Hali hii si tu inaleta kero kwa wasafiri, bali pia inapunguza imani ya umma kwa taasisi zinazohusika.

Wakati wananchi wanapongeza kasi, usalama na unafuu wa SGR, ni muhimu pia kuweka bayana kuwa huduma bora haimaanishi lazima iwe ya gharama kubwa, hasa kwa miundombinu inayotegemea nishati nafuu kama umeme.

Tunahitaji majibu. Tunahitaji mjadala wa wazi. Tunahitaji uwazi.
SGR ni mali ya Watanzania wote – nauli yake pia ni suala la umma.

"Any government is an organ of exploitation by nature."

Mikhail Bukanin.

Kwa hiyo katika maisha yako ya hapa duniani usitarajie kupata Kitu chochote kile kilicho kizuri kutoka kwa Serikali
 
Ni muhimu kufahamu kwamba nauli ya TZS 13,500 kwa safari ya SGR kutoka Dar hadi Moro umbali wa takribani kilomita 200 haipaswi kuangaliwa kwa jicho la gharama za mafuta pekee bali kwa muktadha mpana wa huduma inayotolewa, uendelevu wa mradi na mifano ya kimataifa.
1. Uendeshaji wa SGR unahitaji fedha kubwa:
Ni kweli kuwa gharama za kuendesha treni ya kisasa ya umeme kama SGR ni kubwa. Zinajumuisha mishahara ya watumishi, matengenezo ya mabehewa na reli, gharama za nishati (umeme), usalama wa abiria na mifumo ya udhibiti wa kidijitali. Haya yote yanahitaji fedha za uhakika kila siku.

2. Ruzuku na sekta binafsi
Hivi sasa, serikali ndiyo inayochukua mzigo mkubwa wa awali wa uwekezaji kwenye miundombinu. Hata hivyo, endapo huduma hii ingeachiwa sekta binafsi moja kwa moja bila ruzuku yoyote, kuna uwezekano mkubwa nauli ingekuwa juu zaidi kutokana na azma ya sekta binafsi kutafuta faida ya haraka. Mifumo ya usafiri kama SGR huwa ni ya kimkakati – hivyo siyo rahisi kuiacha mikononi mwa soko huria pekee bila kuathiri upatikanaji wake kwa wananchi wa kawaida.

3. Tuangalie mifano ya kimataifa kwa umbali wa kilomita 200-500

Ufaransa (TGV): Safari ya takriban 300km kutoka Paris hadi Lille hutozwa kati ya EUR 30 hadi 60 (\~TZS 85,000 - 170,000), kutegemea muda wa kununua tiketi.
Uchina (High-Speed Rail): Safari ya km 350 kutoka Beijing hadi Shijiazhuang hutozwa takriban CNY 100 (\~TZS 35,000).
Kenya (SGR): Safari ya 472km kutoka Nairobi hadi Mombasa ni Ksh 1,000 (\~TZS 19,000) kwa daraja la kawaida,sema hii ni ya dizeli.
Japan (Shinkansen): Safari ya 370km kutoka Tokyo hadi Nagoya ni takriban JPY 10,500 (\~TZS 170,000).

Kwa mantiki hii, Tanzania bado imo kwenye kiwango cha chini sana cha bei kulinganisha na huduma zinazotolewa.

4. Uendelevu wa mradi:
Hakuna mradi wa kimkakati unaoweza kujiendesha bila mapato ya kutosha. Ikiwa tunataka huduma bora ziendelee kwa muda mrefu, tunapaswa kuruhusu nauli ambazo angalau zinagharamia sehemu ya uendeshaji huku serikali ikiendelea kufidia maeneo muhimu kama uboreshaji wa miundombinu au punguzo kwa makundi maalum.

5. Faida kwa abiria:
Kwa sasa, SGR inatoa faida ya:

  • Safari ya haraka (saa 2 hadi Moro)
  • Faraja na usalama
  • Gharama ndogo ikilinganishwa na magari binafsi au mabasi ya haraka
  • Kupunguza msongamano barabarani
  • Unafuu wa gharama ya fedha na muda. Kumbuka muda ni mali.

Hitimisho:
Kwa kuzingatia yote haya – kasi, usalama, ustaarabu wa huduma, na muktadha wa kujiendesha kibiashara – bei ya TZS 13,500 kwa umbali huo si tu kwamba ni ya haki, bali ni ya gharama nafuu kulinganisha na huduma zinazotolewa. Nauli hii ni sehemu ya kuhakikisha mradi unakuwa endelevu badala ya kutegemea ruzuku milele.

Mbadala kwa mwananchi ni kudaka basi la Abood Dar-Moro unafika saafi, treni wanapanda wenye 13,500 yao!

N'yadikwa
Ni vizuri umetumia mfano WA nchi nyingine kujilinganisha. Sasa tutumie nchi hizo hizo kuona wao wanalipwa kiasi gani (kima Cha chini) mishahara, ili uone utofauti.

Nchi/NyongezaKiwango kwa TZS
Tanzania (minimum)TZS 500,000/mwezi
China (Shanghai)TZS 990,000/mwezi
China (Guangxi)TZS 622,000/mwezi
UfaransaTZS 5,600,000/mwezi
Japan (Tokyo)~TZS 3,721,600/mwezi
Japan (Akita)~TZS 3,043,200/mwezi
Hizo nchi mishahara Yao ni mikubwa hata gharama zao za maisha zitakuwa Juu TU.
 
Back
Top Bottom