Je, ni chuo kipi kizuri kusoma 'Course' ya 'Information Technology'?

Je, ni chuo kipi kizuri kusoma 'Course' ya 'Information Technology'?

Dogo ataenda kukua tu huko, watu waliosoma IT, IFM wanajua kupiga windows na kutengeneza graphics tu ahahahaha what a joke college.
hili naliona sana kwa watu wanao soma IT wengi wanafanya graphic sijui kwanini aisee
 
hili naliona sana kwa watu wanao soma IT wengi wanafanya graphic sijui kwanini aisee
Ndo wanachokiweza na ni rahisi.
ila kiuhalisia hata sio somo wanalolisoma hata kwa semester moja.
.
Na kuja baadhi ya wapuuzi pale ndaki ya informatics wameanza kufanya huu ujinga mtu yuko third year eti anafanya graphics za YouTube zile, na vi-language vya kuokoteza
 
Mbona sasa na mbwembwe zote lakini walidukuliwa
Watanzania wengi wamekariri kusoma kwa shida na kwa mikiki ndio elimu nzuri. Ukiwa na nia ya kusomea kitu fulani utafanikiwa tu, na ukimaliza utakuwa ni besy.

Unamkuta mtu kasoma UD Engineering anavyokuja kujikita mtaani kuwa yeye ni kichwa utamuonea aibu. Wakati anaburuzwa na vijana wa DIT.

Ninachofahamu mimi ni hiki, kila chuo kina course zake ambazo ni best. Mfano mambo Engineering DIT wapo vizuri, ukija course kama ya IT hakika utawakataa. IFM mambo ya finance hawakamiti, mambo ya Law UD ni namba nyingine. Procurement na Marketing CBE wapo vyema zaidi, IT naona The Unique ya Upanga wapo practical sana, nashauri wale wasiopenda majina ya vyuo wakasome hapo.

Haya mambo sijui nimesoma chuo flani yameshapitwa na wakati, ingekuwa kusoma saaana ndo elimu basi SUA huenda ingekuwa ndo chuo bora Tanzania.
 
Aende DIT, KIU au UCC ndiko kunamfaa.
Asijaribu hata kuifikiria UDOM pale ni kitu ingine ata disco semester ya kwanza tu
Unaijua DIT vzr mkuu kwa hiyo kozi? sidhan ka kuna sehem ngmu kama pale kwa IT, UDOM sjui pakoje but sidhan ka utafkia mzki wa DIT
 
Sir ndio habari ikufukie ile ndaki ya Informatics pale UDOM achana nayo kama IQ ya ni ndogo.
.
DIT nakufahamu nimesoma Diploma pale pakawida sanaaaa yani sanaa
Maybe ulsoma food science,We darasa wanaanz watu 160+ first year linapgwa panga second year mnajikuta 90+ af useme pa kawaida?? chief kua serious dit ka hujielew unap
otea
 
Atafute chuo ambacho anaweza kupiga lab sio vyuo theory nyingi kama UD
Ajaende Unique pale akacheki

tatizo huelewe the bases of the two, theory and practical!!!

theories these are like principles or guidlines! from theories or guidelines anything can be done. Wewe unayefikiri practical ni nzuri kuliko theory umepotea sana!

Mwanafunzi/mtaaruma mzuri inatakiwa uelewe principles behind certain issues then utumie principle our guideline hizo kutengeneza kitu kingine

MFANO: ukiona unaenda chuo cha ICT siku ya kwanza tu unaanza ingizwa lab kufanya practical mpaka unatoka jua umekaririshwa na wewe sio mtaalamu bali ni fundi tu wakawaida. Kwanza inabidi ujue all theories behind ili siku likija tatizo lingine jipya unarefers tu, au unajua what is the source and why it happened
 
tatizo huelewe the bases of the two, theory and practical!!!

theories these are like principles or guidlines! from theories or guidelines anything can be done. Wewe unayefikiri practical ni nzuri kuliko theory umepotea sana!

Mwanafunzi/mtaaruma mzuri inatakiwa uelewe principles behind certain issues then utumie principle our guideline hizo kutengeneza kitu kingine

MFANO: ukiona unaenda chuo cha ICT siku ya kwanza tu unaanza ingizwa lab kufanya practical mpaka unatoka jua umekaririshwa na wewe sio mtaalamu bali ni fundi tu wakawaida. Kwanza inabidi ujue all theories behind ili siku likija tatizo lingine jipya unarefers tu, au unajua what is the source and why it happened
ICT, ukisoma theory bila labs unaona kawaida
Yani mtu akufundishe vmware migration, vcenter, vsphere, high availability na load balancing bila labs mkuu?
Ndio maana unakuta kuna foreigner kibao kwenye private institute
 
Sir ndio habari ikufukie ile ndaki ya Informatics pale UDOM achana nayo kama IQ ya ni ndogo.
.
DIT nakufahamu nimesoma Diploma pale pakawida sanaaaa yani sanaa
Upo sahihi, IT DIT ni kawaida, haina ugumu wowote ule.
 
Habari zenu Wadau wa JamiiForums,

Kuna rafiki yangu anaitaji kujua kuhusu chuo kipi kizuri anachoweza kusoma Course ya Information Technology (IT)

Yeye amemaliza Form Four (IV) mwaka jana


Ushauri wenu tafadhali
Hakuna cha UDSM, DIT wala IFM, vyote ni chenga kwenye IT!!

Kama unajali pesa yako na kama unataka kuwa nondo kwenye IT na kama unataka kusoma modern technology na sio kusoma mambo ya miaka ya 80 basi soma hizi sehemu

1. Udemy.

2. Youtube.
 
Hakuna cha UDSM, DIT wala IFM, vyote ni chenga kwenye IT!!

Kama unajali pesa yako na kama unataka kuwa nondo kwenye IT na kama unataka kusoma modern technology na sio kusoma mambo ya miaka ya 80 basi soma hizi sehemu

1. Udemy.

2. Youtube.
Youtube has all you need
 
Back
Top Bottom