Je, ndoa hii nani mkosaji?

Tatizo hapo lipo kwenye agano mliloweka kwa binti yule aliyekuwa Kampala. Mtafute muombe radhi tena akiridhia yeye kukuachilia kabisa moyoni mwake bila kufikiri muda aliopoteza basi laana yake itakuachia maisha yako yatakuwa sawa kabisa na ndoa yako utaifurahia.
 
Pole xana mkuu,lakin nakushanga xana mwanaume kukosa maamuzi ya kiume,huyo mwanamke kashakuona ww hujielewi ndio maana anafanya tena makusdi,eti analipiza kisasi.Hiyo ndoa bado changa xana kaka na huyo mkeo ni gamba yafaa ulivue mapema.kilichobaki ni kumkuta mume mweza amelala kitandan pako,kwani huna house girl hapo wakuchukua nafasi yake?
 
Si alisema hapo kuwa aliachana na huyo mchumba wake baada ya mke kuwa na mimba.
Ameeleza hapo huyo mke alianza tabia hiyo kabla ya ndoa tena kabla hata huyo mchumba wa jamaa hajarudi.

Huyu mwanamke hafai kuwa mke wa mtu huyu wala usimtetee hapo.

Heti nalipa kisasi!!!
Mke wa mtu kabisaaa huyo anaongea hivyo.

Ningekuwa Mimi tungeachana siku hiyohiyo.

Ndugu ukimchekea huyu basi usubiri kuzikwa na kilo mbili, umuache mwanao yatima.

Pili chunguza vizuri hata huyo mtoto inawezekana si wako huyo kuna kila dalili ya kubambikiziwa hapo.

Unaishi na shetani sio mke huyo na huo uvumilivu wako utakuponza siku si nyingi.
 
Nashangaa hadi leo bado anaifuga hii takataka tu.
Yani ninahasira kama ni mimi ndio nimefanyiwa haya.
Mungu wangu unaniona siku nikioa na nikafanyiwa haya hakika nitamuua Mimi tena nitamchinja kama kuku kama laana basi sawa tu wacha niipata.

Jike linathubutu kusema linalipa kisasi!!!!!!
 
Ubaya nao ni mbegu huna budi kula mazao yake

Binti wa chio Kampala ndio kabeba hatma ya yote mtafute myamalize kiustaarabu ila sio kumuoa tena

Na hiyo ndoa vunja mapema hata Mungu anaelewa katupa ruhusa kuachana unapobainika uzinzi
 
We umesema ndo Warudi nyumbani mida kama hii, unafikiri yeye anawaza ulikuwa wapi???

Yaani wote mmekaa kukomoana tuu!!!! Mkuu hakuna ndoa ya hivyo, na mwanamke haolewi kwa kigezo cha mimba. Usipoangalia mtaleteana magonjwa sasa
Nafanya yote haya baada ya uvumilivu wangu kufika mwisho, yaan hapa naanda taaratibu za mwsho kabla sijamwonesha mlango wa kutokea.
 
Mkuu nishamuomba radhi saaana na akaridhia, ila akasema hawezi olewa maaana hatatokea mwanaume wa kumwamni, yupo Bunda Mara kwa sasa kaajiriwa mamlaka ya mapato hataki kusikia kiumbe aitwae mwanaume.
 
Ubaya nao ni mbegu huna budi kula mazao yake

Binti wa chio Kampala ndio kabeba hatma ya yote mtafute myamalize kiustaarabu ila sio kumuoa tena

Na hiyo ndoa vunja mapema hata Mungu anaelewa katupa ruhusa kuachana unapobainika uzinzi
Nishaongea nae saana,kashakubali japo shingo upande.
 

Piga chini, kama mchumba wako wa mwanzo hajaolewa muombe msamaha mrudiane
 
Sijui hata unalia lia nini! Mbona ulipaswa uchukulie poa yaani ulikuwa na mpenzi ukawa na mtu hadi unaishi naye ndani, hukumwambia tu, ukamtia mimba bado mwenzio unamdanganya unampenda, ukajiandaa nhoa dada wawatu uchumba miaka 7 unampa moyo tu! Huoni wewe unastahili adhabu zaidi ya hiij? Hebu pata picha umeoa halafu mpenzi wako wa zamani ukamchukulia chumba ulitaka udanganye ukalale huko. Huyo mwanamke analipiza sali sana mtafute yule dada muombe msamaha hata kama kaolewa mwambie akusamehe ili uishi maisha mazuri na ndoa yako.
 
Tuliza akili yako kwa makini na kisha piga goti kwa dua ikiwezekana hata swala za usiku muombe mungu akioneshe njia sahihi ya wewe kupita maana sisi hata kama yukikwambia achana nae bado moyo wako ni mgumu maana kwa mazito hayo lakini bado uko nae ni dhahri kuwa ulimpenda na bado unampenda mno. Japo uamuzi sahihi ulikuwa ni kimuacha ili kila mmoja atazame maisha yake siyo rahisi sana kwa yeye kujifunza Leo ila anaweA kukumbuka baadae na akajuta sana zaiditagutie mwanao mazingira mazuri ya kuishi kimaadili ili asijifunze mabaya kwenye familia yako kutoka kwa mama yake.
 
Umetenda dhambi mbaya, mbaya, mbaya kuliko maelezo. Tubu sana mbele ya Mungu umwombe akusamehe. Wewe umekaa uchumba na msichana miaka saba halafu unakuja kumwacha kwa mwanamke wa kuokota? Unatema bigi jii kwa karanga za kuonja?

Fahamu yafuatayo:- Lile agano uliloweka na yule msichana wako wa kwanza litakufata maisha yako yote kama usipoenda kwake ukamwoba msamaha, na akaridhia kukusamehe. Hata ukimwoa mwingine hiyo laana yake itakufuata tu. Kumbuka umeshasema hataki tena mwanaume. Umemwharibia maisha yake kabisa.

Kwanza tubu kwa Mungu. Halafu nenda kamwombe huyo mchumba wako wa kwanza msamaha. Afute maneno yote ya kulaani ambayo amekutamkia wewe na amejitamkia yeye (kama kusema hataki tena mwanaume kamwe). Halafu, kama akikubali mwoe yeye.

Huyu uliyefunga naye ndoa mwache. Hata kama umefunga kanisani. Uasherati ndio sababu pekee ambayo inaruhusiwa kuwa kigezo cha kuvunja ndoa kwenye Biblia. Kamwe usidhani huyo mkeo wa sasa atakaa abadilike. Kama anabadili wanaume kama nguo za ndani huoni anaweza kuja kukuua kwa ugonjwa?
 
Hayo ni malipo ya kilio alicholia mchumba wako wa kwanza na kuipata amani itakua kazi hasa

Huyo mwanamke ulijua tabia zake mbaya tangu mwanzo ila ukakomaa kumuoa hilo ni kosa lako la pili

Sasa basi mtafute mchumba wako wa kwanza muombe msamaha ili upate amani ya moyo na pia ndoa ya kikristo haivunjiki kamwe huo ni msalaba wako ndugu huna budi kuubeba
 
pole kk kama kweli unamjua mungu huwez vunja ndoa lakini huoni furah y ndoa hapo kaa chini na mkeo mtoe tofaut zenu na muanze new life jinsi ulivo eleza inaonesha huyo mwnamke sio chaguo langu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…