Je, naweza kusave SMS kwenye SD CARD?

Je, naweza kusave SMS kwenye SD CARD?

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,902
Reaction score
15,931
Mimi ni wakala wa mitandao ya simu, eneo nililopo lina wateja wengi hivyo kuna uwezekano wa kuhudumia wateja zaidi ya 150 kwa siku, shida ni kwamba huwa nakuwa na uraratibu wa kurekodi meseji zote kwenye vitabu vya mitandao husika kwa ajili ya usalama, kwa sasa hiyo kazi naona imekuwa ngumu kwa sababu ofisi imekuwa na mambo mengi na idadi ya wahudumu ni ileile.

Je, nnawezaje kuzisave msg zote (mfano za mwezi mzima) bila kuziandika, maana changamoto ya hizi simu tunazotumia kwa ajili kuhudumia wateja ni hizi ndogo zenye uwezo wa kutunza msg chache. Asante
 
Swali hili nilikuwa najiuliza sana, kwanini mawakala wengi wanatumia viswaswadu ?

Alafu pili, hivi huwezi kutumia App husika ( mfano app ya Airtel money, M pesa, Tigo pesa) ukiwa wakala ili urahisishe kazi ?
Wengi wanaogopa sim kuzima ila kama ni kufanya tu miamala sim ina uwezo wa kuwa na charge 12hrs+
 
Je smartphone gani ndogo inaweza kufaa kwa kazi hii, yaani inaweza kukaa na chaji muda mrefu na kuperform vizuri?
 
Mkuu alternative tafuta Feature phone ambazo kidogo ni smart, simu kama za Kaios, Android feature phone ama hata symbian na Java phones, zote hizi zina app za backup
Asante mkuu, vipi hizo simu kwenye utunzaji wa chaji?
 
Asante mkuu, vipi hizo simu kwenye utunzaji wa chaji?
Simu za Symbian kama E52 inakaa na chaji uhakika siku kadhaa. Pia kai os si mbaya, sema backup ya sms kwenye Kai os ina mlolongo kidogo.

Ila kama smartphone haikusumbui hio Xz1 compact ni nzuri sana, kidogo sana hakina utofauti sana na vitochi, pia inakaa sana na charge, halafu bei zake used pia ni ndogo chini ya laki 2.

Cha muhimu hakikisha tu battery health ipo poa.
 
Simu za Symbian kama E52 inakaa na chaji uhakika siku kadhaa. Pia kai os si mbaya, sema backup ya sms kwenye Kai os ina mlolongo kidogo.

Ila kama smartphone haikusumbui hio Xz1 compact ni nzuri sana, kidogo sana hakina utofauti sana na vitochi, pia inakaa sana na charge, halafu bei zake used pia ni ndogo chini ya laki 2.

Cha muhimu hakikisha tu battery health ipo poa.
Je hiyo ya Kai internal memory yake inaweza kutunza msg kama 1000? Na chaji inaweza kwenda masaa 24?
 
Back
Top Bottom