Kacharimbe
JF-Expert Member
- Apr 2, 2011
- 211
- 34
Wakuu heri ya mwaka mpya. Kwa muda sasa suala hili limekuwa likinisumbua. Imenitokea mara kadhaa kuwa naweza kuwaza kitu fulani au mtu fulani sura yake ikaja na baadaye kitu hicho hutokea au kama ni mtu unaona anakuja au unakutana naye. Leo nilikuwa naweza jinsi ya kutoka ofisini ili niende kwenye sherehe. Wazo likaniijia kuwa nisingizie kuwa kwa jirani kuna msiba. Wazo hilo nikalifuta haraka sana. Haijapita hata saa moja nikapigiwa simu kuwa jirani yangu amefariki. Hi ni nini au ni coincidence?