mwandende
JF-Expert Member
- Feb 16, 2017
- 10,518
- 19,883
Huyo mtoto hana chake mkuu,,,mwache aende POPOTE,,,,mtoto huyo sio DAMU yako,,,na hakuna mahakama itakayompa ushindi huyo mama,,,Habari wapendwa?
Tuna watoto 4, ila mtoto mkubwa wa kwanza sio wangu nilioa mke wangu akiwa tayari ana mtoto, watoto watatu ndio nilizaa naye. Huyu mtoto wa kufikia tangu akiwa mdogo miaka 2 nimemuhudumia kila kitu hata shule hajawahi kusoma hizi shule za kata, sasa hivi yupo kidato cha 3.
Wakati namuoa nilimpa masharti sitaki mawasiliano na baba mtoto wako, hata yeye anadai hawezi kuwasiliana naye maana aliikataa mimba. Miaka minne iliyopita niligundua anawasiliana na mzazi mwenzie ikafikia hatua kipindi nipo safari alikuwa akimpeleka mtoto kwa mzazi mwenzie nikaona haina shida maana ni damu yake, ila nikamuuliza baada ya miaka 11 leo hii mtoto amekua mkubwa ndio ameona umuhimu wake?
Alikataa mimba leo unamuona wa maana? Ndani ya miaka 2 naona amebadilika sana amefikia hatua anaanza kumwambia mtoto baba yake ndiye anayemuhudumia kila kitu, huyu mtoto ameanza kupunguza upendo kwangu ni tofauti na zamani.
Kiuchumi MUNGU amenisaidia nipo vizuri nilichofanya mali zangu zote pamoja na pesa nimewaandikishia watoto wangu wa damu, huyu wa kufikia nimeachana nae sijampa chochote licha ya kumlea kwa miaka 12. Je, kuna kosa kisheria? Maana mama yake anataka kwenda mahakamani ili na yeye mtoto wake apate sehemu ya mali.
NB: Katika mali zangu huyu mwanamke hana mchango wowote wakati namuoa kila kitu alikikuta
Sent using Jamii Forums mobile app