MGILEADI
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 1,621
- 1,543
Wakalimani hulipwa kwa masaa kama ni mkutano ama kikao na kwa siku kama ni ziara na wageni. Pia angalia uwezo wa hao wageni. Wanasema Watanzania "bajeti yako ni kiasi gani?" Mimi sidhani kama hilo swali ni zuri. Aombe 20000 kwa saa ikiwa ni kikao. Wameketi wanaongea hapa na pale.Kama ni Mkutano anakalimani moja kwa moja. aombe 50000 kwa saa. Ikiwa ni mchanganyiko wa mambo mengi kwa siku aombe 50000 hadi 100000. La msingi apime uwezo wao na uzito wa kazi asizidi 100000 kwa siku watamkimbia. Malipo yategemee huduma. Ikiwa ni biashara ama utalii rate huwa juu usd 50 kwa siku yaani 100000. Lakini kama ni kikanisa yaani kidini aombe hata 50000 kwa siku na 10000 kwa saa.Ushauri tu.Huyo mtafsiri ni mtaalamu wa tafsiri ama mtafsiri tu?