Je Miradi ya Umeme ya Serikali Itakuja Kuua Biashara ya Solar?

Nyaka-One

JF-Expert Member
Oct 27, 2013
4,725
6,730
Kumekuwepo na biashara kubwa ya vifaa vya umeme unaotokana na mwanga wa jua (solar energy system). Biashara hii imeshamiri kila kona ya nchi ikiwa inafanywa na wafanyabiashara wakubwa na wadogo. Pia biashara hii imevutia makampuni mengine ya kigeni kama Off-Grid ambao makao yao kwa Tanzania yapo Arusha, Solar Sister (kanda ya ziwa), M-Kopa Solar Ltd (Dar es Salaam) ambao wao wanawafungia wateja wao vifaa vya solar bure kisha wateja hao kulipa malipo ya kila mwezi kwa kampuni.

Sasa nikiangalia uwekezaji unaofanywa na serikali kwa sasa hivi kwenye kuzalisha umeme na kuusambaza kwa watumiaji ikiwa ni pamoja na mradi uliopo wa umeme wa REA utakaosambaza umeme hadi vijijini, najiuliza kama bado hii biashara ya solar ina muda mrefu wa kuendelea kuwepo na kutengeneza faida kwa wafanyabiashara/wawekezaji kama hao Off-Grid, Solar Sister, M-Kopa Solar? Hebu wadau tuchangie ili kuelimishana.
 
Sasa km umeme wa uhakika unapatikana solar ina umuhimu gani# unahofia kibarua chako nn utaajiriwa TANESCO
 
Nafasi ya Solar hasa ikiwa ya gharama nafuu bado itakuwepo. Nchi za wenzetu pamoja na kuwa na umeme wa uhakika toka vyanzo vingine, bado wanatumia Solar japo hawajabarikiwa kuwa na jua kama sisi
 
Itachukua muda sana hii biashara kutoweka...serikali bado haina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha hadi kwa kila mtanzania...bei ya umeme pia bado ipo juu kuweza kumruhusu kila mtanzania kuwa na hiyo nishati muhimu...hii biashara ya solar bado ipo ipo kwanza
 
Kumekuwepo na biashara kubwa ya vifaa vya umeme unaotokana na mwanga wa jua (solar energy system). Biashara hii imeshamiri kila kona ya nchi ikiwa inafanywa na wafanyabiashara wakubwa na wadogo. Pia biashara hii imevutia makampuni mengine ya kigeni kama Off-Grid ambao makao yao kwa Tanzania yapo Arusha, Solar Sister (kanda ya ziwa), M-Kopa Solar Ltd (Dar es Salaam) ambao wao wanawafungia wateja wao vifaa vya solar bure kisha wateja hao kulipa malipo ya kila mwezi kwa kampuni.

Sasa nikiangalia uwekezaji unaofanywa na serikali kwa sasa hivi kwenye kuzalisha umeme na kuusambaza kwa watumiaji ikiwa ni pamoja na mradi uliopo wa umeme wa REA utakaosambaza umeme hadi vijijini, najiuliza kama bado hii biashara ya solar ina muda mrefu wa kuendelea kuwepo na kutengeneza faida kwa wafanyabiashara/wawekezaji kama hao Off-Grid, Solar Sister, M-Kopa Solar? Hebu wadau tuchangie ili kuelimishana.
mimi nafikiria kuachana na miundo mbinu yao naweka solar japo nigharama lakini baada ya kuweka inakuwa imara
na gharama nafuu
 
Back
Top Bottom