Je Lissu ni mbeba maono?

Je Lissu ni mbeba maono?

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
869
Reaction score
1,282
Tundu Antipas Lissu ni mtu ambaye amekoswa-koswa sana katika siasa za nchi hii. Amenyimwa haki zake alipokuwa Mbunge, Amepigwa, amefungwa, ametukanwa na kumiminiwa risasi nyingi sana ili tu auawe. Lakini Mungu akasema, hapana. Lissu, bado nina ahadi naye.

Ni ahadi ipi aliyonayo Mungu kwa TAL?

Uchaguzi wa ndani wa Chadema ni ishara tosha nyingine tosha kuwa Lissu siyo mtu wa kawaida. Amemshinda Mbowe ambaye kiuchumi yupo vizuri, Mbowe ana mizizi mirefu ndani ya Chadema, Mbowe ana connection nzito nje ya Chama. Mbowe ana wafuasi wengi. Ila Lissu na team yake walimchakaza Mbowe na team yake.

Nini maana ya ushindi wote huu wa Tundu Lissu

Tukiwa wote kama Watanzania na jukumu letu likiwa ni kuleta maendeleo endelevu nchini, mi vyema kutafakari kwa kina haya maushindi yote ya huyu ndugu Lissu. Tusikilize kwa umakini ujumbe alionao na tuutafakari vizuri.

Nina hakika kupitia Lissu, mambo mengi yatabadilika hapa nchini na kuwa bora kabisa.

Mimi ni mwanachama wa Tanzania kwanza.
 
Hata bila reforms Lissu anashinda mapema asubuhi, ishu ni uchaguzi kuwa huru na haki
 
Anyway muda unaongea.. Tushukuru Teknolojia ama kweli. Hii ni Karne ya 21 ya Sayansi na Teknolojia.. Huwezi danganya.. Muda wote.. Walisema za mwizi. 40..
 
UCHAFUZI utazuiwa UCHAGUZI utakuwepo.asante Lissu huzi ndio siasa za Jino kwa jino tulizomuomba Mungu nae katujibu kwa kukuleta wewe na Heche na Mahinyila 🫡🫡🫡
 
Mtu kajiganga kwa waganga Huku, kesha fanya matambiki mia mnataka kuforce awe mteule wa MUNGU.......
MUNGU nu mjomba enu ety ?
 
Back
Top Bottom