Je, kuna uwezekano mwili wa binadamu kupiga shoti pasi na kugusa umeme?

Hot27

JF-Expert Member
Oct 31, 2020
308
422
Habari za wakati huu member wote wa JF. Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye mada ama swali kwa wenye ujuzi na wanaopenda kufahamu.

Jambo liko hivi, Leo wakati nimeenda duka la hatua chache toka ninapoishi nimekutana na jambo lililonishangaza kidogo.

Nilipofika dukani nikamkuta mzee, nadhani ni mstaafu ameamua afungue duka maranyingi nawakutaga watoto wake. Baada ya kumpatia hela kiasi cha shilingi 2000 na kuchukua mahitaji yangu ambapo hela iliyobaki ilikua Tsh 300. Sasa wakati ananipatia ile hela iliyobaki vidole vikagusana nikahisi shoti kama ya umeme iliyonishtua.

Baada ya ile shoti nikahisi ni zile chuma za dirishani ikabidi niziachie haraka hali ambayo yule mzee aliigundua.
Kwa maelezo yake aliniambia kuwa anawiki sasa yuko kwenye hali hio, maranyingi ni yeye ambae anahisi hio hali na si anaegusana nae ila leo amekutana na mtu ambae ameona pia hio hali ambae ni mimi.

Naomba kuuliza hiki kitu kinawezekana?! Nini chanzo chake na je, inatibika?! Ni kivipi anaweza kuitibu hio hali?!

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu.
 
Hio hali mie pia inanitokea sana ama nikigusa chuma au nikigusana na mtu, siku za mwanzo nilikuwa nikishangaa sana ila sasa nimegundua ni aina ya nguo tunazovaa wakati mwengine ndio zinasababisha, hasa za mpira (nylon)

Tena shoti yake inakuja na sauti km ya sparks ivi
 
Hio hali mie pia inanitokea sana ama nikigusa chuma au nikigusana na mtu, siku za mwanzo nilikuwa nikishangaa sana ila sasa nimegundua ni aina ya nguo tunazovaa wakati mwengine ndio zinasababisha, hasa za mpira (nylon)

Tena shoti yake inakuja na sauti km ya sparks ivi
Hizo nguo za Nylon zinaweza kuwa sababu pekee ama?
 
Kama ni mpya hivi kwa baadhi yetu maana si umeona watu walivyotoa ushuhuda kuwa imeshawatokea. Ngoja tuone wataalam nini wanasema
Kabisa , dunia ina mengi sana unaweza kuhisi umeona vingi kumbe bado

Navyo fahamu mwili ndio una system ya umeme lakini sio huu wa kuvibrate mpaka kushot mtu mwingine
 
Kabisa , dunia ina mengi sana unaweza kuhisi umeona vingi kumbe bado

Navyo fahamu mwili ndio una system ya umeme lakini sio huu wa kuvibrate mpaka kushot mtu mwingine
Nimeshangaa sana leo
 
Kama umesoma Physics...
Kuna kitu kinaitwa static charge ..mfano kuna mablanket yakigusana na nywele za mwili zinatengeneza charge ndogo..
Hata wakati mwingine net / coat zenye manyoya..

Kuhusu kugusana na huyo mzee ukapigwa short ni hivii..
Hapo kwenye duka hana mfumo wa earth.. Atafute fundi umeme...akague wiring system kisha anunue chumvi + mkaa na earth road ,wire.. .. Achimbie chini ya ardhi vizuri.. Afunge vizuri tatizo litaisha
 
Back
Top Bottom