Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Kwa kila Mtanzania makini na mwenye moyo wa dhati kwa Taifa hili atakuwa na maswali yafutayo:
1. Katika hali ngumu za maisha ambazo kila kukicha watu maskini wa taifa hili wanaendelea kusota kwa kukosa chakula, malazi na elimu, Je CCM ambao wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005 waliwahidi Watanzania maisha bora wameshindwa kutimiza au wametimiza maisha bora kwa kila Mtanzania?? Jibu unalo wewe mwenyewe Mtanzania??
2, CCM katika ahadi zake ilisema kuwa itatengeneza ajira milioni moja Je Ajira hizo zimepatikana au watu wamepata ajira???
3. CCM katika ilani yake ilisema kuwa itaboresha na kupunguza vifo vya wakina mama je Leo Mama Zetu wanakufa kwa kukosa huduma za afya vijijini au wakati wa kujifungua kwa kukosa huduma za afya??
4. CCM katika ilani yake ilisema kuwa itaongeza wigo wa Elimu ya juu je katika hilo wameweza au wamefanikiwa?? Je uongezeko hilo linaendana na ushindani katika sekta ya elimu na kuboresha vitendea kazi kwa walimu na na walimu ambao wanafundisha katika vyuo vyetu.
5. Katika Ilani ya CCM walisema kuwa watajenda barabara nchi Nzima Leo hii wameweza kujenga na hili unaweza kulinganisha na kipindi cha Mkapa?? Jibu unalo wewe mwenyewe katika kutazama maeneo unayotoka au kwenda na kuona kama kweli wameweza au lahasha??
6. Katika Kutoa mikopo ya elimu ya juu, CCM walisema kuwa Hakuna mtoto yoyote yule atayekosa elimu kwa ajili ya ada na kulipiwa ada katika vyuo vikuu, Lakini leo hii kuna maelfu ya watoto wa wakulima wamekosa au kufukuzwa katika vyuo hivi kwa ajili ya kushindwa kulipa ada na gharama nyingine.?? Jibu unalo wewe mwenyewe
7 Katika kupambana na ufisadi CCM inasema kuwa Rushwa ni adui wa haki Je leo Hakuna hata mtu mmoja aliwahi kuvuliwa hata uchama au ukada wake kwa ajili ya ulaji au utoaji rushwa kubwa kuna watu wengi wapo na wanaendele kuwapo katika Chama japo wamehusika na kuliingizia taifa hasara kubwa kama EPA, Kagoda, Richmond, Meremeta, na madudu mengine katika taifa na kuacha maskini wanateseka na watoto wetu kukosa sehemu hata elimu nzuri kwa ajili ya maisha yao baadae. Je CCM wanatekeleza Ilani yao??
8. Je CCM katika Ilani yake walisema kuwa watatoa Mitaji kwa ajili ya wafanya biashara na wakina mama Je Hizo pesa zimekufikia wewe kama mtu wa kawaida na kutumia katika njia nzuri au zilikwenda tu kisiasa na kufanya kampeni kwa ajili ya kuona kama kweli zimeleta ahueni katika maisha yako ya kila siku???
9. Ilani ya CCM wanasema kuwa wataendeleza yake yote mazuri na kufanya mwafaka kati yake na CUF kwa kumaliza yote na matatizo ya Zanzibar je leo hii bado mwaka mmoja wameweza kumaliza tofauti zao na kukaa kama Taifa moja Jibu la Swali hili unalo na Jibu jingine analo Prof Lipumba na Seif Sharif Hamad??
10 Je Kwa ujumla Maisha yake yameboreka au ndio umaskini umeongezeka katika Taifa letu?? Je kuna haja ya kuwachagua tena viongozi kama hawa?? Je kuna nia ya dhati katika kuwambia ukweli na kwa kuwauliza wakati huu na kuona kuwa wamefanya nini au ndio wao wanaendelea kusema kuwa TUTAFANYA HIVI?? JE hizi kauli za TUTAFANYA HIVI ZITAISHA LINI?? Maswali na majibu unayo wewe mwenyewe
11. Je Taifa kama Tanzania lipo katika njia nzuri ya kwenda au kupiga hatua katika maendeleo kwa sera hizi au mwenendo huu. Majibu unayo wewe mwenyewe.
1. Katika hali ngumu za maisha ambazo kila kukicha watu maskini wa taifa hili wanaendelea kusota kwa kukosa chakula, malazi na elimu, Je CCM ambao wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005 waliwahidi Watanzania maisha bora wameshindwa kutimiza au wametimiza maisha bora kwa kila Mtanzania?? Jibu unalo wewe mwenyewe Mtanzania??
2, CCM katika ahadi zake ilisema kuwa itatengeneza ajira milioni moja Je Ajira hizo zimepatikana au watu wamepata ajira???
3. CCM katika ilani yake ilisema kuwa itaboresha na kupunguza vifo vya wakina mama je Leo Mama Zetu wanakufa kwa kukosa huduma za afya vijijini au wakati wa kujifungua kwa kukosa huduma za afya??
4. CCM katika ilani yake ilisema kuwa itaongeza wigo wa Elimu ya juu je katika hilo wameweza au wamefanikiwa?? Je uongezeko hilo linaendana na ushindani katika sekta ya elimu na kuboresha vitendea kazi kwa walimu na na walimu ambao wanafundisha katika vyuo vyetu.
5. Katika Ilani ya CCM walisema kuwa watajenda barabara nchi Nzima Leo hii wameweza kujenga na hili unaweza kulinganisha na kipindi cha Mkapa?? Jibu unalo wewe mwenyewe katika kutazama maeneo unayotoka au kwenda na kuona kama kweli wameweza au lahasha??
6. Katika Kutoa mikopo ya elimu ya juu, CCM walisema kuwa Hakuna mtoto yoyote yule atayekosa elimu kwa ajili ya ada na kulipiwa ada katika vyuo vikuu, Lakini leo hii kuna maelfu ya watoto wa wakulima wamekosa au kufukuzwa katika vyuo hivi kwa ajili ya kushindwa kulipa ada na gharama nyingine.?? Jibu unalo wewe mwenyewe
7 Katika kupambana na ufisadi CCM inasema kuwa Rushwa ni adui wa haki Je leo Hakuna hata mtu mmoja aliwahi kuvuliwa hata uchama au ukada wake kwa ajili ya ulaji au utoaji rushwa kubwa kuna watu wengi wapo na wanaendele kuwapo katika Chama japo wamehusika na kuliingizia taifa hasara kubwa kama EPA, Kagoda, Richmond, Meremeta, na madudu mengine katika taifa na kuacha maskini wanateseka na watoto wetu kukosa sehemu hata elimu nzuri kwa ajili ya maisha yao baadae. Je CCM wanatekeleza Ilani yao??
8. Je CCM katika Ilani yake walisema kuwa watatoa Mitaji kwa ajili ya wafanya biashara na wakina mama Je Hizo pesa zimekufikia wewe kama mtu wa kawaida na kutumia katika njia nzuri au zilikwenda tu kisiasa na kufanya kampeni kwa ajili ya kuona kama kweli zimeleta ahueni katika maisha yako ya kila siku???
9. Ilani ya CCM wanasema kuwa wataendeleza yake yote mazuri na kufanya mwafaka kati yake na CUF kwa kumaliza yote na matatizo ya Zanzibar je leo hii bado mwaka mmoja wameweza kumaliza tofauti zao na kukaa kama Taifa moja Jibu la Swali hili unalo na Jibu jingine analo Prof Lipumba na Seif Sharif Hamad??
10 Je Kwa ujumla Maisha yake yameboreka au ndio umaskini umeongezeka katika Taifa letu?? Je kuna haja ya kuwachagua tena viongozi kama hawa?? Je kuna nia ya dhati katika kuwambia ukweli na kwa kuwauliza wakati huu na kuona kuwa wamefanya nini au ndio wao wanaendelea kusema kuwa TUTAFANYA HIVI?? JE hizi kauli za TUTAFANYA HIVI ZITAISHA LINI?? Maswali na majibu unayo wewe mwenyewe
11. Je Taifa kama Tanzania lipo katika njia nzuri ya kwenda au kupiga hatua katika maendeleo kwa sera hizi au mwenendo huu. Majibu unayo wewe mwenyewe.