Shoctopus
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 3,435
- 1,995
Aliyehongwa hapo ni yule anayejiita mtumishi wa Mungu. Kwa kufumbia macho uovu badala ya kuukemea.Leo Mh Rais amepewa tuzo na kanisa ambalo enzi za Lina Lazaro na Mzee Klora lilikuwa ni kanisa ambalo lilitela matumaini.
Sipingi kumpa tuzo lakini naangalia hotuba ya Askofu mkuu Bwana Mtokambali kwa kuamua kuwa sehemu ya praise timu bila kuangazia mambo ambayo katika jamii yamezorota kuliko vipindi vyote vya urais wa nchi hii.
1. Watu kupigwa risasi
2. Watu kupotea
3. Kutekwa na kuteswa
4. Kuokotwa mitaani na kwenye fukwe za baharini
Mambo hayo ndiyo kanisa lilitakiwa kuwa jicho. Hakuna nabii kwenye Biblia aliye heka na mfalme mwovu.
Tanzania Assemblies of God, mmepotoka!
View attachment 1536928
Sent from my XT1097 using JamiiForums mobile app

