Je, kanisa la mhubiri Christopher Mwakasege liko wapi?

mimi kidogo namfahamu mwakasege
Ni mnyakusa wa Tukuyu baba wa watoto wanne 3 wasichana na 1 mvulana na ni mme wa mke mmoja. Ni mtaalamu wa uchumi na mipango aliysoma chuo kikuu cha Dar. Alianza kazi kama afisa mipango ktk wilaya ya Arumeru akiishi ktk nyumba za carmatec Duluti, baadaye aliacha kazi serikalini na kujiunga na KKT makao makuu kama afisa mipango na uchumi. Miaka ya tisini alianza kufundisha mafundisho hayo ya kiroho. Kumbuka yeye ni MWALIMU sio nabii wala mchungaji, baadaye aliacha kazi KKT na kujihusisha na shughuli binafsi alifungua ofisi yake inayoitwa TASOET inayojihusisha na ushauri wa uchumi na mipango pia serikali ya awamu ya tatu kampuni hii ilikuwa miongoni mwa kampuni zilizohusika na Debt advocacy ili serikali ipunguziwe madeni. Pia amekuwa akijihusisha na uandishi wa vitabu vidogo vidogo vya mafundisho ya kiroho cha kwanza kikiwa ''Jifunze kusamehe na kusahau'' pia amekuwa akichapiza vigazeti vinavyoitwa MANA kula ukue kiroho, pamoja na uuzaji wa audio na video tapes za mahubiri yake. Amekuwa akiandaaa mikutano yake kupitia timu huru ya NEW LIFE CRUSADE COMETTEE ni timu huru kwa sababu ina wanakamati toka madhahebu yote ya kikristo ktk mikoa yote ambayo anafanya semina, mbali na maombezi semina zake zinahusu ukuaji wa kiroho na jinsi ya kuishi kama mkristo. Pia amekuwa akiandaa safari za Israel ''visit to the holy land'' pamoja na marriage retreat hukohuko. Yeye sio mchungaji na hana kanisa wala dhehebu ni muumini wa kanisa la KKKT kanisa la kijenge. Kwa sasa anaishi Njiro Redio. Hivyo ni kwa ufupi jinsi mimi nnavyomfahamu, mwalimu Christopher Mwakasege
 
mimi kidogo namfahamu mwakasege
Ni mnyakusa wa Tukuyu baba wa watoto wanne 3 wasichana na 1 mvulana na ni mme wa mke mmoja. Ni mtaalamu wa uchumi na mipango aliysoma chuo kikuu cha Dar. Alianza kazi kama afisa mipango ktk wilaya ya Arumeru akiishi ktk nyumba za carmatec Duluti, baadaye aliacha kazi serikalini na kujiunga na KKT makao makuu kama afisa mipango na uchumi. Miaka ya tisini alianza kufundisha mafundisho hayo ya kiroho. Kumbuka yeye ni MWALIMU sio nabii wala mchungaji, baadaye aliacha kazi KKT na kujihusisha na shughuli binafsi alifungua ofisi yake inayoitwa TASOET inayojihusisha na ushauri wa uchumi na mipango pia serikali ya awamu ya tatu kampuni hii ilikuwa miongoni mwa kampuni zilizohusika na Debt advocacy ili serikali ipunguziwe madeni. Pia amekuwa akijihusisha na uandishi wa vitabu vidogo vidogo vya mafundisho ya kiroho cha kwanza kikiwa ''Jifunze kusamehe na kusahau'' pia amekuwa akichapiza vigazeti vinavyoitwa MANA kula ukue kiroho, pamoja na uuzaji wa audio na video tapes za mahubiri yake. Amekuwa akiandaaa mikutano yake kupitia timu huru ya NEW LIFE CRUSADE COMETTEE ni timu huru kwa sababu ina wanakamati toka madhahebu yote ya kikristo ktk mikoa yote ambayo anafanya semina, mbali na maombezi semina zake zinahusu ukuaji wa kiroho na jinsi ya kuishi kama mkristo. Pia amekuwa akiandaa safari za Israel ''visit to the holy land'' pamoja na marriage retreat hukohuko. Yeye sio mchungaji na hana kanisa wala dhehebu ni muumini wa kanisa la KKKT kanisa la kijenge. Kwa sasa anaishi Njiro Redio. Hivyo ni kwa ufupi jinsi mimi nnavyomfahamu, mwalimu Christopher Mwakasege

pukudu umesema kweli
 
Ni mwalimu mzuri sana. Kama alivyosema member hapo huu huwa hafungmani na mkanisa haya yanayojiita ya kiroho na wala halazimishi wanaopata huduma yake kulipa mapesa kibao. Huyu si mfanya biashara kama walivyo wengine, anafundisha habari zote hata za mafungu ya kumi na halazimishi muumini kumpelekea.

Anafundisha pia kwa kutumia taaluma yake ya uchumi, ni kwa namna gani utaweza kufanikiwa, yaani kuwa mjasiriamali na mfanyakazi productive.

Anafundisha kweli hasa masuala ya ndoa. Halazimishi ndoa zilizoshindikana bali anafundisha ukweli kuhusu ndoa hizo na kama kweli zilipata kibali cha Mungu kufungwa au wana ndoa walilazimishana kuona kutokana na cirumstances na mwsihowe are incompartible??? Keep it up mwalimu Christopher and Diana Mwakasege.

:help::kev:
 
yah: Christopher Mwakasege

Mtumishi mwakasege ni kweli ameitwa na Bwana kwa utendaji wa kazi yake na mungu amekupa vitu vizuri vya kuwajenga watu katika imani na mara nyingi nimesoma masomo ya kwenye website yako mfano Roho Mtakatifu, Damu ya Yesu jinsi inavyoweza kulate upatanisho na katika maombi niliamua kufanyia kazi kweli nilipata kitu cha tofauti nanikajiona inavyotenda kazi damu ya Yesu kusema kweli ninayafurahia mafundisho na huwa napenda kila wakati kusoma. kuna somo moja linahusu habari ya kusamehe kwakweli lilinifungua sana na mpaka nilijikuta na mimi nilienda kuwafundisha wenzangu habari ya kusamehe na kupitia hivyo Mungu aliwafungua watu maana walikuwa hawajajua ni maana ya kusaheme na kama hujasamehe kuna hasara gani kubwa. mimi na sema Mungu ambariki sana na azidi kumuinua zaidi na zaidi.
 
yah: Christopher Mwakasege <BR><BR>Mtumishi mwakasege ni kweli ameitwa na Bwana kwa utendaji wa kazi yake na mungu amekupa vitu vizuri vya kuwajenga watu katika imani&nbsp; na mara nyingi nimesoma masomo ya kwenye website yako mfano Roho Mtakatifu, Damu ya Yesu jinsi inavyoweza kulate upatanisho na katika maombi niliamua kufanyia kazi kweli nilipata kitu cha tofauti nanikajiona inavyotenda kazi damu ya Yesu kusema kweli ninayafurahia mafundisho na huwa napenda kila wakati kusoma.&nbsp; kuna somo moja linahusu habari ya kusamehe kwakweli lilinifungua sana na mpaka nilijikuta na mimi nilienda kuwafundisha wenzangu habari ya kusamehe na kupitia hivyo Mungu aliwafungua watu maana walikuwa hawajajua ni maana ya kusaheme na kama hujasamehe kuna hasara gani kubwa. mimi na sema Mungu ambariki sana na azidi kumuinua zaidi na zaidi.
 
namshukuru aliyeanzisha hii topic.namkumbuka mwakasege alisoma iyunga sec --mbeya 1972--1975.baada ya hapo sikujua alielekea wapi mpaka nilipomuona kwenye tv akihubili.
 
Mwalimu Mwakasege yuko juu sana huwezi kumlinganisha na watumishi wengi kwasababu moja kubwa,hafungwi na minyororo ya madhehebu.Nimewahi kuhudhuria semina nyingi za Bwana Mwakasege sikuwahi kumsikia hata siku moja akiwaelekeza watu waende kwenye dhehebu fulani fulani.

Kuna kasoro moja kubwa ambayo nimeiona kwa Bwana Mwakasege siku za karibuni amejikita sana kuwahimiza watu kwenda Israel.Amefikia hatua ya kuandaa safari za kwenda Israel kwa wanandoa as if uponyaji unapatikana unapokwenda Israel.Bwana mwakasege ndiye aliyemshauri E Ngoyai Elowassa kwenda Israel mara baada ya kuitia hasara kubwa nchi yetu na mkataba wa RICHMOND badala ya kumshauri aombe radhi watanzania kwa uzembe anamshauri aende Israel.


Sijaona kosa la Mwakasege kushawishi watu kwenda Israel. Kwetu Wakristo Israel ni sehemu ya kwenda Hijja kama ilivyo kwa Waislam kwenda Makka. Unaposema kuwa hiyo ni kasoro ya Mwakasege ina maana unamaanisha hata Waislamu kushawishiwa kwenda Makka ni makosa
 
Huyu ni mbabaishaji tu anaepata kula yake kupitia migongo ya waliokata tamaa. Hana tofauti na kina Anthony Lusekelo na wengineo. Asanteni!
 
Back
Top Bottom