Tulizo
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 848
- 662
Wapendwa
Natumaini wote mlikuwa na weekend njema.
Hivi ulishawahijiuliza ingekuwaje kama kungekuwa na uwezekano wa kurekodi zile confessions za mapenzi, viapo vya nakupenda sana, sijiwezi juu yako n.k tunavyopeana mwanzoni mwa mahusiano? Je unadhani kama mambo yanakwenda mrama, kisha uka'iplay' that tape back...... kungekuwa na kuumizana, kuachana??
Nawaza tu kwa sauti maana mapenzi nilonayo kwa mwandani, na mahashuo nnayomuashua nahofia yasijenisuta siku moja nkijikuta namfanyia visa (MUNGU pitishia mbali) LOL.
Nakumbuka nliambiwaga .............Wallah we mwanamke nakupenda, ukijaniacha nakuua.......afu nikaachwa mie!!!!
Maisha aina yote yana stage yake... Kumbukumbu ni historia..mambo mengi yamepita na Mwenyezi Mungu ametunyima uwezo wa kutabiri na kuona yajayo ila ametupa uwezo wa kukumbuka yale mazuri yaliyopita..Hata tukiwa na huzuni ..tutaangalia kumbu kumbu na kuishia kusema..' Ni wakati wa dhahabu'.. ni historia haijirudii.