Je, huku ndiko kuokoka?

Ukiona mtu anafanya maombi binadamu mwenzake akutwe na mabaya huyo ni mpinga Kristo! Watu wanapakiwa vitu vichwani hadi wanakuwa kama vichaa! Unakuta mtu anakemea mijusi! Hivi kama ukiona mjusi kemea! paka anapita kemea! Hivi una Mungu gani? Hapo si unaishi kwa nguvu zako za kukemea kila kitu unachohisi tu!

Watu wanalazimisha sana kumsikia Roho Mtakatifu hadi shetani anawaletea sauti yake wanaishia kuamini tu na kutabiri, kuhisi kila kitu ni kibaya.

Kama wewe ni Mkatoliki ishi simple prayer life, maisha ya kisakramenti na utii kwa Kanisa! Neema ya Mungu haitakupungukia na ulinzi wa Mungu utakuwa nao bila kuhitaji kushindana hadi na mijusi!

Nafahamu yapo mamlaka tuliyopewa kama Wakristo lakini si kutumia hovyo kama vichaa! Damu ya Yesu inamwagwa hovyo hovyo tu hata mbu akikung'ata!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu aliyeokolewa harogeki.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]yaani muda mwingine unatamani hata uzabe kibao... [emoji57]

Sent using Jamii Forums mobile app
Walokole wengi siku hizi hutumia trick ya kumpumbaza mtu kwanza na kumfanya ajione hayuko salama au kufeli/matatizo yake kumeletwa na nguvu za giza. Akishakuwa kwenye hiyo hali ya wasiwasi ndiyo inakuwa rahisi kum-manipulate kadiri wanavyotaka. Jambo amablo mtu wa kawaida analiona liko wazi mtu akishakuwa kwenye hali hiyo analiona kitofauti kabisa.
 
Yaani we acha tu ndiyo maana Mimi nacheka tu...
Sawa ukipata muda uletee

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Nitumie kwa address ;
Francis Mwangomba Athumani
P.o Box 13327
Dar es Salaam

NB: Natanguliza shukrani na Mungu akubariki zaidi kwa kujitoa kwako kufanya kazi yake ya kusambaza neno lake.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nitumie kwa address ;
Francis Mwangomba Athumani
P.o Box 13327
Dar es Salaam

NB: Natanguliza shukrani na Mungu akubariki zaidi kwa kujitoa kwako kufanya kazi yake ya kusambaza neno lake.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Noted. Nitatuma mwisho wa mwezi huu.
 

"Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamwendea kwa faragha, wakisema, Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia? Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi" Mathayo 24:3-4
 
Pole sana ndugu yangu kumbe tupo wengi? Kuna ndugu yetu huwezi amini ni msomi ana masers ya IT ya mwaka 2008 hakutaka kufanya kazi alikuwa akishinda kwa mama Mchungaji wakiomba kwa mikesha tu alikonda haswa kama mgonjwa wa tb na alikuwa na nyumba anaishi peke yake kumbe alishajiandaa kutoa nyumba sadaka kwa mama Mchungaji. Kibaya zaidi akiumwa hawamtibu hadi ndugu tukaamua kufunga safari kwenda mwanza kumtoa huko kumleta Nyumbani kwa nguvu kwani alikuwa hataki kusikia habari za Nyumbani hatawazazi wake na ndugu zake wote aliwaita mapepo MTU akifa anadai ni adui yake kafa. Ndugu wakimuita au msiba ikitokea haendi ata kama ni kwao anadai mungu hajampa kibali baada ya muda tukampatia kazi simple ili afunguke akili basi akawa hatumi matumizi hata mia anapeleka sadaka zote kwa mama wakiroho . baada ya ndugu kupambana tena kwa kichapo huku wengine wakitembea kumuombea Mungu akasikia kilio chetu . hivi sasa amerudi kanisani kwake na amekusanya pesa zake amejenga na pia anatuma matumizi Nyumbani na anawatembelea ndugu zake wote kwa kweli Mungu ni muweza. Hawa wamama wa kiroho wengi ni wachawi wanawateka wasomi na kula pesa na Mali zao wanakuharibu akili unawapa hadi nyumba yako. Ndio hawa wanajiita sasa manabii kumbe matapeli. Ndugu yangu naomba pambaneni mkomboeni ndugu yenu msichoke simameni kidete hata bakora mtandikeni IPO siku mapepo yatakimbia nakuhakikishia utashinda manake ndicho kitu tulichokifanya tulitaka hadi kuchoma nyumba ya huyo Mchungaji haki vile alisalimu amri alikoma harudii. Nakutakia kila LA kheri kapambaneni baba hao manabii wengi wachawii
 
Mmh,Huyo mama kuna namna! Chunguza taratibu,huku ukinuombea Hugo ndugu yako,kakamatwa nafsi na ufahamu!! Hakuna ulokole wa hivyo!mi nimeokoka lkn hiyo nakataa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shetani muongo sana!
Muombeeni ufahamu wake,halafu iteni nafsi yake popote ilipowekwa,mtaona! Km inekamatwa mtajua
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmh,Huyo mama kuna namna! Chunguza taratibu,huku ukinuombea Hugo ndugu yako,kakamatwa nafsi na ufahamu!! Hakuna ulokole wa hivyo!mi nimeokoka lkn hiyo nakataa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo mama hana kanisa wala nini alikuwa kawateka wote watatu yani ndugu zangu wote watatu walikuwa wakiishi pamoja mmoja amechomoka kabisa mwingine naye kachomoka sasa kabaki huyu yani huyu kawa kama ndo kamkamata sana
 
Wengi tu mkuu.
naamini kila mtu keshakutana nao wateule wa bwana
Sawa basi ila ujue si kila anayedai ameokoka ni mkweli. Wengi hudhani akisali kanisa fula au akizaliwa damilia wazazi wameokoka na yeye anakuwa automagically. Wengine ni matapeli na wengine ni watapeliwa.

Una hakika walikuwa wameokoka? Unayoyasema hayafanani na wokovu...
 
2Corinth..5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
Therefore if any man be in Christ, he is a new creature: old things are passed away; behold, all things are become new.

Huo ndiyo wokovu wa kweli, mwingine ni bandia.
 
Nyie mnaokejeli walokole Mungu atawakana kama mnavyomkana hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…