Je, hii ina madhara gani katika mahusiano?

Je, hii ina madhara gani katika mahusiano?

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
21,569
Reaction score
28,486
Habari wanaJukwaa pendwa MMU,

Nipo mbele yenu siyo kuhukumiwa bali kuomba ushauri kwa hili jambo ninaloliteta mbele yenu.Nina mpenzi wangu ambaye nimedumu naye katika mahusiano yapata miaka mitatu sasa, katika harakati za kutafuta maisha imetokea tukawa tunaishi mikoa miwili tofauti ila ninapopata likizo ya majukumu huwa tunakutana.

Mimi kuna wakati maisha yananipiga nakuwa sina hela kabisa na wakati mwingine madeni kuniandama sana, kuna wakati huwa namshirikisha huyu mpenzi wangu hali halisi ya mimi kuishiwa hela na bila hiyana huniuliza " Unadaiwa Kiasi gani au nikusaidie kiasi gani mpenzi" ? Kiukweli aibu hunijaa ghafla na kuanza kujiuliza nimuambie kiasi gani? Lakini huwa namtajia kiasi halisi ninachokuwa nakihitaji na bila hiyana huniambia " basi usijali nitakutumia" Punde nashangaa Tigo Pesa inasoma salio. Dah!!

Wakuu siyo mara ya kwanza kumuomba anisaidie hela huyu mpenzi wangu na mimi hata siku moja hajawahi kuniomba hata shilingi mia ingawa nafahamu yeye anaishi maisha ya kawaida tu na hajawahi kuniambia nimrejeshee hela anazonisaidia hata siku moja na wakati nikijaribu kufanya hivyo hunikatalia. Mungu akipenda tuna mipango ya kuanzisha familia lakini wakuu naombeni mnipe ushauri.

Hivi suala la mpenzi wangu kunisaidia fedha mara kadhaa ninapokuwa na uhitaji linaweza kuvuruga mahusiano yetu?



Nawasilisha
 
Ukisikia kuhongwa ndio huko
hakuna maana nyingine ya kuhongwa mbali na hiyo
 
Sisi wanaume sijui hata tunataka nn,tukiombwa sie tunalalamika mpaka baasi tukiomba sie tunajiuliza!kama unamashaka basi usimwambiege shida zako.vingininevyo we muamini tu kwani imanai inajenga ukumwamini kwa mtazamo hasi mara nyingi huwa hivyo na kwa mtazamo chana huwa hivyo pia. Ushauri wangu usiichelewe hio ndoa huyo ni mke mwema na anaekujali wahi kabla ya wanaume wa shoka hawajakuwahi.
 
usiendekeze kupewa pewa mkuu, unajua anakozitoa?
 
Sisi wanaume sijui hata tunataka nn,tukiombwa sie tunalalamika mpaka baasi tukiomba sie tunajiuliza!kama unamashaka basi usimwambiege shida zako.vingininevyo we muamini tu kwani imanai inajenga ukumwamini kwa mtazamo hasi mara nyingi huwa hivyo na kwa mtazamo chana huwa hivyo pia. Ushauri wangu usiichelewe hio ndoa huyo ni mke mwema na anaekujali wahi kabla ya wanaume wa shoka hawajakuwahi.

Ahsante kwa ushauri mkuu,..
 
Siku akikuomba yeye...mlio wake utakuwa ni mamilioni na hapo ndo utakuwa mwisho wenu,kwa kuwa hautomudu!
 
Siku akikuomba yeye...mlio wake utakuwa ni mamilioni na hapo ndo utakuwa mwisho wenu,kwa kuwa hautomudu!

Duh, anafahamu hali yangu halisi kuhusiana na kipato mkuu.....
 
What did you heard Sir..

What did you "heard" aibu mie naona.
Tutumie lugha zetu.

Khs kukupa hela mi sioni shida kwa kuwa ulishamueleza hali yako akakupenda basi no problem. Sikiliza roho yako inasemaje ndani mwako
 
What did you "heard" aibu mie naona.
Tutumie lugha zetu.

Khs kukupa hela mi sioni shida kwa kuwa ulishamueleza hali yako akakupenda basi no problem. Sikiliza roho yako inasemaje ndani mwako


Nashukuru kwa ushauri, just ignore the rest, hizi ni lugha za watu mkuu...
 
mkuu mademu wa dizaini hizo wachache sana aisee..haijalishi hiyo pesa anayokupa inatoka wapi..ila mpaka kufanya hivyo ina maana anakupenda..so usimwangushe..cha msingi ni ww kuchakarika mzee..usiridhike kuwa tegemezi..mbebaji nae huchoka
 
Anafaa na ni wife material but kuwa na plan B..? I mean jee ukijua kuwa anahudumiwa na bwana mwngne utaendelea kumpenda na kumvumilia mkuu..!
 
Back
Top Bottom